Tasnifu za njano5: Marekani, ugaidi, uislamu na demokrasia, utata mtupu

Tasnifu za njano5: Marekani, ugaidi, uislamu na demokrasia, utata mtupu

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
Ugaidi ni nini hasa? Kuna uhusiano gani kati ya uislamu na ugaidi? Kuna uhusiano gani kati ya Marekani na ugaidi? Hivi Somali kuna shida gani? Hivi ilikuwaje Kenya ikajitia kwenye mgogoro na Somali? Mwenye kujua hayo na anijuze.

Nasikitika kuona dunia ikipambana na ugaidi badala ya kung'oa mizizi ya ugaidi. Huwezi kuzungumzia ugaidi kisha usizungumzie nchi za Afghanstan, Somali, Iraq, Pakistan, Palestina, Israeli, Saud Arabia, na Marekani.

Ukichunguza kwa makini ugaidi ni matokeo ya kuangushwa kwa tawala za nchi au majimbo zisizofuta siasa za kimagharibi(Demokrasia) au zilizokaidi kuwa vibaraka wa umagharibi. Tawala hizi ziliangushwa na badala yake zikasimikwa tawala zinazofuata mfumo wa demokrasia au zile zilizofyata mkia kwenye mikono ya wamagharibi.

Katika vita hakuna mshindi wala mshindwa, bali kuna kurudi nyuma na kujipanga. Kwenye mazungumzo ndio yupo mshindi; mshindi ni yule aliyefanikiwa kujenga hoja zenye mashiko hata mshindani wake akazielewa na kuacha hoja zake mufilisi. Katika mazungumzo mwenye kukubali kushindwa hubaki kwa furaha kwani anajua amekubali jambo lenye kumfaa.

Watu wamagharibi wanadhani kuwa mfumo wa kidemokrasia ndio mwarobaini wa shida zote za mwanadamu, na pia wanadhani kila sehemu yenye rasilimali wanaweza kuingia watakavyo hata ikibidi kwa mabavu. Mienendo ya nchi za kimagharibi ndio chanzo cha machafuko makubwa yote yaliyowahi na yanayoendelea kutokea ulimwengu.

Tukiwa kama dunia hatujasaahu biashara utumwa iliyoitajirisha Ulaya, lakini hadi sasa lawama kwa biashara ile kwa hapa Afrika Mashariki kaibeba mwarabu kama vile mashamba ya buni kule bara Amerika yalikuwa mali yake, ukoloni, vita ya kwanza ya dunia na ya pili. Hayo yote yaliinufaisha Ulaya na si mashariki au Afrika yenyewe. Katika ulimwengu wa ukoloni mamboleo zile nchi ambazo hazitaki kuwa vibaraka wa magharibi basi zitaundiwa kila aina ya zengwe ikiwemo na zengwe la kuzisema hizo nchi hazifuati utawala wa kidemokrasia au zina silaha za maangamizi.

Libya ya Ghadafi, ilikuwa ni nchi inayoongozwa vizuri pamoja na kwamba kulikuwa hakuna utawala wa kidemokrasia. Wananchi wa Libya walikuwa wanaishi vizuri na kuthaminiwa na serikali yao kuliko hata sisi watanzania tuliokuwa na serikali ya kidemokrasia. Tatizo la Ghadafi ni kukataa kwake kuwa kibaraka wa nchi za magharibi na yale maandamano na uasi umedhaminiwa na wamagharibi. Ukorofi wa Ghadafi ni kuona rasilimali za Libya zinawafaa zaidi walibya kuliko wazungu, Sasa hivi walibya wanajuta, wanatamani Ghadafi harudi hata sasa.

