Quartz360
Senior Member
- Mar 27, 2023
- 133
- 317
"Lack of Capital"
Umekua ni msamiati unaoimbwa kila siku kila Kona ya nchi yetu na hata nje ya nchi pia.
Kijana akiambiwa kwa nini hufanyi kazi yeyote ama hujajiari,, Anasema sina mtaji.
Kiukweli imekua ni changamoto kubwa Sana hasa kwa Biashara zinazochipukia "Startups"
Lakini ukweli mchungu ni kuwa, hili tatizo HALITAISHA KAMWE Kama vijana wenyewe hawataamua kupambana wenyewe kusaka fursa za kuwapatia kipato
Usitarajie hata siku moja serikali itaweza kutatua hii changamoto, Kama ajira tuu zimekua ngumu iweje kuhusu MITAJI.
Kazi ya serikali ni kuandaa tu mazingira wezeshi,,, Lakini nalo imekua ni changamoto......
Hata serikali isipofanya yote hayo hakuna cha kuwafanya, usitegemee mbunge wako akutengenezee ajira, it's absolutely impossible, usitegemee serikali iwezeshe vijana wote, it's absolutely impossible also. Ni Jambo la kupambana tu hakuna namna,,,, ukitegemea outside Forces ndo ufanikiwe itakuwa changamoto Sana.
Bila kujitoa mhanga kusaka fursa, maisha yatakuwa magumu sana. Ni vyema kukubaliana na hali, kupambana iwe ndo nguzo mhimu katika kutafuta mafanikio.
Hivyo, vijana wasibweteke na kuanza kuitupia lawama serikali ama hata familia zao, ni wakati wa kupambana, hakuna kutia huruma Tena, ni wakati wa kutengeneza msingi imara wa kiuchumi, hakuna kushinda vijiweni kutupa lawama kwa yeyote.
Mabadiliko yaanzie katika kubadili fikra kwanza, kuongeza maarifa mapya, nidhamu, juhudi na malengo katika kazi ndio itakuwa njia thabiti katika kuyaelekea mafanikio.
Big up! kwa wapambanaji wote.
#MyCountryPeople[emoji1241].
Umekua ni msamiati unaoimbwa kila siku kila Kona ya nchi yetu na hata nje ya nchi pia.
Kijana akiambiwa kwa nini hufanyi kazi yeyote ama hujajiari,, Anasema sina mtaji.
Kiukweli imekua ni changamoto kubwa Sana hasa kwa Biashara zinazochipukia "Startups"
Lakini ukweli mchungu ni kuwa, hili tatizo HALITAISHA KAMWE Kama vijana wenyewe hawataamua kupambana wenyewe kusaka fursa za kuwapatia kipato
Usitarajie hata siku moja serikali itaweza kutatua hii changamoto, Kama ajira tuu zimekua ngumu iweje kuhusu MITAJI.
Kazi ya serikali ni kuandaa tu mazingira wezeshi,,, Lakini nalo imekua ni changamoto......
Hata serikali isipofanya yote hayo hakuna cha kuwafanya, usitegemee mbunge wako akutengenezee ajira, it's absolutely impossible, usitegemee serikali iwezeshe vijana wote, it's absolutely impossible also. Ni Jambo la kupambana tu hakuna namna,,,, ukitegemea outside Forces ndo ufanikiwe itakuwa changamoto Sana.
Bila kujitoa mhanga kusaka fursa, maisha yatakuwa magumu sana. Ni vyema kukubaliana na hali, kupambana iwe ndo nguzo mhimu katika kutafuta mafanikio.
Hivyo, vijana wasibweteke na kuanza kuitupia lawama serikali ama hata familia zao, ni wakati wa kupambana, hakuna kutia huruma Tena, ni wakati wa kutengeneza msingi imara wa kiuchumi, hakuna kushinda vijiweni kutupa lawama kwa yeyote.
Mabadiliko yaanzie katika kubadili fikra kwanza, kuongeza maarifa mapya, nidhamu, juhudi na malengo katika kazi ndio itakuwa njia thabiti katika kuyaelekea mafanikio.
Big up! kwa wapambanaji wote.
#MyCountryPeople[emoji1241].