Tatizo hili la ulevi hasa wa pombe,Unga na Bangi linaanzaje

Tatizo hili la ulevi hasa wa pombe,Unga na Bangi linaanzaje

Maalim Jumar

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2010
Posts
1,259
Reaction score
118
Wana JF!
Heri ya mwaka wa Twenty Eleven.

Hili jambo la ulevi haswa wa pombe na madawa ya kulevya n.k

Nimeona kuanzia dini mbali mbali hata serikali wanalipiga vita kwa nguvu zote.

Ajabu japo baadhi ya Nchi chache duniani wanaona ni jambo la kawaida tu.

Sasa pamoja na kuona madhara yake...kwa walevi wa pombe..hutokea ikawa sababu ya kuharibika ndoa yake au kusambaratika familia yake..kwa madeni mbali mbali...hata kufukuzea kazi n.k.

-Wavuta bangi kufanya mambo ya ajabu mitaani hata maofisini n.k

-Hivi hadi muhusika akaingia katika hivi vishawishi hua analazimishwa na jamaa zake? Au kuna nguvu ziada humzidi?

- Kuna kijana mmoja kwao wanao uwezo wa mali...ambazo angeweza kusima hadi Phd kwa pesa za kwao...ajabu ni kua ameingia kwenye utumiaji wa Unga...hata form four matokeo si mazuri..akapelekwa akasome japo (IT) na huko imeshindikana...sasa ni nini mambo haya?

HITIMISHO:
Tunawasaidiaje waathirika na wale
E wapo njiani kuingia humu katika utumiaji wa viharibu akili na mambo mengine?
Au kuna faida ambazo wanazipata kwenye hayo matumizi yz madawa ?

Nawasilisha nisaidiwe kujua.
 
Mkuu,

Vijana wengi huanza hayo uliyoyataja kutokana na kupenda kuiga. Kwa mfano wanapotizama filamu za action, za kimafia na kuona matumizi ya vileo na wale watumiaji wanavyoonekana wajanja.

Pia vigenge,vikundi vya marafiki wanaokuzunguka au unaowahusudu kuwa ni mfano mzuri kwako(peer group influence)

Pia kwa wakubwa huingia huko kutokana na frustration za maisha ili kupoteza mawazo(kutaka kusahau kwa muda shida walizonazo)
Wengine ndio huwa wana hela na husema wanataka kustarehe, nao huelekea huko vilabuni kukamata chupa na gilasi.
Tatizo ni kuwa watu wanapoanza huanza kama utani hivi, wakisahau kuwa vileo huendana na (addiction) Vileo vina kawaida ya kuwa ving'anganizi.Unapovichokoza vinakuganda na inakupa kufanya kazi ya ziada kuvibandua kutoka katika fikra(hamu) na kutoka katika damu yako.
Vileo vinakujengea utegemezi, kwamba lazima uvipate ndio akili itulie....in the long run vinakuathiri hiyo akili na kukupopotoa, una-loose control ya utashi wako, na vileo huwa vinakuamrisha ukavitafute kokote kule.

Nani wa kumlaumu? hili ni suali gumu kulijibu
lakini lawama zianzie kwa mtumiaji mwenyewe, pili wale wanaofanikisha kupatika kwa vileo hivyo.....huenda nitarudi tena kuchangia jinsi ya kugawa lawama ... lakini la msingi ni kuwa kinga ni bora kuliko kutibu! na lawama hazisaidii sana tatizo likishakuwepo.
 
Mkuu,

Vijana wengi huanza hayo uliyoyataja kutokana na kupenda kuiga. Kwa mfano wanapotizama filamu za action, za kimafia na kuona matumizi ya vileo na wale watumiaji wanavyoonekana wajanja.

Pia vigenge,vikundi vya marafiki wanaokuzunguka au unaowahusudu kuwa ni mfano mzuri kwako(peer group influence)

Pia kwa wakubwa huingia huko kutokana na frustration za maisha ili kupoteza mawazo(kutaka kusahau kwa muda shida walizonazo)
Wengine ndio huwa wana hela na husema wanataka kustarehe, nao huelekea huko vilabuni kukamata chupa na gilasi.
Tatizo ni kuwa watu wanapoanza huanza kama utani hivi, wakisahau kuwa vileo huendana na (addiction) Vileo vina kawaida ya kuwa ving'anganizi.Unapovichokoza vinakuganda na inakupa kufanya kazi ya ziada kuvibandua kutoka katika fikra(hamu) na kutoka katika damu yako.
Vileo vinakujengea utegemezi, kwamba lazima uvipate ndio akili itulie....in the long run vinakuathiri hiyo akili na kukupopotoa, una-loose control ya utashi wako, na vileo huwa vinakuamrisha ukavitafute kokote kule.

Nani wa kumlaumu? hili ni suali gumu kulijibu
lakini lawama zianzie kwa mtumiaji mwenyewe, pili wale wanaofanikisha kupatika kwa vileo hivyo.....huenda nitarudi tena kuchangia jinsi ya kugawa lawama ... lakini la msingi ni kuwa kinga ni bora kuliko kutibu! na lawama hazisaidii sana tatizo likishakuwepo.

Hakuna njia zozote za kuwasaidia waliokwisha zamia katika ulevi?
 
Hakuna njia zozote za kuwasaidia waliokwisha zamia katika ulevi?

Mkuu,
Zipo.
Mara nyingi njia inayotumika ni kwa wale walikubuhu ni kuwaingiza katika rehabilitation program. Kuwekwa katika jengo, kama gereza-hospitali, ili wanaomsaidia wawe wanamwangalia kwa karibu ,lakini pia ni kumuondolea yale mazingira ya kupata vileo kirahisi.

Huko anaweza kupewa kileo chake lakini dose inapunguzwa kidogo kidogo hadi anaacha kabisa. Pia huwa anapata ushauri nasaha.
wengine wanahitaji medication na ushauri nasaha. kwa hiyo inategemea na ukubwa wa tatizo alilonalo huyo mtumiaji.

Viko vitengo vya kusaidia waathirika wa madawa ya kulevya. Na huwa na mafaniko hasa mtumiaji anapoamua yeye mwenyewe kutafuta msaada ili aweze kuacha kuliko yule atakayeshurutishwa na jamaa zake.
 
Mkuu,
Zipo.
Mara nyingi njia inayotumika ni kwa wale walikubuhu ni kuwaingiza katika rehabilitation program. Kuwekwa katika jengo, kama gereza-hospitali, ili wanaomsaidia wawe wanamwangalia kwa karibu ,lakini pia ni kumuondolea yale mazingira ya kupata vileo kirahisi.

Huko anaweza kupewa kileo chake lakini dose inapunguzwa kidogo kidogo hadi anaacha kabisa. Pia huwa anapata ushauri nasaha.
wengine wanahitaji medication na ushauri nasaha. kwa hiyo inategemea na ukubwa wa tatizo alilonalo huyo mtumiaji.

Viko vitengo vya kusaidia waathirika wa madawa ya kulevya. Na huwa na mafaniko hasa mtumiaji anapoamua yeye mwenyewe kutafuta msaada ili aweze kuacha kuliko yule atakayeshurutishwa na jamaa zake.

Huku uswazi hiyo huduma inaweza kuwafikia hawa jamaa?
Wameathirika kila kitu...uhakika wa kula hawana...matokeo yake wanakaba wenzao...na ndio hao hao utawakuta wakishiriki hivyo vileo!
Au umasikini wa hizi familia zetu inachangia?
 
Back
Top Bottom