Hebu niambie, kwa wale wafuasi wa GHADAFI wakianza kulipiza kisasi dhidi ya serikali ya Tripoli ya sasa, Marekani na nchi za magharibi ni kosa? Ndio maana sikushangaa na wala sikusikitika pale ubalozi wa Marekani katika nchi ya Libya uliposhambuliwa. Iweje upande upepo kisha ughairi kuvuna tufani? Hichi ndicho kilichotokea Somali, Afghanstan na Iraq na sehemu zingine nyingi ambazo ziko na machafuko. Kung'olewa kwa tawala zile kimabavu huku Marekani ikishiriki aidha kwa chinichini au dhahiri ndio chanzo cha hii sinema ya ugaidi na vita dhidi ya ugaidi inayoendelea duniani.

Badala ya dunia kuamua kupambana na huo ugaidi kwa kudhamiria kuyapoteza makundi na magenge ya kigaidi kama Al-shababi na Al-qaida, ni vema dunia kwa nia ya dhati ikawakutanisha makundi yanayokinzana dhidi serikali, katika nchi za Afghanstan, Somalia na Iraqi, na wakati huo huo mgogoro kati ya Palestina na Israeli, na matatizo yaliyo katika nchi ya Chechinyia yapatiwe ufumbuzi. Matatizo na migogoro katika sehemu nilizozitaja hayawezi kuisha kwa nguvu za kijeshi ambazo Marekani inajivunia nayo.

Sehemu hizo zote ukizichunguza kwa makini utagundua kuwa tawala zake zilikuwa zinafuata sharia au zilikuwa hazikubali kuwa vibaraka wa magharibi. Wamarekani hawataki kusikia na wala hawapendi kuziona tawala zinazofuata sharia ya kiislamu na pia hawapendi tawala ambazo hazikubali kuendeshwa na wamagharibi. Kwa msingi huu, tatizo si ugaidi tatizo ni aina mpya ukoloni unaosambazwa na wamagharibi, kwani, kwa vyovyote vile ukoloni huu ndio chanzo cha ugaidi. Haya makundi yanayoitwa ya kigaidi huenda yanapambana na huo ukuloni mpya.

Serikali za Afrika ni za kinafiki sana na wapo kama mizombi kwa kukubali kuendeshwa. Kwa akili zao wanafikiri tatizo la Somalia linaweza kumalizwa kwa kutumia nguvu za kijeshi. Ukiangalia maumbile ya tatizo kati ya CONGO DRC na Somalia ni rahisi sana kulimaliza kijeshi tatizo DRC kuliko Somalia. Mabavu yaliyotumika dhidi ya Alshababi na wasomalia kwa ujumla kabla hata ya vikosi vya Afrika kuingia Somalia vinaumiza sana.

Video zinazoonesha yalitokea wiki hii Kenya zinatia machozi, lakini pia video zinazoonesha wasomalia wanavyofanyiwa vibaraka wa magharibi na wakati mwingine na majeshi ya kigeni pia zinaumiza na kuliza sana. Wasomali wakati mwingine hata kufanya ibada kwao ni tabu. Wakati nchi za Afrika zinapeleka vikosi Somali pia zingefikiria namna ya kuumaliza mgogoro wa Somalia kimazungumzo na si kutumia ubabe kama inavyofikiri Marekani.

Nimechukizwa na vitendo walivyovifanya Al-shabi Kenya, wangeipiga na kuvamia Ikulu ya Kenya nisingeumia hata kidogo, lakini kitendo cha kuua watu wasio na hatia binafsi kwa sasa nashindwa kuitafautisha hiyo Al-shababi na Marekani. Huenda hasira za Al-shababi kwa serikali ya Kenya zikawa ni za haki, lakini wale watu waliokufa na kujeruhiwa kwa tukio lile ndio watunga sera au ndio serikali ya Kenya? Huu ni uonezi dhidi ya utu wa mtu uliodhahiri na katu si wa kuungwa mkono. Marekani imeua maelfu ya watu wasio na hatia huko Iraq na Afghanstan nayo Al-shababi yafanya unyama uleule kama wa Marekani.

vita.jpg
Watu hawa hata ugomvi kati ya Al-shababi na Serikali yao hawajui na hauwahusu, lakini wameuliwa kinyama na kuumizwa kinyama, Mungu awalaani wote wanaofanya unyama huu,,pamoja na hayo, nani katudanganya kuwa vita ina macho?

