Tatizo la figo

shalet

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2013
Posts
3,430
Reaction score
3,547
habar,
nimekuwa nikisumbuliwa kwa tatizo la figo kwa miezi 5 sasa kila nikipima napewa dawa lakin tatizo linaendelea dozi ikiisha, ninasumbuliwa sana na kuvimba miguu nilipima renal test mara ya mwisho ikaonyesha 204.4 creatinine nikapewa dawa zifuatazo.
1. lasix
2. preonsolone
3. amplix
4. ciprofloxin
nikaambiwa tatizo likiendela nikaonane na doctor muhimbili anaitwa dr. linda yeye ni mtaalamu wa figo, lakini kwa sasa nipo udom na ninafanya mitihani ya mwisho u.e naomba ushauri nitumie dawa gani tena au nifanyaje manake miguu bado inavimba na tatizo inaonekana limeendelea.

NB: nilichukua vipimo vya echo nipo sawa, x-ray kifua nipo sawa.
thanks in advance.
 

pole sana mkuu kwa tazizo hilo,nakuombea kwa mungu inshallah akupe wepesi upone kabisa,ngoja nikuitie dr. MziziMkavu anaweza kukupa mwangaza nn cha kufanya,pole sana kaka
 
Last edited by a moderator:
Mkuu shalet Pole sana kwa hayo matatizo yako ya Figo nina dawa za aina 2 za Tiba Mbadala ukiweza moja kati ya hizo dawa 2 Tumia kwa muda wa siku kama 10 kisha nenda tena hospitali ukapime ili

kujuwa je bado una matatizo ya Figo? ukitumia Dawa moja kati ya hizo mbili kwa muda wa siku 10 na umekwenda

Hospitali wamekupima na kugunduwa bado unaumwa Figo tumia dawa ya pili siku 10 tena kisha nenda ukapime Figo kujuwa je bado unaumwa na hayo matatizo ya Figo? ukisha uje hapa unipe Feedback. Dawa zenyewe hizi hapa :

Dawa ya Figo Fanya hivi (1) chukua ndevu za Mahidi mabichi achemshe kisha achuje maji yake yakishapoa anywe ujazo wa kikombe cha kahawa asubuhi na mchana kwa muda wa mwezi kwa uwezo Mwenyeeziş Mungu utapona.

Dawa ya Maradhi ya Figo (2) Dawa ya Maradhi ya Figo Kunywa mkojo wako mwenyewe kwa muda wa siku 10 tu zinatosha kila siku asubuhi ukinge mkojo wako mwenyewe kipimo cha glasi 1

kabla ya kula kitu unywe kisha ukae baada ya saa 1 unaweza kula chakula chako cha kawaida

ufanye hivyo kwa muda wa siku 10 kisha nenda Hopitali kwa Daktari kupima utakuta huna tena

Maradhi ya Figo Tumia hiyo Dawa kisha uje hapa unipe feedback.

Muhimu unapotumia Dawa zangu acha kutumia Dawa za hospitali Tafadhali sana usichanganye Dawa.

pole sana mkuu kwa tazizo hilo,nakuombea kwa mungu inshallah akupe wepesi upone kabisa,ngoja nikuitie dr. MziziMkavu anaweza kukupa mwangaza nn cha kufanya,pole sana kaka
Mkuu steveachi hujambo lakini? Habari za Masiku?
 
thanks mkuu nitaanza na hiyo ya MziziMkavu itakupa feedback nikikamilisha dozi
 
Last edited by a moderator:

Unaweza kutumia Majani ya Basil na Asali. Uliza Kariakoo. Pia supu ya maharage mekundu ni tiba kamili. Kwa details pitia: Mafanikio Na Afya Njema: Je Una Matatizo Ya Figo? - Home Remedies for Kidney Stone
 

nipo mkuu wangu,nimeona nikumensheni umsaidie shalet coz moyo wa imani umenigusa kwa tatizo
lake lkn ujuzi sina,pole sana kwa majukumu kaka,g9t
 
Last edited by a moderator:
Pole sana mkuu
Nakushauri tumia aloe berry nectar tatizo litakwisha kabisa. Unaweza kunicheki kwa ushauri na kupata msaada wa tiba kwa namba 0768 955 185
 
