TANZIA: Gavana wa Nyeri nchini Kenya Wahome Gakuru afariki kwa ajali ya gari

mwathadan

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2016
Posts
3,136
Reaction score
4,271
Nyeri Governor Wahome Gakuru has died.
Mr Gakuru was involved in a freak road accident on Tuesday morning after his car rammed into a barrier along Thika road at Makenji, Muranga County.
He was rushed to Thika Level 5 hospital awaiting a transfer to a Nairobi Hospital but succumbed to his injuries.
His driver and bodyguard were also seriously injured in the accident.
Earlier this year, another Nyeri Governor Nderitu Gachagua passed on while receiving treatment at a London Hospital.
 
Nyeri Governor Wahome Gakuru has died.

Mr Gakuru was involved in a freak road accident on Tuesday morning after his car rammed into a barrier along Thika road at Makenji, Muranga County.
He was rushed to Thika Level 5 hospital awaiting a transfer to a Nairobi Hospital but succumbed to his injuries.

His driver and bodyguard were also seriously injured in the accident.
Earlier this year, another Nyeri Governor Nderitu Gachagua passed on while receiving treatment at a London Hospital.



 
Gavana wa Kaunti ya Nyeri nchini Kenya, Dr. Wahome Gakuru, amefariki mapema leo Jumanne kufuatia ajali mbaya ya barabarani katika eneo la Kabati, katika barabara kuu ya Thika-Sagana katika Kaunti ya Murang'a.

Alikimbizwa katika Hospitali ya Thika Level 5 kwa matibabu ya dharura lakini akaaga dunia.

Kamishna wa Kaunti Murang'a John Elungata alithibitisha kifo cha hicho.

Bwana Elungata alisema kuwa Kabati ni eneo hatari sana na madereva hukosa mwelekeo kila mvua inaponyesha.

Maafisa wa polisi wamesema kuwa gari la Gavana huyo lilikuwa na abiria wanne wakati wa ajali hiyo, akiwemo msaidizi wake wa kibinafsi, mlinzi wake na dereva.

Mkono na mguu wa msaidizi wake wa kibinafsi ilivyunjika huku miguu ya msaidizi wake ikijeruhiwa vibaya huku dereva akidaiwa kuwa katika hali nzuri.

Polisi wanasema kuwa ajali hiyo ilitokea baada ya gurudumo moja la gari hilo kupasuka wakati mvua kali ilipokuwa ikinyesha.

Mwili wa Gavana huyo umesafirishwa hadi katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Lee mjini Nairobi.

Inadaiwa kuwa Gavana huyo alikuwa akielekea kuhudhuria kipindi kimoja cha redio na runinga wakati gari lake lilipokumbwa na ajali hiyo.

Dr. Gakuru ni Gavana wa pili wa Nyeri kufariki dunia wakati yupo madarakani baada ya Gavana Nderitu Gachagua kufariki mwezi Februari mwaka huu.
 
Haihitaji rocket science kuona mwanga ulioko humo na likely dereva hakufariki,R.I.P Gavana,vyyuma vimeingilia upande aliokaa!!
 
Haihitaji rocket science kuona mwanga ulioko humo na likely dereva hakufariki,R.I.P Gavana,vyyuma vimeingilia upande aliokaa!!
Inasikitisha sana kifo chake. Pole kwa waathiriwa wa mkasa huo wa ajali mbaya.
 
Duh, poleni kwa waliopoteza ndugu. Kifo ni kitu kibaya sana.
 
Hii GIKUYU wacha iende tu, amfuate GACHAGUA
 
kwan alizungumza nini kuhu raila? Mganga ni hatari sana
 
Inasikitisha..kiongoz umetangulia mbele za haki...ndio njia ya waja tofauti ni kwamba siku zetu za mauko hutofautiana tu! Poleni sana familia ndugu ,marafiki na taifa kwa jumla.Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi
 
Tbc wanasema Dereva kafariki ila kuna watu wawili mbali na dereva ndio majeruhi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…