Tarehe kumi mwezi wa kumi; Sikukuu ya Moi dei. Wakenya tujikumbushe kidogo

pingli-nywee

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
11,923
Reaction score
13,350
Leo ndio sikukuu ya Moi Dei, na ingawa Rais mstaafu Daniel Toroitich Arap Moi hakuacha tupumue kwa miaka ishirini na nne kuna mengi ya kukumbukwa, kwenye enzi hizo za utawala wake. Kwa mfano. Maziwa ya Nyayo. [emoji1][emoji1][emoji1]Ambayo wanafunzi wote nchini walipewa, bure bila malipo. Jogoo wa KANU. Bila kusahau rungu ya musee.
 
Nyimbo za kumsifia rais Moi, tawala Kenya, tawala.
 
Tunapaswa kusherehekea kazi yake ya ushindi. Hawa ndio watu wanaojulikana kwa kazi yao kwa ajili ya ubinadamu.
Nilishangaa jana kuona wakenya wakimkumbuka Moi na siku ya Moi dei wakati siku yenyewe ilifutwa kwenye kalenda na sio sikukuu rasmi tena. Ni kweli lakini, atakumbukwa pia kwa mazuri aliyoyafanya.
 
πŸ˜€Najua wewe hukuyanywa yale maziwa. Ulikuwa dunia nyingine.πŸ˜€
Hahaha! [emoji1] Acha wale walionyweshwa haya maziwa na Nyayo waje watuhadithie. Sisi enzi zetu tulikuwa tukingoja kwa hamu kubwa kengele ipigwe ili tukimbie nyumbani tukanyonye maziwa ya mama. [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…