Tatizo hili ni la mke wangu tu au wanawake wote married?

Nitamkaribisha ili awashukuru ila pia ndio utakuwa mwanzo wake wa kuwa member humu

Mbona watu wamekushauri usimwoneshe hizi comments? Mengi yaliyosemwa ni kwa ajili yako. Labda kama hajui ID unayotumia. Vinginevyo sikushauri kabisa!
 
Mwana Kwetu; shauri huu ni wa kiutu uzima na unaonyesha ukomavu wa hali ya juu ;mkuu nakushukuru na mawaidha yako na mengine mengi nitayafanyia kazi kwa kina kwani mimi ni msikivu na pia napenda wazo la upande wa pili ndo maana nimelileta hili hapa jamvini nashukuru sana.


Mkuu nashukuru pia, ila tu nakusisitiza kum-compliment shemeji ndo mpango mzima. Najuwa inaudhi kuona makosa madogo madogo mliokwisha kuongea yanajirudia lakini chukulia kuwa ni ubinadamu watu hatuko sawa. Angalia mambo mazuri anayofanya shemeji na mpe credits na umsifiye. Atafurahi kaka nakwambia. Uonyeshe kuwa msaada kwake pale anaposhindwa kutimiza mliokubaliana na umsikilize. Furaha katika ndoa nayo inahitaji palizi mkuu, inatengenezewa mazingira ili iweze kuwepo na idumu bila kusahau kujitoa na uvumilivu.
 
Ukimuuliza mara ya mwisho kumsifu mkewe ni lini ? au mara ya mwisho kutoka nae out ni lini ? au mara ya mwisho kumletea zawadi ni lini ? au hata mara ya mwisho kumkumbatia mkewe bila sababu yoyote ni lini ?
Unaweza kuambiwa hakumbuki ni lini,ndoa sio lele mama na haina fomula ni give and take.
 

Mueleze Mkuu! Mengine madogo madogo unamezea tu na kumuonyesha thamani kubwa mkeo. Tena msomi, anampigia mpaka pasi angeweza kabisa kudai akitoka kazini huwa anachoka sana na kazi ya kupiga pasi ifanywe na msaidizi wa ndani kama wanaye au kama hawana basi wamuajiri.
 
BAK ukimwambia mtu kuwa saa zingine unampikia mkeo au anakuja nyumbani na kukuta ile sidiria na nguo ya ndani aliyoacha bafuni umemuoshea na kuanika wanaweza kushangaa,mwanamke ukimthamini unaweza kushangaa wema anaokufanyia,huyu sidhani hata mara moja amewahi tekenyana na mkewe sebuleni au kugombana na mito au kufukuzana ndani ya nyumba bila sababu NDOA NI RAHA MWANAKWETU FUNGUKA UTASHANGAA!
 
we fanya unayotakiwa kufanya, usimpangie mwenzako ratiba utafikiri mko shule, acha kila kitu kijiendeshe, na kama mambo ya muhimu yanaenda shukuru Mungu
 
we fanya unayotakiwa kufanya, usimpangie mwenzako ratiba utafikiri mko shule, acha kila kitu kijiendeshe, na kama mambo ya muhimu yanaenda shukuru Mungu
shantel nyumba hii inaendeshwa kwa 'memo' kama ofisi,this guy has to lossen-up.
 
ni vyema kufaham katika ndoa kuna stages, hatua mliyofikia ni lazima hayo yatokee, hivyo hapa ndio inakuja maana ya love ni kubeba mapungufu ya mwenzako ambayo hayana madhara katika ndoa yenu. upo kipindi kigumu cha ndoa mkuu. keep it up
 

Hapo kwenye red hebu niambie na nyinyi wanaume hizo tabia ambazo ziko nje ya ulimwengu huu mumezitoa wapi? Specifically wewe hapo mlalamikaji.

Kama ulitaka wa nje ya dunia hii ungemuumba mwenyewe labda, fanya genetic modification uweke hizo tabia unazotaka akazaliwe kwenye test tube. Au labda ukaoe mzungu maana yeye hatoki kijijini.

Grow up man!
 
Mwanakwetu,

Hilo tatizo nadhani ni common kwa wanawake wengi, ok, nisiseme wengi! Ila wa kwangu exactly yuko hivyo hivyo! Nime-fight sana! Nimeamua kuachana naye! Ila it is too bad. Sijajua mwisho wa yote, ila small sampling niliyoifanya ilinionesha kuwa haya matatizo yapo kwingi. If you are such a serious man, naona living with a woman may be difficult or near to impossible.
Wengine huwa wanafikia hatua ya kusema wake wanapenda kudanganywa na wasipodanganywa basi lazima wao wadanganye!! I believe there are some truth on this (serious).
 
shantel nyumba hii inaendeshwa kwa 'memo' kama ofisi,this guy has to lossen-up.
Tatizo la kukremisha,mahusiano hayaendeshwi hivyo, anatakiwa aangalie vitu vya muhimu, coz huwezi mbadilisha mtu mzima kila kitu
 

Wewe Zeburner kweli sijui ni bunsen burner ndiyo inaunguza ubongo wako? Kama wanawake ni mitihani jee wanaume nao ni nani? As if you are half gods! kha munaboa kweli kweli.
 
Bintimkongwe jamaa is beyond help umeona kauli anayotumia 'nikimfukuza' badala ya 'tukitengana' au kuachana.Hiyo statement ya 'nyie wanawake wote mna vitabia' na tunaodai 'tumeoa lulu' eti tunategemea hao wanawake.
The whole idea of marriage is to COMPLIMENT each other its like a key and lock or a bolt and nut.
Two keys or two bolts or two people with similar traits dont make an ideal marrige.
 
haya matatizo na dhani wanawake wengi wanayo sijui huwa wanafanya kama hawajui vile au ni kiburi au ni udhaifu wao kweli tujue tunakaa na weza wetu walio wadhaifu sana hasa katika kurudia rudia mliokubaliana yasitendeke au msifanyiane

Ningekushauri ukagoogle kutafuta nyimbo ya Harry Belafonte 'women are smarter than men...'
 
mwanakwetu punguza wivu kwa wife wako inaonekana unamfatilia sana embu mpe uhuru yeye ana akili mambo yataenda sawa ugomvi utapungua pia jaribu kupuuzia mambo mengi ne we wa kiume kaka mengine unavumilia unauliza kwa upole na upendo mambo yataenda tu!
 

Mtu kama huyu utakuta kesha jenga nyumba bila hata wewe kuwa na habari
 
we fanya unayotakiwa kufanya, usimpangie mwenzako ratiba utafikiri mko shule, acha kila kitu kijiendeshe, na kama mambo ya muhimu yanaenda shukuru Mungu

Hakuna kitu kinachojiendesha chenyewe bila kupangwa kikafanikiwa. Na hakusema kuwa anampangia ratiba. Ni makubaliano ambayo huwa wanafikia pamoja lakini mwenzake hatekelezi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…