Tanzania Yashinda Tuzo 4 za World Travel Awards

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Eneo Bora la Utalii Afrika (Tanzania)

Bodi Bora ya Utalli Afrika (TTB),

Hifadhi Bora ya Afrika (Serengeti),

Kivutio Bora cha Utalii Afrika (Mlima Kilimanjaro).
Tanzania imenyakua tuzo 4 katika Tuzo za Utalii zinazotolewa na World Travel Awards na Marekani, usiku wa kuamkia Oktoba 19, 2024.

Tuzo hizi zimetolewa jijini Nairobi nchini Kenya, huku Serengeti ikiendelea kuwa Hifadhi Bora ya Afrika kwa miaka sita mfululizo (2019, 2020, 2021, 2022, 2023, na 2024), pia Bodi ya Utalii Tanzania imekuwa Bora Afrika kwa miaka mitatu mfululizo (2022, 2023, na 2024).

Aidha, Tuzo za World Travel zilianzishwa mwaka 1993 kwa lengo la kutambua, kutunza, na kusherehekea ubora katika sekta.
 
Ni habari njema kwetu, tutegemee watalii zaidi, bado tuzo ya filam bora ya utalii iende kwa Royal tour tufunge hesabu.
 
Hongera kwetu
 
Your browser is not able to display this video.
 
Nimebahatika kufika serengeti & Kilimanjaro. Kiukweli tukiamua tunaweza kupiga pesa nyingi sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…