mkuu MziziMkavu asalaam aleykum
nashukuru kwa ushauri wako ulionipa kwa mazingira ya chuo nilianza na dozi ya mkojo kwa siku 10..... kama nilivyokuwa nikutumia dawa za hospitali niliendelea vizuri lakini ile hali ikarudi tena safari hii nikiwa dar es salaam nilishindwa dozi hiyo ya pili kwa sababu ya mazingira ikanibidi niende clinic ya figo MNH nilifanyiwa vipimo ikaonekana bado kuna tatizo kwenye figo nikapewa dozi ya miezi miwili
kama ifuatavyo.
atorvastatin, lasix, enalypril, losartan potassium na prednsolone
pamoja na vipimo vya figo nilipima hiv i & ii na hepatitis b & c sikuwa na tatizo
nashukuru sana kwa ushauri wako ninaendelea na dozi hii yahospitali mpaka mwezi ujao .
Mungu akubariki kwa muda wako unaotumia kutoa ushauri hapa jf.
thanks alot!!!!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu MziziMkavu vipi ikiwa mkojo hautoki? Nina mgonjwa ambaye figo zake zimefeli, ana siku 3 sasa hajapata haja ndogo. Je kuna tiba ya tatizo la figo katika hatua hiyo?
Mwana-JF yeyote mwenye ujuzi, utaalam au uzoefu wa tatizo hili naomba msaada kwenu. Mgonjwa yuko mkoani, amelazwa hospitali.
 
Last edited by a moderator:
Dawa ya Figo Fanya hivi (1) achukue ndevu za Mahindi mabichi achemshe

kisha achuje maji yake yakishapoa anywe ujazo wa kikombe cha kahawa

asubuhi, mchana na usiku kwa muda wa mwezi kwa uwezo Mwenyeezi Mungu utapona.

 
Endelea kutumia Dawa za hospitali kisha uje hapa utupe Feedback. Ninakutakia kila la kheri inshallah.
 
Dawa ya Figo Fanya hivi (1) achukue ndevu za Mahindi mabichi achemshe

kisha achuje maji yake yakishapoa anywe ujazo wa kikombe cha kahawa

asubuhi, mchana na usiku kwa muda wa mwezi kwa uwezo Mwenyeezi Mungu utapona.


Asante sana kwa kujibu haraka. Lakini hapo juu umeonya, mtu asichanganye dawa zako na za hospitali. Itakuwaje kwa huyu ambaye bado amelazwa?
 
Asante sana kwa kujibu haraka. Lakini hapo juu umeonya, mtu asichanganye dawa zako na za hospitali. Itakuwaje kwa huyu ambaye bado amelazwa?
Mwache atumie dawa yangu na hiyo ya Hospitali pamoja itamsaidia inshallah..............
 
Mwache atumie dawa yangu na hiyo ya Hospitali pamoja itamsaidia inshallah..............

Asante Mkuu. Barikiwa sana. Wacha sasa nisake wachoma mahindi maana kipindi hiki mahindi mabichi na nadra. Shukrani kwako MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:
Asante Mkuu. Barikiwa sana. Wacha sasa nisake wachoma mahindi maana kipindi hiki mahindi mabichi na nadra. Shukrani kwako MziziMkavu
Mwambie anywe Maji ya Uvuguvugu kwa wingi itamsaidia pia hayo matatizo ya figo.

PINDA AWAAMBIA WATANZANIA: KUNYWENI MAJI MENGI KUZILINDA FIGO ZENU


*Azindua SMS ya ”Ijue Afya ya Figo Yako” kwenda 15021 kupitia TIGO
*Aonya wanaokimbilia kununua dawa bila kupima


………………………………………………………….


WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewahimiza Watanzania kuwa na tabia ya kunywa maji mengi kila siku ili kujikinga na matatizo ya figo ambayo yanazidi kuongezeka kila siku.

Ametoa wito huo leo mchana (Alhamisi, Machi 14, 2013) wakati akizungumza na mamia ya wananchi wa mji wa Arusha waliohudhuria kilele cha maadhimisho ya Siku ya Afya ya Figo Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya hospitali ya AICC jijini humo.

Kaulimbiu ya Siku ya Afya ya Figo Duniani mwaka huu ni “Figo Salama kwa Maisha yako: Epusha Madhara Makubwa kwa Figo” au “Kidneys for Life: Stop Acute Kidney Injury”

Waziri Mkuu alisema mtoto wa miaka 10 hadi mtu mzima wanatakiwa wanywe maji kiasi kisichopungua lita moja na nusu kwa siku wakati mtoto mwenye mwaka mmoja anatakiwa anywe maji yasiyopungua nusu kikombe (sawa na mililita 100) na kwamba kiasi hicho huongezeka kadri umri wa mtoto unavyoengezeka. “Hii itasaidia kuhakikisha hawaishiwi maji mwilini,” aliongeza.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, imekadiriwa kuwa watu milioni mbili hupoteza maisha kila mwaka kutokana na maradhi ya ghafla ya figo wakati asilimia 20 ya vifo vya wagonjwa waliolazwa hospitalini husababishwa na maradhi hayo.

