Tanzania yashika nafasi ya pili Afrika kwa ukuaji wa uchumi

MUUZA NGADA

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2018
Posts
340
Reaction score
497
Leo March 16, 2018 Jarida maarufu la Business Chief limeitaja Tanzania kama taifa la pili lenye uchumi unaokuwa kwa kasi zaidi barani Africa. Tanzania uchumi wake unakua kwa asilimia 7 imeshika nafasi ya pili nyuma ya Ivory Cost ambayo uchumi wake unakuwa kwa asilimia 8.5.

Orodha hiyo inayotangazwa kila mwaka, imesheheni mataifa ya Africa mashariki kwani ndio ukanda ambao umetajwa kuwa na uchumi unaokuwa kwa kasi, huku kilimo, utalii, usafiri, mawasiliano na biashara zikitajwa kama sekta zinazotazamwa na kuingiza vipato vikubwa

Source : MillardAyo
 
Kwa awamu hii tunatatizo kubwa la takwimu zisizo sahihi, hii takwimu yaweza kuwa sahihi au batili, ila cha msingi ni kuwa haina msaada kwangu so napita tu...
 

hakuna hicho ulichosema

African Business Chief - African Business Magazine & Website - African Business News
 
Mleta mada kwa akili za kawaida unaona uchumi umekuwa ?!!. Aina hii ya uchumi ndiyo tunayotarajia ?!! Poor Tz
 
Habari mbaya kwa bavicha! Itabidi wakashitaki kwa da mange .. ficha id yangu please
 
Uchumi usiogusa maisha ya raia hauna maana kabisa.. Ukuaji wa uchumi lazima uendane na mabadiliko chanya kwenye maisha ya wananchi
 
Habari mbaya Kwa wana ukawa
Na nni mbaya zaidi kwa Wapenda ukweli wote!! Pia ni habari njema sana kwa wanaopenda kudanganywa! Hilo gazeti ni la mtaa gani kwanza? Kwenye issue za uchumi tunaliamini kabisa Economist!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…