Na ilaaniwe ile siku niliyozaliwa.

Njano5
0784845394.
 
Ugaidi ni nini hasa? Kuna uhusiano gani kati ya uislamu na ugaidi? Kuna uhusiano gani kati ya Marekani na ugaidi? Hivi Somali kuna shida gani? Hivi ilikuwaje Kenya ikajitia kwenye mgogoro na Somali? Mwenye kujua hayo na anijuze.

Nasikitika kuona dunia ikipambana na ugaidi badala ya kung'oa mizizi ya ugaidi. Huwezi kuzungumzia ugaidi kisha usizungumzie nchi za Afghanstan, Somali, Iraq, Pakistan, Palestina, Israeli, Saud Arabia, na Marekani.

Ukichunguza kwa makini ugaidi ni matokeo ya kuangushwa kwa tawala za nchi au majimbo zisizofuta siasa za kimagharibi(Demokrasia) au zilizokaidi kuwa vibaraka wa umagharibi. Tawala hizi ziliangushwa na badala yake zikasimikwa tawala zinazofuata mfumo wa demokrasia au zile zilizofyata mkia kwenye mikono ya wamagharibi.

Katika vita hakuna mshindi wala mshindwa, bali kuna kurudi nyuma na kujipanga. Kwenye mazungumzo ndio yupo mshindi; mshindi ni yule aliyefanikiwa kujenga hoja zenye mashiko hata mshindani wake akazielewa na kuacha hoja zake mufilisi. Katika mazungumzo mwenye kukubali kushindwa hubaki kwa furaha kwani anajua amekubali jambo lenye kumfaa.

Watu wamagharibi wanadhani kuwa mfumo wa kidemokrasia ndio mwarobaini wa shida zote za mwanadamu, na pia wanadhani kila sehemu yenye rasilimali wanaweza kuingia watakavyo hata ikibidi kwa mabavu. Mienendo ya nchi za kimagharibi ndio chanzo cha machafuko makubwa yote yaliyowahi na yanayoendelea kutokea ulimwengu.

Tukiwa kama dunia hatujasaahu biashara utumwa iliyoitajirisha Ulaya, lakini hadi sasa lawama kwa biashara ile kwa hapa Afrika Mashariki kaibeba mwarabu kama vile mashamba ya buni kule bara Amerika yalikuwa mali yake, ukoloni, vita ya kwanza ya dunia na ya pili. Hayo yote yaliinufaisha Ulaya na si mashariki au Afrika yenyewe. Katika ulimwengu wa ukoloni mamboleo zile nchi ambazo hazitaki kuwa vibaraka wa magharibi basi zitaundiwa kila aina ya zengwe ikiwemo na zengwe la kuzisema hizo nchi hazifuati utawala wa kidemokrasia au zina silaha za maangamizi.

Libya ya Ghadafi, ilikuwa ni nchi inayoongozwa vizuri pamoja na kwamba kulikuwa hakuna utawala wa kidemokrasia. Wananchi wa Libya walikuwa wanaishi vizuri na kuthaminiwa na serikali yao kuliko hata sisi watanzania tuliokuwa na serikali ya kidemokrasia. Tatizo la Ghadafi ni kukataa kwake kuwa kibaraka wa nchi za magharibi na yale maandamano na uasi umedhaminiwa na wamagharibi. Ukorofi wa Ghadafi ni kuona rasilimali za Libya zinawafaa zaidi walibya kuliko wazungu, Sasa hivi walibya wanajuta, wanatamani Ghadafi harudi hata sasa.