“Wataalam wanasema maambukizi ya magonjwa hayo husababisha madhara makubwa ya figo (Acute Kidney Injuries) ambayo huchangia kwa kiasi kikubwa kuharibika kwa utendaji kazi wa figo. Hali hiyo husababisha watu kupata ugonjwa wa ghafla wa figo (mshtuko wa figo) na pia kusababisha athari kubwa kwenye figo na kuzifanya zishindwe kufanya kazi ipasavyo,” alisema.

Alisema maradhi yanayoweza kujitokeza ghafla na kuharibu figo hayajatiliwa mkazo ipasavyo, hasa katika nyanja za utoaji mafunzo ya tiba, utafiti na elimu ya afya ya figo kwa umma. “Hali hii husababisha kutotumika kikamilifu kwa fursa za kubaini maradhi yanayojitokeza ghafla na kuharibu figo; pia inaathiri utoaji huduma za afya ya figo usiokidhi, na hivyo wagonjwa kulazwa kwa muda mrefu hospitalini,” alisititiza.

Akifafanua umuhimu wa kuwepo haja ya upimaji afya ya figo, Waziri Mkuu alisema Machi, 2011 Taasisi ya Figo Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ilitoa huduma ya bure na kuwachunguza watu 3,500 ambapo watu 1,200 walikutwa na magonjwa ya figo.

“Mwaka huu 2013 katika maadhimisho yanayoendelea katika Jiji la Arusha, yaliyoanza Machi 11, 2013, jumla ya watu 2,020 kufikia saa 7.00 mchana jana walisajiliwa na kati yao 1,640 walifanyiwa uchunguzi. Kati yao wananchi 37 walipatikana na maradhi ya figo, wengine 219 walipatikana na matatizo ya shinikizo la juu la damu. Wananchi 65 kati ya 141 waliofanyiwa uchunguzi kwa kipimo cha Ultra Sound na walikutwa na matatizo. Jumla ya wananchi 63 walifanyiwa uchunguzi wa moyo wakwa vipimo vya ECHO na ECG.

Alisema jukumu kubwa kwa upande wa Serikali ni kuhakikisha kuwa fedha, vifaa, vifaa tiba na dawa za kukabiliana na ugonjwa wa mshtuko wa figo vinapatikana kwa wakati ili kulinda afya ya jamii. “Katika kudhihirisha azma hii ya Serikali, tayari tuna Kitengo cha Huduma za Tiba ya Magonjwa ya Figo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kitengo hiki kinatoa huduma kwa wagonjwa wote wanaohitaji huduma za tiba ya magonjwa ya figo. Chuo Kikuu cha Dodoma kimeanzisha utoaji wa huduma za tiba ya magonjwa ya figo. Ninazo taarifa kwamba, pale Dodoma kuna mashine za kisasa 10 za kusafishia damu.”

Alisema hospitali za rufaa za Bugando, KCMC na Mbeya ziko kwenye hatua mbalimbali za maandalizi ya kuanzisha huduma za tiba ya magonjwa ya figo. “Matarajio ni kwamba, kuwepo kwa huduma hizo kutaliwezesha Taifa katika kupambana na magonjwa ya figo,” aliongeza.

Alikemea tabia ya baadhi ya watu kujiamulia kununua dawa na kumeza bila kufanyiwa uchunguzi wa kitatibu na kuonya kuwa kuwa tabia hiyo inaweza kusababisha matatizo makubwa ya kiafya.

“Tuwaelimishe Watanzania umuhimu wa kuhakikisha kuwa wagonjwa wanaougua maradhi mengine wanapelekwa hospitali na wanapata tiba sahihi kwa kuzingatia matumizi sahihi ya dawa kama inavyoelekezwa na wataalam wa afya. Vilevile, ni vizuri kuwahi katika vituo vya kutolea huduma za afya mara tuonapo dalili za ugonjwa ili kupatiwa tiba inayostahiki mapema,” alisisitiza.

Waziri Mkuu alizindua Programu ya Ujumbe Mfupi wa Simu ya Mkononi (SMS) ya IJUE AFYA YA FIGO YAKO kwa kutuma ujumbe wenye neno FIGO kwenda namba 15021 kupitia mtandao wa simu wa Tigo ambapo mhusika atajibu maswali kadhaa na kupatiwa taarifa.

Aliishukuru kampuni ya simu ya mkononi ya Tigo kwa kutoa huduma hiyo bure na kuwasihi wananchi waitumie ili kupata taarifa juu ya afya ya figo zao.

Naye Mwenyekiti waTa asisi ya Figo Tanzania, Jaji Frederick Werema, aliwasihi Watanzania kujitolea kwa hali na mali kuiunga mkono taasisi hiyo ili iweze kufanya shughuli zake kwenye mikoa mingi zaidi.

Chanzo. PINDA AWAAMBIA WATANZANIA: KUNYWENI MAJI MENGI KUZILINDA FIGO ZENU | FULL SHANGWE BLOG
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…