Tatizo hili ni la mke wangu tu au wanawake wote married?

Huyu mke ata akipewa talaka nina imani atakaye replace nae atachemsha tu; naona masharti ya huyu bwana magumu.

 
Nimesoma baadhoi ya michango ya watu humu ndani. Mengi yanaweza kusemwa lakini ukweli ni kwamba mke wako ndie mtu unayetegemea kuishi naye for the rest of your life. Sasa kama huwezi kupata comfort kwake what's the use? Haya mambo ya kusema mvumilie nayo yana mwisho wake, binadamu ana uwezo wa kuvumilia mambo fulani for sometime and not forever. Anayofanya mkeo hasa kwa level yake ya elimu ni makusudi tu, kwa elimu yake hawezi kuwa mjinga kiasi hicho, nachukulia kwamba uiliyosema yote ni kweli na sio kuvutia upande wako. Kama vipi mpuuze kwa kadri uwezavyo, sikushauri kumwacha, lakini ni lini utaishi maisha yako? Unategemea atabadilika?
 
kipato chake cha ofisi anakitumiaje?
naanza kuhisi kama wewe ni controling sana..
pengine una tatizo hujijui.....
angekuwa na tatizo kubwa asingekuwa anaomba kurudiana ukimfukuza

Mkuu huyu mama yuko very free na income yake.Kwa ufupi mimi mshahara wangu unatumika kwa kuendesha familia ila yeye akaona siyo vema akae tu aangalie. Positive side yake ni very good katika kutumia mapato yake kwa manufaa ya familia kwani yuko transparent ingawaje ana keep akaunti yake mwenyewe na mimi yangu. sometime akitingwa hunipa ATM yake nimchukulie hela nimletee na huwa nafanya hivyo kwa uaminifu na moyo mweupe.
 
Hayo ndio mambo ya nyumba na unyumba..kazi kweli kweli..kaka kila mtu anamatatizo yake ila vumilia mambo yakuwa powa.ila muhimu jaribu kuongea naye jinsi unavyopenda na unavyojisikia pindi anapofanya kwa jinsin unavyopenda..
 

take it from me...

mkeo angekuwa wangu,ningeringa sana...
na ukimuacha utajuta mno...na watu watamuoa so fast,utashangaa
 

Kuvumiliana ni kweli kuna mwisho. Hivi niendelee kuvumilia tu au what should I do. Na kama nitampuuza ndo itakuwa ndoa ya namna gani?
 
Hata mimi nilili note hilo. Huyo mwanamke amefundwa kwao. Yani umfukuze aende kwa mama mkwe; hiyo ni bahati kubwa aisee. Wengi wanaenda usikokujuai ili hata ukimtafuta usimpate ng'o. Nadhani hata mama mkwe anajua how lucky mwanae his; ndio maana anaomba msamaha ndoa isife.

kwanza ana bahati....
mwanamke ana masters na unamfukuza anakwenda kwa mama mkwe kuomba mrudiane????

aulize wenzie waliooa wenye diploma tu za kuunga unga inakuwaje?lol
 
take it from me...

mkeo angekuwa wangu,ningeringa sana...
na ukimuacha utajuta mno...na watu watamuoa so fast,utashangaa

Uko right pia unaweza ukawa na assumption ambayo si kweli kwani huwa namfukuza kabisa na ni heri umkate panga kuliko aondoke . Kama anajua yuko so marketable si angekimbia tu anangangania nini wakati hatuwezi kuelewana tena sometime vitu vidogo ambavyo havihitaji mtu kuwa hata na elimu ya form four ili kuvielewa?
 
Una bahati sana hayo mapungufu alonayo yanamezwa na mazuri yake. Kuna watu wana wake mizigo lakini wanavumilia knowing divorce ina cost. Kwa kupata mke asiye msiri na mchoyo na pato lake ni bahati sana kaka.


