bakuza
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 492
- 104
Ndani ya rasimu hii tumeingiziwa serikali tatu yaani Ya Tanganyika,Zanzibar na ya Muungano,na mpaka sasa Zanzibar wanayo katiba yao kwa sasa tunahangaikia ya katiba ya Muungano ambayo itakamilika Mungu akijaalia mwaka 2014 na Uchaguzi mkuu ni 2015.Je uchaguzi utafanyika bila Katiba ya Tanganyika?Na kama tukianza maandalizi ya katiba ya Tanganyika hiyo miezi kadhaa itatosha kuikamilisha?
Na je nini kilitakiwa kuanza kati ya katiba ya Muungano na katiba za nchi zinazoungana? Tumeingiziwa Serikali tatu makusudi ku buy time ili uchaguzi upite..Haiingii akilini kuwa Wasomi wetu wote ndani ya Tume hawakuyaona haya… Kwa uelewa wa kawaida tu ni kuwa hata katiba ya Zanzibar lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na katiba ya Muungano endapo Muundo wa muungano unabadilika.
Watanzania ondoeni matumaini ya kupata suruhisho la kikatiba mwaka 2014 kwa kuitegemea rasimu hii yenye baadhi ya mambo mazuri ya kutupumbaza ili mambo yaendelee kama wapangavyo,wanasiasa wanaangalia faida yao kisiasa na si taifa na watu wake.
Kuna mapungufu Mengi ndani ya rasmu hii yatupasa tupitie kwa utulivu na tutajifunza mengi.
Muda utaamua...
Na je nini kilitakiwa kuanza kati ya katiba ya Muungano na katiba za nchi zinazoungana? Tumeingiziwa Serikali tatu makusudi ku buy time ili uchaguzi upite..Haiingii akilini kuwa Wasomi wetu wote ndani ya Tume hawakuyaona haya… Kwa uelewa wa kawaida tu ni kuwa hata katiba ya Zanzibar lazima ifanyiwe marekebisho ili kuendana na katiba ya Muungano endapo Muundo wa muungano unabadilika.
Watanzania ondoeni matumaini ya kupata suruhisho la kikatiba mwaka 2014 kwa kuitegemea rasimu hii yenye baadhi ya mambo mazuri ya kutupumbaza ili mambo yaendelee kama wapangavyo,wanasiasa wanaangalia faida yao kisiasa na si taifa na watu wake.
Kuna mapungufu Mengi ndani ya rasmu hii yatupasa tupitie kwa utulivu na tutajifunza mengi.
Muda utaamua...