Tathmini ya wapinzani watatu watarajiwa wa Simba hatua ya robo fainali CAF Shirikisho

Tathmini ya wapinzani watatu watarajiwa wa Simba hatua ya robo fainali CAF Shirikisho

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Katika hatua ya robo fainali ya mashindano ya CAF Shirikisho, Simba enaenda kukutana na timu mojawapo kati ya hizi tatu, Stellenbosch ya Afrika Kusini, ASEC Mimosas ya Ivory Coast na Al Masry ya Misri.

Hii ni tathmini yangu fupi ya timu hizi tatu na aina ya upinzani ambao Simba iutegemee.

AL MASRY
Simba ilifahamu fika kuwa itaenda kukutana sana na timu za waarabu msimu huu na ni kitu ambacho inabidi ujifunze kukikabili katika mashindano yote ya CAF maana kawaida ndiyo timu ngumu.

Simba kwa kujua hilo iliweka kambi yake ya pre-season nchini Misri. Hii ilisaidia kuwaandaa wachezaji mapema sana kujua kikwazo kikubwa cha msimu ni kipi katika kufikia malengo ya klabu.

Kama ilivyotarajiwa, hatua ya awali kabisa Simba ikakutana na kigingi kizito cha Al Ahly Tripoli ya Libya, ikavuka tena kwa kishindo. Hatua ya makundi ikakutana na waarabu wawili Sfaxien ya Tunisia na CS Constantine ya Algeria, simba ikashinda mechi 3 kati ya 4 na timu hizo ikiwemo kuweka rekodi ya kumfunga mwarabu nje ndani. Maandalizi ya pre-season kujiandaa na waarabu yakaonesha kulipa mpaka sasa.

Sasa kuna uwezekano wa kukutana na huyu mwarabu mwingine hatua ya robo fainali. Kutoka sasa kama Simba itafika hadi fainali kuna uwezekano mkubwa wa kukutana na waarabu wengine wawili au watatu. Nadhani hili lilifikiriwa mapema sana na Simba imejiandaa kwa hilo.

STELLENBOSCH
Hii ni timu ambayo imeanza kutingisha siku za hivi karibuni. Mwanzoni kwa msimu huu Mo Dewji aliitembelea hii klabu na kuisifia. Ni wazi Mo na Simba walishanusa potential ya hii timu kabla hata wengi hawajaijua au kuitilia maanani.

Ni timu ya kuizingatia sana maana imeonyesha imedhamiria kuja kuleta ushindani ndani ya ligi ya Afrika Kusini na Afrika kwa ujumla.

ASEC MIMOSAS
Kwa msimu huu ASEC ina timu ya kawaida sana ila kitendo cha kufika robo fainali kinaonyesha siyo timu ya kubeza. ASEC haikaukiwi vijana wenye njaa ya mafanikio na usije kushangaa mwishoni mwa msimu huu wakatoa mastaa wengine wapya kabisa.

Wasiwasi wangu mkubwa kwa ASEC kulinganisha na hizo timu zingine zinazoweka kukutana na Simba ni kuwa Yanga inaweza kuweka mkono wake kuzipa ugumu mechi za Simba iwapo itakutana nayo. Yanga ikumbuke kuwa ASEC ni moja ya timu 4 zinazoweza kuishusha Yanga kwenye rank za CAF kwa jinsi zinavyoendelea kufanya vizuri kwa hiyo wakiisaidia watakuwa wanajishusha wenyewe!

Kingine kinachonipa moyo ni kuwa ASEC inaendeshwa kiprofesheno na ina mahusiano mazuri ya kibiashara na Simba. Sitegemei kama wataingia kwenye hizo siasa za Simba na Yanga. Nadhani wakikutana na Simba watakuja kucheza mpira wa fair tu usio na drama zozote.

Kwa kumalizia, huu ni utabiri wangu wa matokeo. Nategemea yoyote atakayekutana naye, Simba itavuka kwenda nusu fainali.

