Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,470
- 40,593
Kwenye mfumo wa Elimu Yetu tuna matatizo mengi sana ambayo kwa haraka haraka inawezekana ikatuchukua hata miaka zaidi ya 20 kuyarekebisha, tena kama tukiwa makini na tuliodhamiria kufanya marekebisho yanayotakiwa.
Kwenye Mfumo wetu wa Elimu watu waliofundishwa kuwa Maafisa Elimu kwenye vyuo vyetu vikuu, kutokana na ukosefu wa ajira ndiyo wanageuka kuwa waalimu kwenye shule zetu za Msingi na Sekondari. Mtu aliyeandaliwa kwa miaka mitatu au zaidi kuwa msimamizi wa Sera za Elimu, mitaala, na usimamizi wa mifumo ya Elimu ndiyo wanakuwa mwalimu.
Kwenye mfumo wetu wa Elimu Kanuni na Taratibu za kuendesha elimu zinashangaza sana. Elimu ambacho ni kitu muhimu sana kwa Taifa kama ulivyo moyo kwa viumbe hai, imeachwa mikononi mwa mtu mmoja tu, WAZIRI WA ELIMU.
Waziri wa Elimu anaweza kubadili mitaala ya shule, mfumo wa kusoma (Idadi ya madarasa), mfumo wa kusahihisha, idadi ya masomo mashuleni, mifumo ya ajira na nafasi za uongozi kwa waalimu, bila ya kuingiliwa na mtu yeyote yule.
Matokeo yake Elimu yetu imekuwa na mabadiliko kwa kadri Waziri wa Elimu aliyeko madarakani anavyoona inafaa. Siyo Bunge wala Rais aliyemteua waziri wa Elimu wanaweza kugeuza maamuzi yanayotolewa na Waziri wa Elimu. Matokeo yake Elimu yetu hutegemea zaidi Kudra za Mwenyezimungu kumjaalia "Hekima" na "Busara" waziri wa Elimu atakayekuwa madarakani kwa wakati husika.
Ukienda kwenye mashule ya Umma utashangaa ndiko kanuni za kuendesha shule hazifuatwi kabisa. Kanuni za wanafunzi darasani inataka wanafunzi wawe wanafunzi 45 kwa kila darasa. Lakini kwenye shule za Umma darasa moja linakuwa na zaidi ya watoto 100 kwa wakati mmoja.
Kwa mujibu wa Kanuni za Elimu angalau kwa kiwango cha chini kabisa Kitabu kimoja cha Kiada, kinatakiwa kitumiwe na watoto si zaidi ya wawili au kwa watatu kwa kiwango cha juu kabisa. Nenda sasa kwenye shule za Umma ukute darasa zima lenye watoto 100 lina vitabu saba tu vya kiada kwa somo husika.
Kwa ngazi ya shule za Sekondari nako hali siyo nzuri hata kidogo. kwa ivo kwa Tanzania Tatizo la mfumo wa Elimu linaonekana zaidi kwenye shule za umma na siyo kwenye shule za Binafsi.
Kwenye Mfumo wetu wa Elimu watu waliofundishwa kuwa Maafisa Elimu kwenye vyuo vyetu vikuu, kutokana na ukosefu wa ajira ndiyo wanageuka kuwa waalimu kwenye shule zetu za Msingi na Sekondari. Mtu aliyeandaliwa kwa miaka mitatu au zaidi kuwa msimamizi wa Sera za Elimu, mitaala, na usimamizi wa mifumo ya Elimu ndiyo wanakuwa mwalimu.
Kwenye mfumo wetu wa Elimu Kanuni na Taratibu za kuendesha elimu zinashangaza sana. Elimu ambacho ni kitu muhimu sana kwa Taifa kama ulivyo moyo kwa viumbe hai, imeachwa mikononi mwa mtu mmoja tu, WAZIRI WA ELIMU.
Waziri wa Elimu anaweza kubadili mitaala ya shule, mfumo wa kusoma (Idadi ya madarasa), mfumo wa kusahihisha, idadi ya masomo mashuleni, mifumo ya ajira na nafasi za uongozi kwa waalimu, bila ya kuingiliwa na mtu yeyote yule.
Matokeo yake Elimu yetu imekuwa na mabadiliko kwa kadri Waziri wa Elimu aliyeko madarakani anavyoona inafaa. Siyo Bunge wala Rais aliyemteua waziri wa Elimu wanaweza kugeuza maamuzi yanayotolewa na Waziri wa Elimu. Matokeo yake Elimu yetu hutegemea zaidi Kudra za Mwenyezimungu kumjaalia "Hekima" na "Busara" waziri wa Elimu atakayekuwa madarakani kwa wakati husika.
Ukienda kwenye mashule ya Umma utashangaa ndiko kanuni za kuendesha shule hazifuatwi kabisa. Kanuni za wanafunzi darasani inataka wanafunzi wawe wanafunzi 45 kwa kila darasa. Lakini kwenye shule za Umma darasa moja linakuwa na zaidi ya watoto 100 kwa wakati mmoja.
Kwa mujibu wa Kanuni za Elimu angalau kwa kiwango cha chini kabisa Kitabu kimoja cha Kiada, kinatakiwa kitumiwe na watoto si zaidi ya wawili au kwa watatu kwa kiwango cha juu kabisa. Nenda sasa kwenye shule za Umma ukute darasa zima lenye watoto 100 lina vitabu saba tu vya kiada kwa somo husika.
Kwa ngazi ya shule za Sekondari nako hali siyo nzuri hata kidogo. kwa ivo kwa Tanzania Tatizo la mfumo wa Elimu linaonekana zaidi kwenye shule za umma na siyo kwenye shule za Binafsi.