Hebu niambie, kwa wale wafuasi wa GHADAFI wakianza kulipiza kisasi dhidi ya serikali ya Tripoli ya sasa, Marekani na nchi za magharibi ni kosa? Ndio maana sikushangaa na wala sikusikitika pale ubalozi wa Marekani katika nchi ya Libya uliposhambuliwa. Iweje upande upepo kisha ughairi kuvuna tufani? Hichi ndicho kilichotokea Somali, Afghanstan na Iraq na sehemu zingine nyingi ambazo ziko na machafuko. Kung'olewa kwa tawala zile kimabavu huku Marekani ikishiriki aidha kwa chinichini au dhahiri ndio chanzo cha hii sinema ya ugaidi na vita dhidi ya ugaidi inayoendelea duniani.

Badala ya dunia kuamua kupambana na huo ugaidi kwa kudhamiria kuyapoteza makundi na magenge ya kigaidi kama Al-shababi na Al-qaida, ni vema dunia kwa nia ya dhati ikawakutanisha makundi yanayokinzana dhidi serikali, katika nchi za Afghanstan, Somalia na Iraqi, na wakati huo huo mgogoro kati ya Palestina na Israeli, na matatizo yaliyo katika nchi ya Chechinyia yapatiwe ufumbuzi. Matatizo na migogoro katika sehemu nilizozitaja hayawezi kuisha kwa nguvu za kijeshi ambazo Marekani inajivunia nayo.

Sehemu hizo zote ukizichunguza kwa makini utagundua kuwa tawala zake zilikuwa zinafuata sharia au zilikuwa hazikubali kuwa vibaraka wa magharibi. Wamarekani hawataki kusikia na wala hawapendi kuziona tawala zinazofuata sharia ya kiislamu na pia hawapendi tawala ambazo hazikubali kuendeshwa na wamagharibi. Kwa msingi huu, tatizo si ugaidi tatizo ni aina mpya ukoloni unaosambazwa na wamagharibi, kwani, kwa vyovyote vile ukoloni huu ndio chanzo cha ugaidi. Haya makundi yanayoitwa ya kigaidi huenda yanapambana na huo ukuloni mpya.

Serikali za Afrika ni za kinafiki sana na wapo kama mizombi kwa kukubali kuendeshwa. Kwa akili zao wanafikiri tatizo la Somalia linaweza kumalizwa kwa kutumia nguvu za kijeshi. Ukiangalia maumbile ya tatizo kati ya CONGO DRC na Somalia ni rahisi sana kulimaliza kijeshi tatizo DRC kuliko Somalia. Mabavu yaliyotumika dhidi ya Alshababi na wasomalia kwa ujumla kabla hata ya vikosi vya Afrika kuingia Somalia vinaumiza sana.

Video zinazoonesha yalitokea wiki hii Kenya zinatia machozi, lakini pia video zinazoonesha wasomalia wanavyofanyiwa vibaraka wa magharibi na wakati mwingine na majeshi ya kigeni pia zinaumiza na kuliza sana. Wasomali wakati mwingine hata kufanya ibada kwao ni tabu. Wakati nchi za Afrika zinapeleka vikosi Somali pia zingefikiria namna ya kuumaliza mgogoro wa Somalia kimazungumzo na si kutumia ubabe kama inavyofikiri Marekani.

Nimechukizwa na vitendo walivyovifanya Al-shabi Kenya, wangeipiga na kuvamia Ikulu ya Kenya nisingeumia hata kidogo, lakini kitendo cha kuua watu wasio na hatia binafsi kwa sasa nashindwa kuitafautisha hiyo Al-shababi na Marekani. Huenda hasira za Al-shababi kwa serikali ya Kenya zikawa ni za haki, lakini wale watu waliokufa na kujeruhiwa kwa tukio lile ndio watunga sera au ndio serikali ya Kenya? Huu ni uonezi dhidi ya utu wa mtu uliodhahiri na katu si wa kuungwa mkono. Marekani imeua maelfu ya watu wasio na hatia huko Iraq na Afghanstan nayo Al-shababi yafanya unyama uleule kama wa Marekani.

View attachment 113618
Watu hawa hata ugomvi kati ya Al-shababi na Serikali yao hawajui na hauwahusu, lakini wameuliwa kinyama na kuumizwa kinyama, Mungu awalaani wote wanaofanya unyama huu,,pamoja na hayo, nani katudanganya kuwa vita ina macho?

