LiverpoolFC
JF-Expert Member
- Apr 12, 2011
- 11,483
- 3,369
Ndg zangu WanaJF! Hili nimependa niwajuze tu! Yule Mmasai aliyekuwa anatangaza bia ya kampuni ya TBL kwa kutoa advertise ya kukimbia na kutaka kuruka mto na kudondosha kizibo cha bia ya safari lager amefariki dunia leo alfajiri ktk hosptal ya Tank la maji hapa Arusha mjini,kilichonigusa sana ni familia yake kulia kwa uchungu makubwa ila hakika MUNGU alimpenda zaidi. Ndipo nikakumbuka alivyokuwa akiadvertise ile tangazo la safari ni safari na nikajiuliza, Je? Kampuni ya TBL itashughulika na chochote kama watapata taarifa hii nzito ya msiba? Hayo nimeyakuta leo nilipofika pale hosptalini lakini ina machungu sana. Marehemu Meshiliek Lendwala Mollel amekutwa na mauti baada ya kuugua kwa muda mfupi sana na ameacha wake wawili na watoto! Na mpango wa mzishi inaandaliwa pale Dukabovu wilaya ya Monduli post kbs na pale kile kitengo cha nyoka maarufu hapa Arusha kuitwa Snake Park. Bwana ametoa na Bwana ametwaa! Jina lake lihimidiwe sasa na hata milele! Amen!