Tanzia.

Pretty R.

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2012
Posts
200
Reaction score
31
Kuna habari za kusikitisha kwamba MARIAM KHAMIS amefariki dunia wakati wa kujifungua katika hospitali ya Muhimbili na mtoto amebaki mzima. Marehemu alikuwa star wa muziki wa taarabu kama "paka mapepe", "sitishiki na lawama zenu" na zingine kibao. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Ameeen.
 
Breaking News: Msanii wa taarab nchini Tanzania wa kundi la TOT plus, Mariam Khamis maarufu kama paka mapepe amefariki dunia usiku wa jana kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam mara tu baada ya kujifungua .

Mariam Khamis umauti umemkumba akiwa anaimba kundi la TOT plus lakini enzi za uhai wake aliwahi kuimbia katika makundi mbalimbali ya taarab likiwemo East Africa Melody, Zanzibar Stars na 5 Stars.

Khamis Muhidini Shomary baba wa marehemu amesema mipango ya mazishi inaendelea kufanyika ambapo anatarajiwa kuzikwa hapo kesho Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.
 
Inna lillah wa Inna illah rajiun!
 
R.I.P

 
Last edited by a moderator:
Nikiwa kama mdau, mpenzi na mshabiki wa taarab, Sio siri Mwenzenu nimesikitika sana tena sana tu zaidi ya sana!! Kiukweli ule wimbo wa paka mapepe, Dada Mariam alikamua vilivyo. Naupenda sana ule wimbo. Ndo ivo jamani, "Dunia mti mkavu, viumbe tusiegemee!"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…