Tanzania yapata Sh trilioni 1 kufadhili programu za kilimo

Huyu mama akili yake yote ni kupewa vya bure na mikopo! Ikifikia kulipwa atakuwa na umri wa miaka 80
Hebu mshauri hapa pahala pa kupata fedha ili tupige hatua,maana hakuna serikali iliyofadhiliwa kuliko ya awamu ya kwanza,Sasa nadhani hakuna njia nyingine maana wote wamepita hiyohiyo
 
Upo tayari kuchangia buku kila wiki kwenye mfuko wa serikali wa kujinasua na mikopo!?
 
Nani akamsikilize msomali ache kusaidia ndugu zake Mogadishu aje kumsaidia mkulima wa Tanzania?

Huko kwenye ubaguzi hunipeleki. Ukimsikiliza usimsikilize zote ni haki zako.

Tupo wengi sana tunamsikiliza na tunamuelewa ingawa anaongea na sisi Kisomali.

Labda huelewi mimi ni Muislam, Kiislam kubaguwana kwa rangi, kabila, dini ni haram. Mbora kati yetu kwa Mwenyezi Mungu ni mcha Mungu.
 
Mwigulu 'atatuua' na haya madeni!
Anachotakiwa sasa hivi kukifanya ni kuzungumza na wakopeshaji wafanye debt restructuring ili pesa za kigeni tutakazo ziokoa zitumike kwenye kulipia bidhaa na huduma wakati huu wa uhitaji mkubwa wa pesa za kigeni.
Mwigulu anatakiwa aache kuwaza urais kwa sasa 🤣🤣🤣, 'ahamie' Ulaya na Marekani kuhakikisha tunapata debt relief ili tuweze 'kuokoa' hizi Dollar.
 
Hii ndo Habari ambayo huwa mnapenda sana kutangaza kwenye TV wiki nzima

Kwamba jamani tumejaaa mihela ni aibu kwa taifa badala ya kuhimiza uwajibikaji

Hii ina faida gani kwa raia wakati inishia kwa viongozi?
 
Watazihamisha ...matumizi....tunawajuaa
 
FaizaFoxy Tangu lini nawewe Umekuwa zuzu?
Unakuja na Kilimo tena?
Umeachana na Udini?
Au kwakuwa Rais mwendazake alikuwa Mkristo UKAWA UNA MPINGA?
ama kweli, dunia duara
 
Upo tayari kuchangia buku kila wiki kwenye mfuko wa serikali wa kujinasua na mikopo!?
Ndiyo, kikubwa serikali iweke mazingira ya Mimi kupata zaidi ya hiyo 1000 ili niweze kupitia hiyo 1000. Ni Rahisi kabisa.
 
Hii scheme ya kilimo ni jambo la maana sana na ni mpango ambao utawakomboa vijana wengi wa kitanzania. Kwa hili ninampa pongezi nyingi sana Mh. Rais Mama yetu SSH na pia Mh. Bashe.

Kasoro niliyoiona mimi na haya ni mawazo yangu, ni kufanya scheme ya makundi. Jambo lolote lenye dhana ya ushirika huwa haliendi sawa sawa na ni rahisi sana kufa au kwenda kwa kusua sua. Hili lilitakiwa Serikali iweke miundombinu yote wezeshi kisha kila kijana apewe/akodishiwe sehemu yake na kila mmoja apewe targets. Kwamba wakivuna na wakishauza watarejesha kiasi kwenye Mfuko wa Serikali ili fedha hizo ziwasaidie vijana wengine. Ushirika wa namna ilivyo sasa kufeli ni rahisi kwasababu sio vijana wote wana passion ya kilimo na wengine watategeana. Refer masuala ya Ujamaa na Ubepari mtanielewa vizuri.
 
Wanafundishwa ki makundi lakini kila mmoja anawezeshwa kivyake. Hilo waliliona mapema.
 
Kwajinsi serikali hii inavyo nuka rushwa, hiyo hela watagawana Mwigulu na Samia wallahi
 
Kwajinsi serikali hii inavyo nuka rushwa, hiyo hela watagawana Mwigulu na Samia wallahi

Na vile visima 67,000 utavilipia wewe kuchimbwa kwake, au siyo?
 
Haya mambo makubwa anayo yafanya mama kwa masilahi ya wananchi ndio yanawakera sana na kuumiza nyoyo za baadhi ya watu wachache.
Walitegemea kuwa hatoweza lkn kwa uwezo wa Mungu anasonga mbele tena kwa mafanikio makubwa.
Mungu aiendelee kumlinda.
 
Pamoja na andishi refu la kuchusha, kaa ukijua kwamba hela zote zitaingia kwenye mifuko ya mafisadi na hakuna lolote la maana kwenye kilimo litakachotekelezwa kwa ufanisi.
 
Pamoja na andishi refu la kuchusha, kaa ukijua kwamba hela zote zitaingia kwenye mifuko ya mafisadi na hakuna lolote la maana kwenye kilimo litakachotekelezwa kwa ufanisi.
Linalochusha linajibiwa?

Hakunabutabiri hapa, vitu vipo live. Wewe utabiri wako peleka kwa wajinga ndiyo waliwao.

Vijana batch ya kwanza saa hizi wapo mashambani wameshaanza kutengeneza pesa.

BBT imeshaanza iuzalisha ma CEO wapya, vijana wadogo kabisa. hujawaona juzi kwenye kongamano?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…