habari zenu wakubwa naombeni ufafanuzi kuhusiana na tatizo hili kwamba mgonjwa huanguka na kupoteza fahamu mara kwa mara pasipo kupata dalili zozote kama kuumwa kichwa sana au kizunguzungu kabla ya kutokewa hujikuta yeye ni mtu wa kusimuliwa tu kama umepoteza fahamu umeanguka yaani mgonjwa baada kupata fahamu hushindwa kujielewa kabisa kama alianguka mpaka aambiwe kwamba umeanguka ndo ajitambue vinginevyo labda atajihisi yupo ktk mazingira tofauti tu kwamfano alikua anatembea akaanguka anapopata fahamu zake akajiona yupo chini kalala