Na ilaaniwe ile siku niliyozaliwa.

Njano5
0784845394.

Nanukuu maneno yako haya.."Na ilaaniwe ile siku niliyozaliwa"
Mkuu hapo unataka kutwambia kwamba Mama yako angekutumbukiza chooni, angetoa mimba usizaliwe, asingekutana na baba yako wakatunga mimba yako..... Kauli kama hizi Mungu hapendi kabisa!!
 

Nanukuu maneno yako haya.."Na ilaaniwe ile siku niliyozaliwa"
Mkuu hapo unataka kutwambia kwamba Mama yako angekutumbukiza chooni, angetoa mimba usizaliwe, asingekutana na baba yako wakatunga mimba yako..... Kauli kama hizi Mungu hapendi kabisa!!

NILIANDIKA MAKALA HII SIKU YA KUZALIWA KWANGU KATIKA UKURASA WANGU WA FB, NAOMBA ISOME HUENDA UTAPATA MAZINGATIO.

NAOMBA SIKU ILIYOTUNGWA MIMBA YANGU ILAANIWE, NAAM, ISIWE NA BARAKA ABADANI.

"Na ilaaniwe siku niliyozaliwa, isibarikiwe siku ile aliyonizaa mama yangu. Na alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, akisema, Umezaliwa mtoto mwanamume; akimfurahisha. Mtu huyo na awe kama miji ile, ambayo Bwana aliiangamiza, asijute; na asikie kilio asubuhi, na kelele za fujo adhuhuri; kwa sababu hakuniua nilipotoka tumboni, na hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, na mimba yake sikuzote nzito. Nalitoka tumboni kwa sababu gani, kuona taabu na huzuni, hata siku zangu ziharibike katika aibu?" Yeremia 20:14-18

Kwa vyovyote vile siku kama ile, yaani ya tarehe 02 mwezi wa 08 ya mwaka 1986 ndio chanzo cha mateso yangu na huzuni yangu niliyonayo katika moyo wangu. Kila siku kwangu afadhali ya jana, yaani, nakwenda hatua tano mbele pasina hata habari hujikuta narudi hatua saba nyuma. Nakopa hapa nikalipe pale, na hata wale ambao walikuwa wananikimbilia kwa shida zangu za kaskazi na kusi naona sasa wamenawa mikono kama Pilato kwa kesi ya Masiha, niko mwenyewe jangwani, mama yangu uko wapi? Nimekuwa mwanao, na sasa ndio nayaona mwanao, eeeh, yale uliyoyasema kuwa yaniladhimu nikue ndio nipate kibali cha kuyaona, mama nilidhani nitakuja kuona uzuri wa dunia kumbe ubaya wa dunia?

Pamoja na hayo, dunia imekuwa si sehemu salama tena kwangu, dunia imezungukwa na UKIMWI, saratani, njaa, majanga ya asili, ajali za vyombo vya usafiri, vita, chuki, fitina, mauaji ya halaiki, unyonyaji, rushwa, migomo ya watumishi wa umma, maradhi ya milipuko, tawala kandamizi, ubakaji, uchawi, husuda, ufisadi, unajisi kwa vichanga, ukahaba, na kifo. Hata kama uko na maisha mazuri na ya hadhi ya juu huwezi kukosa huzuni moyoni, maradhi na hatimaye kifo, huu kama si upuuzi wa kujilisha upepo n' nini hasa?Ama kwa hakika Mfalme Suleiman [a.s] alikuwa sahihi, rejea kitabu cha mhubiri sura ya pili na ya tatu.

