Tarehe 2 Februari mwaka 1971 Idd Amini alijitangaza kuwa Rais wa Uganda

anonymousafrica

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2016
Posts
611
Reaction score
640

Siku kama ya leo mwaka 1971, jitu la Miraba minne Idd Amin alijitangaza kuwa Rais wa nchi ya Uganda na hii ni baada ya kugutuka kwamba Milton Obote alikuwa akipanga kumkamata kwa matumizi mabaya ya fedha za jeshi, Awali, Amin alichukua mamlaka kwa kufanya mapinduzi ya kijeshi tarehe 25 Januari 1971, wakati Obote akiwa anahudhuria mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Madola huko Singapore. Wanajeshi watiifu kwa Amin walifunga Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe na kuchukua Kampala.

Kila kitu kina chanzo aisee, hivi ni kwanini walifika hapa? em tuipitie uganda na historia ya wawili hawa kwa ufupi mno (Amini na Obote) Baada ya zaidi ya miaka 70 chini ya utawala wa Uingereza, Uganda ilipata uhuru wake Oktoba 9, 1962


Hapo Milton Obote akawa waziri mkuu wa kwanza wa taifa hilo. Kufikia 1964, Obote alikuwa ameunda muungano na Amin, unaambiwa walikuwa mabest mno na Amini ndiye alisaidia kupanua ukubwa na nguvu ya Jeshi la Uganda.(Mnyonge mnyongeni ukweli wake nausema hapa)

Mnamo Februari 1966, kufuatia shutuma kwamba wawili hao walihusika na kusafirisha dhahabu na pembe za ndovu kutoka nchini Kongo ambazo ziliuzwa kwa silaha,(Congo imepigwa mtungo kwa muda mrefu sana, Marehemu Profesa Baregu aliwahi kutuambia kadhaa (apumzike kwa amani)


Obote alisimamisha katiba na kujitangaza kuwa rais mtendaji na Muda mfupi baadaye, Obote alimtuma Amin kumwondoa mfalme Mutesa wa Pili, anayejulikana pia kama "Mfalme Freddie," ambaye alitawala ufalme wenye nguvu wa Buganda

Kwa uwezo wake na eneo kubwa alilolishikilia huyu tumuite ndiye Rais wa kwanza wa Uganda. Jaribio la kumuua lilifeli hapo awali, ila inahisiwa liliendelea kimya kimya hadi mwaka aliofariki kwa madai ya kunywa sumu (kujiua kupitia kilevi) japo wengine walikana haikuwa kujiua bali ni kuuliwa baada ya kulazimishwa kunywa pombe hiyo yenye sumu na mmoja kati ya wanajeshi watiifu wa Obote. Kuku lazima warudi zizini kulala alisema Malcom X akimaanisha ukifurahia ndugu zako kuua, basi kuna siku mauwaji hayo yatakurudia mwenyewe.


Obote alianza kutilia shaka uaminifu wa Amin na kuamuru akamatwe akiwa njiani kuelekea Singapore kwa Mkutano wa Wakuu wa Serikali wa Jumuiya ya Madola.

Wakati wa kutokuwepo kwake, Amin alichukua hatua hiyo na kufanya mapinduzi Januari 25, 1971, na ndipo tarehe 02 mwezi Februari bwana Idd Amin akajitangaza kama rais wa Uganda.
 
Huyu Amin naona kama alitolewa madarakani kwasababu ya kuwa na itikadi za kiuongozi zinazoshabihiana na Moja wa maraisi waliwahi kutawala Moja ya nchi za Africa Mashariki.

Kutowapigia magoti mabwanyenye
 
 
Mtasema yote lakini ukweli utabaki palepale kwamba Iddi Amin Dada alikuwa moja ya viongozi wakatili sana kuwahi kutokea duniani.

Atakumbukwa sana kwa namna alivyowauwa watu nchini Uganda miongoni mwao ni Dr. Benedict Kiwanuka aliyekuwa Jaji Mkuu, Brigedia Okoya, Brigedia Smutts Guwedeko, Askofu Janan Luwum wa kanisa la Anglikana na wengine wengi tu.
 
Huyu Amin naona kama alitolewa madarakani kwasababu ya kuwa na itikadi za kiuongozi zinazoshabihiana na Moja wa maraisi waliwahi kutawala Moja ya nchi za Africa Mashariki.

Kutowapigia magoti mabwanyenye
Afrika mashariki hapajawahi kuwa na rais aliyekataa kuwapgia magoti mabwanyenye
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…