 
<br />
<br />
 
kwanza ana bahati....
mwanamke ana masters na unamfukuza anakwenda kwa mama mkwe kuomba mrudiane????

aulize wenzie waliooa wenye diploma tu za kuunga unga inakuwaje?lol

Huwa siyo hivyo tu wakati akisha chemsha na ugomvi kutokea mkubwa ukianza kumwambia sikutaki tena yeye kuliko aondoke kuna wakati unamkuta sebuleni anaendelea kupasi nguo zako na baada ya hapo anakutengenezea chai ingawaje inakuwaga vigumu kunywa kutokana na hasira.
 

mkuu kuna personility ya watu inaitwa 'PEFERCTIONIST'
hebu ifuatilie hiyo,yaweza kuwa wewe upo group hilo
una sound like that...
 
ngoja nisikie version ya mke lol manake JF siku hizi haiishi drama za mke na mume heheee
 
<br />
<br />
Mke una kafundwa akafundika,eti umuache.au una smallhouse nini?
 
Una bahati sana hayo mapungufu alonayo yanamezwa na mazuri yake. Kuna watu wana wake mizigo lakini wanavumilia knowing divorce ina cost. Kwa kupata mke asiye msiri na mchoyo na pato lake ni bahati sana kaka.

Nasema ukweli hana uchoyo wa aina yoyote kwenye hela yake na sometime nikimaliza fedha mapema kabla ya mwisho wa mwezi kama kawaida ya wanaume wengi basi analichukua hilo jukumu bila malalamiko wala ubishi.

Pamoja na haya mazuri bado amani ni muhimu kwani fedha si suluhisho la kila kitu kwani si kila kitu fedha inaweza kununua. kama moyo wangu ungekuwa kwenye fedha zake basi ningeona nina ndoa nzuri sana ila sometime kero zina supersede umuhimu wa hizo fedha.
 
ningumu aisee
kwani ukidharau itakuwaje?
ni vitu gani hasa?

kuna vitu vidogo kama ukipiga simu,simu yake iko kwenye begi,utajipa presha sana
most womens wako hivyo..au kusahau kitu ulichomsisitiza n,k

Nakubaliana nawe BOSS kwamba kama makosa yenyewe si makubwa kiasi hicho basi jaribu kuyasamehe na ili kutoleta mifarakano ndani ya ndoa au unapotaka kuyaleta makosa yake ili myajadili basi mfanye kama ni maongezi tu ya kawaida badala ya kupandisha sauti zenu na kuongea kwa jazba kubwa na hatimaye kosa dogo tu linazaa ugomvi mkubwa sana.

Niliwahi kuona ugomvi mkubwa sana kisa sufuria iliyopikiwa ugali. Hii ilileta kasheshe kubwa sana ndani ya ndoa ile na kuharibu kabisa amani iliyokuwepo na baadaye magomvi yakaongezeka katika idara nyingine na hatimaye ndoa kuvunjika. Hivyo kama makosa yake si makubwa kiasi hicho basi jaribu kuyavumilia vinginevyo ombeni msaada kwa watu mnaowaamini ili wawasaidie kutatua matatizo yenu.
 

you sound like control freak,na hii ndoa umeichoka unamtafutia reasons tu mwenzio za kujustfy kuchoka kwako....wanaume sijui mkoje mnataka kwenda kutafuta nyumba ndogo nendeni sio mnaanza kumtafuta mchawi kwa kutafuta vikosa vidogo vidogo na kuanza kuvikuza,mkeo hana tatizo wewe ndio una tatizo kama ukimfukuza haondoki,ondoka wewe,wewe si ndio umeichoka ndoa? kwa nini yeye aondoke?
 

wewe ulihitaji uoe 'shangingi la mjini' kwanza....halafu ndo uje umuoe huyo mkeo...
ndio ungeelewa....kwa nini tunaona hayo matatizo yako sio makubwa kabisa...
 
Kuvumiliana ni kweli kuna mwisho. Hivi niendelee kuvumilia tu au what should I do. Na kama nitampuuza ndo itakuwa ndoa ya namna gani?

Kwa kweli endelea tu kumuelekeza na kumuongoza kwani kutokana na post zako huyo mwanamke ndivyo alivyo na hafanyi hivyo kwa makusudi. Inaweza kuchukuwa muda mrefu kubadilika kidogo kidogo na awe kama unavyotaka wewe.

Kama alivyoongea mdau mmoja inawezekana wewe ni perfectionist na tatizo unaloliona wewe mwenzako anaona ni sawa tu. Subiri watoto wakue wamsaidie mama yao katika hayo yanayokukwaza wewe (mfano usafi).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…