Tatizo la keloids

Tatizo la keloids

ameline

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
2,292
Reaction score
1,151
Salaam ndugu zangu,. naomba msaada kwa anayejua matibabu ya keloids(uvimbe fulani mweusi huota kifuani, shingoni, mgongoni au hata usoni) kuna mdogo wangu |(wa kike)ana uvimbe huo nitaweka picha kama haitaeleweka, ana miaka kumi sasa akiwa na tatizo hilo, upo kifuani kila nikimpeleka hosp, doct anamwambia akizikata zitaota tena, labda twende KCMC ndipo tutapata madoctor wazur wanaokata na kuchoma, au anaweza kuziacha tu hazina madhara yeyote, wakati yeye anasema zinawasha wakati mwingine zinachoma kama sindano na zinaongezeka ukubwa.Sasa tupo dillema sijui nifanyeje ndugu zangu. ni kweli akikata hazitarudi? au tiba yake hasa ni nini au kama kuna mdau ambaye ameshawahi kuziondoa anishuhudie jamani maana naona hii kitu imemuathiri kisaikolojia kabisa huyu binti Ahsanteni
 
Salaam ndugu zangu,. naomba msaada kwa anayejua matibabu ya keloids(uvimbe fulani mweusi huota kifuani, shingoni, mgongoni au hata usoni) kuna mdogo wangu |(wa kike)ana uvimbe huo nitaweka picha kama haitaeleweka, ana miaka kumi sasa akiwa na tatizo hilo, upo kifuani kila nikimpeleka hosp, doct anamwambia akizikata zitaota tena, labda twende KCMC ndipo tutapata madoctor wazur wanaokata na kuchoma, au anaweza kuziacha tu hazina madhara yeyote, wakati yeye anasema zinawasha wakati mwingine zinachoma kama sindano na zinaongezeka ukubwa.Sasa tupo dillema sijui nifanyeje ndugu zangu. ni kweli akikata hazitarudi? au tiba yake hasa ni nini au kama kuna mdau ambaye ameshawahi kuziondoa anishuhudie jamani maana naona hii kitu imemuathiri kisaikolojia kabisa huyu binti Ahsanteni

Pole sana ameline na tatizo la mdogo wako, Keloids ni kweli huwa ukukta na kuzitoa zinarudi na hivyo huyo hata akitogwa masikio ama kuumia kwa aina yeyote kwenye ngozi yake hata kukwaruzwa na kijiti zitatokea, huwa ni familial kwa maana ya kuwa huenda ipo kwenye familia na ni kule kupona kupita kiais kwa jeraha, excessive tissue healing. Kuna sindano za steriod ambazo hupunguza na madaktari wa ngozi wamekuwa wakizitumia sasa inategemea na ukubwa wa keloid na mahali ilipo pia. Kama ulivyosema umeshauriwa kwenda KCMC na mimi ningekushauri uende pia pale idara ya ngozi kuna wataalamu wa ngozi wataweza kukushauri vyema zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana ameline na tatizo la mdogo wako, Keloids ni kweli huwa ukukta na kuzitoa zinarudi na hivyo huyo hata akitogwa masikio ama kuumia kwa aina yeyote kwenye ngozi yake hata kukwaruzwa na kijiti zitatokea, huwa ni familial kwa maana ya kuwa huenda ipo kwenye familia na ni kule kupona kupita kiais kwa jeraha, excessive tissue healing. Kuna sindano za steriod ambazo hupunguza na madaktari wa ngozi wamekuwa wakizitumia sasa inategemea na ukubwa wa keloid na mahali ilipo pia. Kama ulivyosema umeshauriwa kwenda KCMC na mimi ningekushauri uende pia pale idara ya ngozi kuna wataalamu wa ngozi wataweza kukushauri vyema zaidi.

asante sana mamy, kupata ujumbe huu ni nafuu kwake, sindano ameshachoma ndo maana nilichukua uamuzi wa kuziondoa kama itawezekana,. nashukuru sana kwa mchango wako, ubarikiwe
 
Back
Top Bottom