TANZIA: Papa Baupa Diop afariki Dunia

Yani mkuu bado habari za Mungu wetu hazina mashiko kwako?

Siyo kwangu tu. Hata kwako.

Zikiwa na mashiko hizo si za Mungu tena.

Zinaenda kwenye falsafa, sayansi, historia, anthropojia etc.

Hata kama hujui hilo.

Mungu hadithi yake by definition anatakiwa akuache kwenye mataa humuelewielewi, sasa habari ambazo hazielewekieleweki zitakuwaje na mashiko?

Ukishaona zina mashiko ushazielewa.

Ukishazielewa tu, huyo si Mungu.

Ndiyo maana waliotunga hizo hadithi wamejiwekea insurance policy kwa kusema "the lord works in mysterious ways".

Wanajua wakishakukubalisha hivyo, wanaweza kukujaza ujinga wowote.

Ukiuliza swali ambalo halina jibu, utaambiwa tu "the lord works in mysterious ways".
 
Mkuu...

.hivi sisi tulioamua kumuamudu Huyu Mungu wetu mmoja na wale wazee wa zamani walio abudu Miungu ya miti,wanyama na masanamu unaweza kututofautisha vipi kwa misingi ya hicho unacho kiamini.
 
Roman Catholic wana imani za ajabu sana.

Anyway this is life.
Ukisikia wendawazimu ndio huu,ya waroma yanakuhusu nini hata yakukere?
ninyi ndio wale wajinga mnaong'atwa na nyoka badala yakuwahi tiba mnakimbilia maombi mwisho wa siku mnakufa kizembe,
Ninyi ndio wale mnaongizwa kwenye ugaidi huku mkifundishwa ukiua kafiri basi wewe ni moja kwa moja peponi.
Nasisitiza fuatilia mambo ya dhehebu lako ya waroma hayakuhusu.
 
Mkuu...

.hivi sisi tulioamua kumuamudu Huyu Mungu wetu mmoja na wale wazee wa zamani walio abudu Miungu ya miti,wanyama na masanamu unaweza kututofautisha vipi kwa misingi ya hicho unacho kiamini.

Kwanza, siongelei ninachokiamini tu.
Naongelea zaidi ya kuamini tu. Naongelea documented facts.

Pili, wale watu wa zamani walioabudu miti na wanyama, kwa kulinganisha elimu ya wakati ule na ya sasa, walikuwa na maarifa fulani ya asili kuliko watu wa sasa wanaoamini Mungu asiyeonekana wala kuthibitishika.

Nitakupa mfano, watu walioabudu miti kama Mungu, kwa kujua au kutojua, imani yao iliendana na uanamazingira. Walitunza mazingira kwa kutokata miti, na hilo liliwasaidia kupata mvua.

Waliishi an environmentally sustainable life mostly.

Leo dini zinatuambiaje? Ukristo kwa nfano unasema zaeni muongezeke mkaitawale dunia na vilivyomo. Si mtunze mazingira ku balance maisha kati yenu na nature, watu waneambiwa watawale mazingira. Na humo humonunaoenyezwa ujinga wa kuwafanya watu watumwa kwa sababu hawa si Wakristo au hawa ni makafiri. Ujinga mtupu.

Matokeo yake watu leo wamekata miti mingi sana, wameharibu mazingira. Huu ni mfano mmoja tu.

Mvua hazinyeshi, joto linazidi.

Sasa, ukiwaweka wale watu wa zamani kwenye mizani ya cross multiplication, kiasi kidogo walichojua na walivyoishi bila kuharibu mazingira, na watu wa sasa wanaojua mengi na kuharibu mazingira, watu wa leo wanapwaya.

Ingawa wote wapo katika kundi moja la kuamini supernatural powers bila ushahidi.
 
Mkuu ,Acha niendelee kukufuatilia. Naona kamavile kuna madini nayapata aisee.[emoji848]
 
Terms and Conditions za JF haziruhusu hii lugha. CC Moderator


That's a part of Quran verse. The Quran is written in Arabic.

You needed to ask for the translation of the words.
Hizi lugha za jangwani hizi.

R. I. P


Unashangaa lugha ya jangwani, mbona hushangai hicho kilemba ulichovaa??!!--- angalia Avatar yako hicho ni kilemba cha ulaya, Afrika au jangwani???, Nyani haoni kundule 🤣🤣.
 
Dah jamaa alikuwa tafu sana kiungo pale alifunga goli pia kwenye mechi na uturuki ya 3 kwa 3 nadhani iliisha kwenye makundi yaani Rest In Peace Mwamba
Nop ilikuwa n.....Uruguay vs Senegal group stage.
 
Figisu?.Vipi kuhusu Ghana Vs Uruguay kombe la dunia la South Afrika 2010.Gyan angepata ile penati,wangewazuia vipi kuingia nusu fainali?.Tupunguze kujiona wanyonge mkuu.Mtazamo hatari sana huu kwa afya ya Afrika.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Mwamba wa Senegal anasawazisha magoli ya kisukari kupanda
 
That's a part of Quran verse. The Quran is written in Arabic.

You needed to ask for the translation of the words.
We don't need to find or ask for translation here in JF. It has been declared that Only English and Swahili Shall be used in this Platform.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…