Taratibu za KUANZISHA gazeti ni zipi?

Mshinga

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
3,532
Reaction score
1,126
Ukitaka kuanzisha gazeti nchini ni zipi taratibu zinazohitajika?
1.Gharama za uanzishaji kwa makadirio
2.Pia mtaji angalau inahitajika kiasi gani
3.je inawekana kuwa na gazeti linalotumia mitambo ya kukodi kabla hujanunua mitambo yako?
 
Nenda Idara ya Habari na maelezo (msajili wa Magazeti) hapo utapewa Fomu kwa ajili ya maelekezo ya usajili.
1. Unapaswa kuwa na hati ya usajili wa Kampuni itakayoendesha bishara hiyo ya Gazeti.
2. CV's za Director wa Kampuni hiyo,
3. CV's za Editor wako na waandishi 10
4. Bank Statement ya A/C ya kampuni yako ikionyesha uwezo wako wa Mtaji
5. Location ya ofisi
6. Publisher wa Magazeti yako, hapa anaweza kuwa ni kampuni namba 1,
7. Baada ya kukamilisha kwa msajili wa Magazeti utakwenda Maktaba kuandikisha ambako utapata ISSN namba.
8. utaandikisha Posta

Hayo yanaweza kusaidia ila gharama zimeandikwa kwenye Fomu utakapozichukua Idara ya Habari Maelezo.
 
Asante,hiyo ofisi ipo wapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…