Mambo hayo si kwamba yanaifanya dunia kuwa si sehemu salama kwa kuishi mwanadamu, lakini pia yanaifanya dunia kuwa sehemu ya kuogofya kuishi na sehemu ya kuogofya kuiacha, naam, kuiacha kwa njia ya kifo, na mbaya zaidi hakuna njia mbadala ya kuweza kututoa duniani zaidi ya kifo kinachotukumba sanjari na utungu wa kutoka roho. Ninakumbana na shida hizi ni kwasababu tu nimezaliwa, kama ndivyo kuna sababu yoyote ya msingi kwangu mimi kuitukuza siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwangu? Sina, ni jambo la busara kwangu mimi kuiombea laana siku ile niliyozaliwa kama alivyofanya nabii Isaya miaka mingi iliyopita.

"Heri sifa njema kuliko marhamu nzuri; Na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa. Heri kuiendea nyumba ya matanga, Kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake." Mhubiri 7:1-2

Maneno hayo katika kitabu hicho cha mhubiri aliyatamka nabii na mfalme Suleiman[a.s] miaka mingi iliyopita, lakini yangali yana ijara njema kwetu. Pamoja na kwamba kifo kinaogopesha, lakini ni heri kufa kuliko kuzaliwa. Naam kwa "kuzaliwa" mwanadamu hukutana na tabu na mateso ya dunia, lakini kwa "kufa" binadamu huyaacha mateso na tabu za dunia. Njaa, UKIMWI, vita, huzuni, kifo, kiu,na kila aina ya mateso mwanadamu huyaacha pindi akifa.

Baba, mama na baadhi ya wapendwa wangu wamekufa, yaani, wameipa kisogo dunia yenye mateso, wameniacha mimi mwenyewe duniani ili hali nasukwa na hayo mateso ya dunia. Natamani kufa, natamani kifo cha asili, kifo kinachotawaliwa na qadar, wallahi dunia imenikinai na kunichosha vya kutosha, nimemkosa mama na baba yangu vya kutosha, kiukweli nawahitaji. Wao hawawezi kuja kwangu lakini mimi naweza kwenda kwao kwa njia ya kifo tu, kama ndivyo huu si uhalali wa mimi kutamani kifo? Dunia ni ino ino, na waja ni wale wale, hayana budi kuwa ili unabii upate kutimia kwa mapenzi yake aliye juu.

"Lakini sasa amekufa nifungie nini? Je! Naweza kumrudisha tena? Mimi nitakwenda kwake lakini yeye hatanirudia mimi." 2 Samweli 12:23

Miaka mingi iliyopita maneno hayo hayo aliyatamka mfalme na nabii Daud [a.s] mara baada ya kufiwa na mtoto wake aliyezaa na Bath-Sheba aliyekuwa mwanamke wa Uria. Pia nami nimeyatamka katika namna ya kupata faraja ya ndani ya moyo wangu. Najua ipo siku nitaungana na wapendwa wangu, mama na baba yangu na wengineo.

Hakika niko na imani kuwa tutaungana na wapendwa wetu, naomba rejea qur-an katika surat Mariam aya 12 hadi 15. Naomba mrejee aya hizo na mpate mazingatio kwazo. Kwani pamoja na mambo mengine, aya hizo zinatambua siku za kuzaliwa, kufa na kufufuliwa. Niko na imani nitakufa na nitafufuliwa pamoja na wapendwa wangu tukiwa na manabii, masharifu, mawalii na watu wema ishallah!!!

."Ewe Yahya! Kishike Kitabu kwa nguvu! Nasi tulimpa hikima angali mtoto. Na tukampa huruma itokayo kwetu, na utakaso, na akawa mchamungu. Na akawa mwema kwa wazazi wake, wala hakuwa jabari mua'si. Na amani iwe juu yake siku ya kuzaliwa, na siku ya kufa, na siku ya kufufuliwa" qur-an 19:12-15

Kila mwaka tarehe 2 ya mwezi 8 umri wangu huongezeka, nawashukuru watu wote walionitakia heri ya kuzaliwa, samahani sijawajibu kwasababu sikuwa hewani. Pamoja na hilo, naomba niseme kitu biidhini llah taala, ya kwamba, nguvu, utajiri, busara, hekima, elimu, ujuzi, maarifa, upeo, na hata umri huongezeka sanjari na majukumu, kinyume chake ni upuuzi si kama ujuha wa kuhesabu matone ya mvua.

