Tarime wamkumbuka Chacha Zakayo Wangwe

Tarime wamkumbuka Chacha Zakayo Wangwe

TUNTEMEKE

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2009
Posts
4,587
Reaction score
580
Tarehe 28/07/2009 ilikuwa ni siku ya pekee Tarime kwani kulikuwa na maadhimisho ya mwaka mmoja tangu apate ajali na kufariki Mbunge na Mwanaharakati mpigania haki za wanyone Mh. Chacha Zakayo Wangwe "Chacha Rasta".

walichofanya katika siku hiyo ni kuwa na maandamano makubwa hadi katika shule ya Sekondari Nkende, ambayo ni moja ya shule zilizoasisiwa na kujengwa na Kamanda Wangwe akiwa diwani wa kata ya Tarime Mjini mwaka 2004, katika shule hiyo wananchi wa Tarime walipanda miti zaidi ya 30 kama sehemu ya kumbukumbu hiyo.

baada ya hapo waliandamana hadi katika hospitali ya wilaya ya Tarime na kufanya usafi katika mochwari ya kisasa ya wilaya hiyo, kufyeka na kupanda miti pia, kisha wakarudi kwa maandamano na miziki ya reagae na ngoma za asili hadi kwenye uwanja wa mpira wa Tarime kulipokuwa na tamasha la kumuenzi ambapo watu mbalimbali na vikundi vilijitokeza na kutoa burudani kamambe ikiwa na msg za kuthamini kazi aliyoifanya katika uhai wake ya kuwatetea wana Tarime hadi kufungwa huku wakionyesha hisia kuwa kutetea haki kwake ndiyo kumegharimu hata maisha yake.

Tamasha hilo liliandaliwa na Kampuni ya Kind Brothers ikishirikiana na NGO iitwayo Tukamilishane Women Home Association (TUWHA)
 
Tarime na CHADEMA watusaidie jambo moja; huyu waliempa nafasi ya Marehemu Chacha Wangwe haonekani kama ataimudu nafasi hii. Watutafutie mtu mwingine mwakani. Huyu nafasi ya UDIWANI inamtosha kabisa. Angalia jinsi anavyoishughulikia ile sumu inayomwagwa na ule mgodi wa North Mara.
 
Nafikiri Mwita anaweza kazi hiyo kwa sasa; maana nimeona upambanaji wake uko makini kidogo; sijui wanajamvini mnasemaje; kijana nimecomment sijui wenzangu mnasemaje?
 
Nafikiri Mwita anaweza kazi hiyo kwa sasa; maana nimeona upambanaji wake uko makini kidogo; sijui wanajamvini mnasemaje; kijana nimecomment sijui wenzangu mnasemaje?

Waliomchagua ni wananchi jamvini hawaingizi mtu mjengoni
 
Hata mimi naona huyu Mwera viatu ya Chacha Wangwe vimempwaya! Marehemu Chacha tunaendelea kukuombea kwa Mungu mwenyezi akurehemu na hatimaye urithi ufalme wa Mbinguni!
 
Guys did you want a copy cat? let him be with time he will mellow and develop his own style. Marehemu Wangwe had his own style and charisma.

MAY GOD BLESS HIS SOUL
 
Tarime hawawezi kuondokana na hisia za Wangwe.
  • Alifanana nao
  • Alifanya walichotaka, kama walivyotaka
  • Aliwaambia walichotaka kusikia namna walivyotaka kusikia
  • Aliwaongoza kufanya walilotaka kufanya namna walivyotaka kuongozwa kufanya.
R.I.P Chacha Zakayo Wangwe
 
Back
Top Bottom