Tarimba: Serikali iangalie njia bora ya kupanua wigo wa Walipakodi

Tarimba: Serikali iangalie njia bora ya kupanua wigo wa Walipakodi

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas ameishauri Serikali kuangalia utaratibu mzuri wa kupanua wigo wa Walipakodi badala ya kuongeza Kima cha Kodi

Akichangia Mjadala wa Bajeti Kuu amesema, "Tatizo lililopo hasa upande wa Serikali, wanamlenga Mlipakodi wanayemuona. Leo iwe 10% kesho iwe 12% kama njia ya kupandisha Mapato"

Amesema utaratibu huo ni mbaya, akishauri Mamlaka kuweka Kima kidogo ili watu wengi waweze kulipa kodi. Amesema kuweka Kima kikubwa kutapelekea Watanzania kutafuta njia ya kupenya na kutolipa Kodi
 
Watu wamejimegea maranchi makubwa na hawalipi kodi kwa kuwa wao ndo wamiliki.

Iko siku watu wataamua zaidi ya Hamza
 
Nimemsikiliza katoa ushauri mzuri kila siku tunasema unapoongeza kodi kwenye bidhaa mfano magari inafikia hatua purchasing power inashuka hivo hata kodi hutoipata lakini, kodi ikiwa himilivu kwanza inachochea mzunguko hata wa biashara na hata manunuzi yatakua mazuri kodi utakusanya sana maana ukuaji ni mkubwa
 
Kodi ni tools ya kuwafanya wengi wawe masikini Ili wao wazidi kulamba asali. Si kwamba awajui ukitoza kidogo utakusanya zaidi.

Lengo la kutoza kodi kubwa ni kukukomoa usifurukute rejea kodi za kuingiza gari nchini au mitambo au vitu vinavyokuja zalisha ajira na kuinua uchumi wachache ndo wenye kumudu.
 
Nimemsikiliza katoa ushauri mzuri kila siku tunasema unapoongeza kodi kwenye bidhaa mfano magari inafikia hatua purchasing power inashuka hivo hata kodi hutoipata lakini, kodi ikiwa himilivu kwanza inachochea mzunguko hata wa biashara na hata manunuzi yatakua mazuri kodi utakusanya sana maana ukuaji ni mkubwa
Kwao gari ni anasa na sio basic needs.
 
Nasubiria mchango wa babu tale
Kuhusu masuala ya kodi

Ova
 
Wigo ushatanuka hadi mwisho, utachanika
 
Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas ameishauri Serikali kuangalia utaratibu mzuri wa kupanua wigo wa Walipakodi badala ya kuongeza Kima cha Kodi

Akichangia Mjadala wa Bajeti Kuu amesema, "Tatizo lililopo hasa upande wa Serikali, wanamlenga Mlipakodi wanayemuona. Leo iwe 10% kesho iwe 12% kama njia ya kupandisha Mapato"

Amesema utaratibu huo ni mbaya, akishauri Mamlaka kuweka Kima kidogo ili watu wengi waweze kulipa kodi. Amesema kuweka Kima kikubwa kutapelekea Watanzania kutafuta njia ya kupenya na kutolipa Kodi
Suala la kuongeza walipa kodi limetawaliwa na unafiki kuliko uhalisia. Wote wanaopiga kelele kuwa walipa kodi ni wachache vichwani mwao wanaangalia wafanyakazi na wafanysbiashara ambao wanalipa income taxi lakini kiuhalisia wanaolupa kodi ni zaidi ya hao. Isipokuwa majina ndio tofauti lakini pesa yote inaingia hazina. Wakulima wanapouza mazao yao wanatozwa ushuru kwa kila gunia la kilo mia au kwa kutumia vipimo vingine, tofauti hapo ni kuwa wafanyabiashara wa mazao wanalipa tozo hiyo kwa niaba ya wakulima halmashauri kupitia mtendaji wa kijiji kisha wanamkata mkulima katika bei wanayomlipa kwa kila gunia. Fikiria halmashauri zote nchini zinakusanya takribani shilingi bilioni mia sita kutokana na ushuru wa mazao lakini watu hawaoni kama ni kodi wanahesabu wafanyakazi tu. Hebu tupanue mindset. Mfanyakazi anzlipa kila mwezi mfanyabiashara analipa kila robo mwaka na mkulima analipa kila anapovuna na zote hizo zinatiririka hazina japo kwa,majina tofauti. Pili kila mtu anapofanya manunuzi analipa kodi japo hajasajiliwa rasmi.

Ukwepaji kodi hufanywa na wafanyabiashara wakubwa wenye fungamno na wanasiasa hasa wanapoimport bidhaa .
 
Back
Top Bottom