Binaadamu mwenye kutambua hayo yote ya juu na akaishi kwa kuyakabili majukumu yake badala ya kuyakimbia, hana tafauti na nyumba iliyojengwa juu ya mwamba moto, nyumba ambayo hata kama ikisukwa na kupigwa na tufani za rangi mbalimbali itaendelea kusimama pasina kutetereka hata kidogo.

Binaadamu mwenye kutambua hilo, siku zote huongozwa na fikra pevu na himilivu, fikra ambazo huumpa mamlaka na uwezo wa kutimiza ndoto zake njema alizoota jana, haijalishi hizo ndoto kaota usiku wa manane wenye kiza kinene, alfajiri wenye kiza cha utusitusi, adhuhuri ya jua la utosi, alaasiri ya jua la komwe, magharibi ya mawio au muda wowote.

Binaadamu mwenye kutambua hilo, haitaji msaada kutoka kwa watu wenye damu na mwili katika kutimiza ndoto zake kama nilivyozitaja hapo juu, bali anahitaji mtu mwenye pumzi ya ziada, pumzi ambayo ina nguvu ya kutawala na kuziamrisha pumzi ngeni hata zikatii matakwa ya mja muhusika.

Binaadamu mwenye kutambua hilo, lazima matakwa ya moyo wake ndio yawe yenye kuheshimiwa na ulimwengu unaotawaliwa na sheria za kiuchumi [unlimited of human wants & limited ways of satisfying dem] na sheria za kimaumbile[laws dat governs universe]

Binaadamu mwenye kutambua hilo, ni lazima atazaliwa mara ya pili, uzaliwa ambao ni tafauti kabisa na ule wa asili, uzaliwa wa kutoka kwa baba na mama. Kuzaliwa huku mara ya pili kunaonekana kupitia matokeo chanya yenye faida ya kufuzu kuzikabili changamoto[majukumu]. Kuijua na kisha kuiendea au kuipiga vita qadari yako hata uishinde ni kiashiria kikuu cha kuzaliwa mara ya pili.

Binaadamu mwenye kutambua hilo, hato onja mauti kamwe katika ulimwengu wa leo, ataishi duniani kwa miaka dahari hata kama mwili wake utakuwa ni mavumbi. Mfano ni Adam Smith, aliyekuwa bingwa wa uchumi katika zama zake, Newton bingwa wa fizikia, kemia na hesabu katika zama zake. Hawa watu wangali wanaishi hata sasa.

Binaadamu mwenye kutambua hilo, ataishi milele katika raha na mustarehe katika ulimwengu wa kesho, atafurahi na mahurain wake atakavyo, huku akisaahu maumivu aliyokuwa akiyapata wakati akiishi katika ulimwengu unaotawaliwa na majukumu na changamoto.

Binaadamu huyo, yaani mwenye kutambua hilo, ninaamuru niwe mmoja wao kama aishivyo NIKO AMBAYE NIKO, na lazima mimi nitakuwa miongoni mwao, si kama nitakavyo mimi, bali kama atakavyo MUNGU WA MAJESHI MFALME WA SIKU YA MWISHO NA MMILIKI WA SIKU YA HUKUMU yaani YEHOVA.

Naomba nijitakie kheri na fanaka katika siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwangu. Allah[s.w] atimize mapenzi yake mema kwangu, nipate siku nyingi za kuishi na katika siku hizo niketi na kufukiri hata nizidi kujua kuwa MUNGU YU MWEMA NA FADHILA ZAKE NI ZA MILELE.

Naomba nichukue nafasi hii pia kwa kuwashukuru wale wote walioungana na mimi katika siku hii adhimu kwangu, mungu awabariki na awalipe badala inshalla!

Togwa, fulu, mkembe au bada la tui bubu, na embe ng'ongo zi wapi?

Nawapenda sana rafiki zangu nawatakia idd njema.

Njano5.

0784845394

 
Back
Top Bottom