UTABIRI:
Al Masry - Simba itashinda mechi zote mbili, nyumbani na ugenini
ASEC - Draw ugenini, Simba inashinda nyumbani.
Stellenbosch - Draw ugenini, Simba itashinda mechi ya nyumbani.
 
sema kabisa,isipotokea hivyo tukufanye nini?
Hapana hatakiwi kusema kama unavyotaka,alichofanya ni kitu kizuri sana,yaani tafakari.
Katika maisha tunatakiwa tuishi hivyo,sisi ni binadamu tofauti na wanyama,kutafakari changamoto zinazoweza kutokea kesho,mfano kujua kesho nitakula Nini,nitafanya Nini,nitavaa nini.,nikiumwa nitatibiwa vipi,(gharama)sipotokea hivyo ulivyotafakari sio mbaya lakini usipotafakari halafu changamoto zikatokea utapata shida kubwa.
 
Katika hatua ya robo fainali ya mashindano ya CAF Shirikisho, Simba enaenda kukutana na timu mojawapo kati ya hizi tatu, Stellenbosch ya Afrika Kusini, ASEC Mimosas ya Ivory Coast na Al Masry ya Misri.

Hii ni tathmini yangu fupi ya timu hizi tatu na aina ya upinzani ambao Simba iutegemee.

AL MASRY
Simba ilifahamu fika kuwa itaenda kukutana sana na timu za waarabu msimu huu na ni kitu ambacho inabidi ujifunze kukikabili katika mashindano yote ya CAF maana kawaida ndiyo timu ngumu.

Simba kwa kujua hilo iliweka kambi yake ya pre-season nchini Misri. Hii ilisaidia kuwaandaa wachezaji mapema sana kujua kikwazo kikubwa cha msimu ni kipi katika kufikia malengo ya klabu.

Kama ilivyotarajiwa, hatua ya awali kabisa Simba ikakutana na kigingi kizito cha Al Ahly Tripoli ya Libya, ikavuka tena kwa kishindo. Hatua ya makundi ikakutana na waarabu wawili Sfaxien ya Tunisia na CS Constantine ya Algeria, simba ikashinda mechi 3 kati ya 4 na timu hizo ikiwemo kuweka rekodi ya kumfunga mwarabu nje ndani. Maandalizi ya pre-season kujiandaa na waarabu yakaonesha kulipa mpaka sasa.

Sasa kuna uwezekano wa kukutana na huyu mwarabu mwingine hatua ya robo fainali. Kutoka sasa kama Simba itafika hadi fainali kuna uwezekano mkubwa wa kukutana na waarabu wengine wawili au watatu. Nadhani hili lilifikiriwa mapema sana na Simba imejiandaa kwa hilo.

STELLENBOSCH
Hii ni timu ambayo imeanza kutingisha siku za hivi karibuni. Mwanzoni kwa msimu huu Mo Dewji aliitembelea hii klabu na kuisifia. Ni wazi Mo na Simba walishanusa potential ya hii timu kabla hata wengi hawajaijua au kuitilia maanani.

Ni timu ya kuizingatia sana maana imeonyesha imedhamiria kuja kuleta ushindani ndani ya ligi ya Afrika Kusini na Afrika kwa ujumla.

ASEC MIMOSAS
Kwa msimu huu ASEC ina timu ya kawaida sana ila kitendo cha kufika robo fainali kinaonyesha siyo timu ya kubeza. ASEC haikaukiwi vijana wenye njaa ya mafanikio na usije kushangaa mwishoni mwa msimu huu wakatoa mastaa wengine wapya kabisa.

Wasiwasi wangu mkubwa kwa ASEC kulinganisha na hizo timu zingine zinazoweka kukutana na Simba ni kuwa Yanga inaweza kuweka mkono wake kuzipa ugumu mechi za Simba iwapo itakutana nayo.

