Tanzania yatia aibu huko Olympic

The Genius

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2018
Posts
822
Reaction score
2,095
Picha hizi mbili zimepigwa jana tarehe 23 Julai 2021 wakati wa tukio la ufunguzi wa michezo ya Olimpiki jijini Tokyo, Japan.

Ki-utaratibu, kila nchi iliyopeleka wawakilishi inatajwa halafu wawakilishi wanapita mbele ya umati wakiwa na bendera ya taifa lao. Kutakuwa na jumla ya matukio 339, kwa aina za michezo 33, kwa namna 46

Picha ya juu ni tukio baada ya Tanzania kutajwa. Wawakilishi wa Tanzania ni watatu tu, lakini hawakuwepo. Hapa alionekana mtu mmoja mwenye asili ya Asia akipeperusha bendera ya Tanzania kama mwakilishi wa nchi yetu.
Picha ya chini ni tukio baada ya Kenya kutajwa.

Jumla ya wanamichezo 11,091 kutoka nchi 206 duniani watashindana kupata medali za dhahabu, fedha au shaba. Zipo nchi zimepeleka wanamichezo 100+, 200+, 400+ hadi 600+

Tanzania, nchi yenye watu takribani milioni 60, na asilimia zaidi ya 90 wapo chini ya miaka 35, umri wa michezo, imepeleka wawakilishi watatiu, ambao hawajaonekana wakati nchi yao ikitajwa.

Vijana wamebaki ndani ya nchi yao wanacheza ndondo, kubeti, singeri na kuuza karanga. Viongozi wao hawajali! Maneno mengi ya kutia matumaini yanasemwa majukwaani, vijana wanakubali bila kufikiri, na akili ya kudai hawana. Wamefungwa akili, wanaamini Mungu ndiye aliyewapangia kuwa kama walivyo, siku yao itakuja... miaka mia ijayo.

Ni nani mwenye akili ya kupunguza tatizo la ajira kwa vijana kwa kuboresha sekta ya michezo na kuiunganisha nchi na jumuia za michezo za kimataifa? Hakuna. Kuna wizara ya michezo? Ipoipo tu.

Tuendelee na masiasa yetu ya kuumizana, ndicho tunachoweza.
 
Utasikia nchi yetu ina amani na utulivu na maigizo kibao,sasa sijui hiyo amani na utulivu vinatusaidia nini! Nchi hadi leo ni masikini,elimu mbovu, huduma za afya mbovu yaani hadi mtu unajiuliza tuna laana gani!
 
Ina maana hadi leo hujui kuwa Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu?

Ni nchi gani nyingine duniani kwa mfano ambapo katikati ya mapambano dhidi ya Corona ambayo yanakataza msongamano wa watu,waziri wa afya anaitisha tangazo la kuita umati wa watu ili kutengeneza msongamano wa kwenda kupokea chanjo airport?
 

Masai nayenyewe imefika tokyo, imevaa na barakoa 😂😂😂😂
 
[emoji3059][emoji3059][emoji3059][emoji3059] inasikitisha lakini ndivyo ilivyo, watanzania wenye asili ya ki Asia ndio WAZALENDO kuliko sisi asilia.
Mfano kodi hii ya miamala ya simu A.K.A "YAKIZALENDO" inayotukosesha raha, mgunduzi wake ni mbunge mtanzania mwenye asili ya kiasia Zungu.
 
unamaaanisha wafaransa na timu yao ya taifa ya mpira wanatia aibu?
 
... yule mwarabu koko? Katuumiza kweli kweli!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…