Mzee wa Rula
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 8,169
- 3,351
Inna Lillahi Wa-Inna Illaihir Rajiuun!!
Bwana alitoa, Bwana ametwaa, Mapenzi ya Bwana yatimizwe.
Pole sana ndugu yangu LiverpoolFC Mungu akutie nguvu ya uvumilivu kwa wakati huu mgumu wa uzuni, narudia tena pole saana wewe na mama mzazi wa mtoto!!!!!!!!!!WanaJF,
Napenda kuchukua fursa hii kuwajuza kuwa mwanaJF mwenzetu aitwaye LiverpoolFC amefiwa na mwanae mchanga leo asubuhi muda wa saa tatu na nusu.
Taarifa ilichelewa kitufikia kidogo lakini naomba wote kwa ujumla wetu kuelewa juu ya tukio la huzuni lililomkumba mwenzetu.
Mazishi yameshafanyika leo tarehe 13.12.2011.
LiverpoolFC binafsi nakupa pole mkuu, nakuomba uwe mvulivu na mtulivu katika kipindi hiki kigumu sana ulichonacho. Zidi kumuomba Mungu, zidi kumtukuza Bwana maana sote ni wake. Narudia tena pole sana mkuu.
Pole sana ndugu yangu LiverpoolFC Mungu akutie nguvu ya uvumilivu kwa wakati huu mgumu wa uzuni, narudia tena pole saana wewe na mama mzazi wa mtoto!!!!!!!!!!
Inna li Llahi wa Inna iLlahi Rajiun.
Kila msiba wa kifo huwa ni mawaidha kwa tulio hai. Hakuna umri, si ujana si uzee, si mtoto si mkubwa, kifo kinaweza kumjia yoyote wakati wowote, tuhimizane kutenda mema.
Pole sana LiverpoolFc na wote.
Nakuombea ujasiri kipindi hiki kigumu.
Ni kazi ya Mola