Kinachonipa moyo ni kuwa ASEC inaendeshwa kiprofesheno na ina mahusiano mazuri ya kibiashara na Simba. Sitegemei kama wataingia kwenye hizo siasa za Simba na Yanga. Nadhani wakikutana na Simba watakuja kucheza mpira wa fair tu usio na drama zozote.

Kwa kumalizia, huu ni utabiri wangu wa matokeo. Nategemea yoyote atakayekutana naye, Simba itavuka kwenda nusu fainali.

Al Masry - Simba itashinda mechi zote mbili, nyumbani na ugenini
ASEC - Draw ugenini, Simba inashinda nyumbani.
Stellenbosch - Draw ugenini, Simba itashinda mechi ya nyumbani.
Utashangaa uyo Al marsy ndoo anasumbua
 
Utashangaa uyo Al marsy ndoo anasumbua
Ni utabiri tu wa haraka haraka. Hata hao wengine Simba anaweza kuwapiga nje ndani.

Simba ikiwa on form na kucheza kwa tahadhari, timu zote hizo tatu zinaweza kupigwa nje ndani lakini nimeona niwe fair na kuupa mpira heshima ndiyo maana nimeweka hizo droo za ugenini.
 
Asec ni Kama Ajax au Borussia ya ujerumanu , hata uuze timu nzima bado inaibua vipaji vingine.
Niliangalia Asec iliyochukua ubingwa wa Afrika, iliuza wachezaji karibia wote Ila super cup wakacheza waliopandishwa daraja kina Toure hivyo ni timu ya kuogopwa zaidi.
Timu ya Africa Kusini imekosa uzoefu zaidi hiyo ni advantage kwa Simba.
 
Asec ni Kama Ajax au Borussia ya ujerumanu , hata uuze timu nzima bado inaibua vipaji vingine.
Niliangalia Asec iliyochukua ubingwa wa Afrika, iliuza wachezaji karibia wote Ila super cup wakacheza waliopandishwa daraja kina Toure hivyo ni timu ya kuogopwa zaidi.
Timu ya Africa Kusini imekosa uzoefu zaidi hiyo ni advantage kwa Simba.
Sahihi kabisa Stellenbosch uzoefu unaweza kuwacost. ASEC siwachukulii poa, unaweza kushangaa wanafika hata fainali.

Napenda timu zinazoamini vijana, zinakupa fursa ukipata nafasi nenda ili na wengine wapate fursa.
 
Sahihi kabisa Stellenbosch uzoefu unaweza kuwacost. ASEC siwachukulii poa, unaweza kushangaa wanafika hata fainali.

Napenda timu zinazoamini vijana, zinakupa fursa ukipata nafasi nenda ili na wengine wapate fursa.
Mnaangalia historia au current perfomance? Kama mnaangalia current form al masry ndio timu ngumu kuliko asec na stellenbosch.

Al masry wapo kwenye kiwango bora sana wa 5 kwenye ligi na wamefungwa mechi 1 tu. Kwenye shirikisho pia wamefunga mechi 1 tu na zamalek.

Al masry ni ngumu kututoa ila anaweza kutupa tough gemu.

Stellenbosch ndo timu rahisi kuliko zote hawa tukipewa tukiamua kwa mkapa wanaweza kufa hata 5.

Asec labda uzoefu tu lakini in terms of current form wa kawaida tu kama bravos tu au tripoli hv.
 
Hii draw ya leo inamaanisha Simba ina uwezo wa kuwa top 3 katika ranking za CAF maana ina uwezo wa kumzuia Zamalek asifike fainali.

Fainali ya Simba vs Zamalek ingenoga zaidi ila tukiwalipizia kisasi vyura dhidi ya USMA itapendeza pia.

Muhimu sana kwa wachezaji kufocus kwa mpinzani wa robo fainali Al Masry wasifikirie hao wapinzani wa mbele.
 
Back
Top Bottom