#COVID19 Tanzania yapokea Dozi za Chanjo ya Moderna

#COVID19 Tanzania yapokea Dozi za Chanjo ya Moderna

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Waziri wa Afya Dkt.Dorothy Gwajima, amepokea Chanjo za Moderna chini ya Mpango wa COVAX hii ikiwa ni Awamu ya Kwanza kwa aina hii ya Chanjo kuingia nchini kiasi cha dozi 376,320 ambazo zitatumika kuchanja wananchi 188,160.

"Tumepokea chanjo aina ya Moderna kupitia mpango wa COVAX jumla ya dozi 376,320 ambazo zitatumika kuchanja wanachi 188,160, nichukue fursa hii kuishukuru mpango wa COVAX na hii ikiwa ni awamu ya kwanza kwa aina hii ya chanjo kuingia nchini kupitia mpango wa COVAX"

"Mapokezi ya chanjo hizi za leo yanafanya jumla ya chanjo tulizopokea nchini tangu tuanze kutoa chanjo dhidi ya UVIKO 19 hadi sasa kuwa dozi 6,408,950 zikijumuisha (Sinopharm, Janssen na Pfizer), ambazo zinatosha kuchanja jumla ya watanzania 3,204,475"

"Serikali itaendelea kutoa Chanjo dhidi ya UVIKO-19 katika vituo mbalimbali vya Afya hapa nchini kwa mujibu wa miongozo iliyopo, hivyo niwaombe wanaohusika na zoezi hilo kuwajibika kwa kasi kubwa ili kuwawezesha watanzania wengi kupata chanjo mapema iwezekanavyo, Wizara ilitoa Mwongozo wa Chanjo unaofafanua vyema taratibu za utoaji wa chanjo hizi wenye lengo la kufikia uchanjaji wa asilimia 60 ya watanzania"


MillardAyoUPDATES
 
mi mwenyewe siwezi kukaa karibu na mtu aliyechanja kwa muda murefu maana najua muda wowote kuna hatari ya kugeuka zombi...
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23]
 
Korona na chanjo vinatumika kwa nia ovu na waabudu shetani dhidi ya ubinadamu........ni Mungu Mwenyezi pekee ndo anaingilia kati ndo maana unaona mipango yao ya gizani inavurugika.
 
mi mwenyewe siwezi kukaa karibu na mtu aliyechanja kwa muda murefu maana najua muda wowote kuna hatari ya kugeuka zombi...
Unatushauri sisi ambao atutaki kuchanjwa tutembee na silah kujiami na Zombies.
 
Naumwa mafua,homa pia,lakini mmmmh! nina hofu ya kuchanjwa
 
Walete walete ila watoe maelezo yaliyonyooka chanjo ni kinga au inasaidia unapopata ugonjwa usiumwe sana?

Bado nabaki na msimamo wangu wa kutochanja mpaka nijiridhishe.
Haya yanaonekana ni maandalizi tu , naamini wote waislam na wakeisto tunaamini juu ya kiama, huku kuna mpinga Kristo huku kuna nabii dajal lakini theme ni ileile, so kwa wasiotaka kuchanja naamini muda wa shurti ni bado, ipo siku ila bado, haya ni maandalizi, they are setting things ready for action,
 
Back
Top Bottom