Tatizo la Kutamka "R" na "L"

Tatizo la Kutamka "R" na "L"

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
TATIZO LA KUTAMKA "R" NA "L"
Hili tatizo la shida ya kushindwa kutofautisha kati ya "R" na "L" ni tatizo jipya.

Nyakati zetu tunasoma shule ya msingi katika miaka ya 1950 tatizo hili halikuwapo

Walimu walikuwa makini kuanzia miaka ya awali katika kunyoosha matamshi ya wanafunzi yawe ya Kiswahili au Kiingereza.

Nashangaa leo kuwasikia watu waliofika hadi chuo kikuu hawajui tofauti ya "R" na "L".

Najiuliza inawezekanaje?
Hawa wamesomeshwa na walimu gani?

Najiuliza kuwa hata huko vyuoni walikuwa wakitamka, "Plesident," badala ya "President?"

Nilipokuwa sekondari niliingia katika mchuano wa English Elocution shule za Dar-es-Salaam.

Shule yetu St. Joseph's Convent miaka yote tukishinda nafasi ya kwanza na sababu ni kuwa shule yetu ilikuwa English Medium toka enzi na enzi.

Kiingereza kilikuwa ndiyo Kiswahili chetu.

Imefika siku ya mchuano kuchagua watakaokwenda kuwakilisha shule yetu.

Kwangu haikuwa shida wala tabu kuhifadhi ukurasa mzima wa William Shakespeare.

Mwalimu wangu wa Kiingereza Mrs. Grant kasimama mbele yangu kunisikiliza.

Darasa zima liko kimya.

Nimechagua hotuba ya Dr. Martin Luther King "I Have a Dream."

Nashuka bila tabu bila kujikwaa popote.

Hifdhi nilijifunza chuoni yaani madrasa na walimu wangu wa kwanza nawakumbuka Mwalimu Badi na Mwalimu Mussa walionihifadhisha majina ya Mtume kwenda nyuma.

Yote yalikuwa yamenasa.
Nilikuwa hata darasa la kwanza sijaanza.

Hiki kilikuwa Kiarabu na ilinisaidia sana baadae katika matamshi yangu katika lugha ya Kiingereza.

Ndiyo maana niliingia kwenye mchuano bila shida wala hofu.

Sikupita mpambano huu.
Nini sababu ya kushindwa kwangu?

Mrs. Grant mwalimu wetu wa Kiingereza hakunipasisha kwa kuwa mshindani mwenzangu alikuwa na "accent" nzuri akikizungumza Kiingereza kama Mwingereza mwenyewe.

Mrs. Grant alikuwa Mwingereza.

Haikuwa tatizo la "Glound" badala ya "Ground" lililonifanye nishindwe.

Ndiyo leo nashangaa kumsikia mtangazaji wa Radio na TV akitamka, "Blitish Bloadcasting Coplation."

Maini yananikatika nikisikia matamshi hayo.
Tunatokaje katika shida na dhiki hii?
 
Mzee nashukuru umeleta hii mada jukwaani.Shida kubwa ni elimu inayotolewa hivi sasa ukifatilia wanao shindwa tofauti ya R na L ni hili kundi la vijana wa miaka 30's na 20's.Nadhani kuna shida sana huko mashuleni kwa sababu hai ingii akilini msomi mzima kusema "plesident" badala ya president.
 
TATIZO LA KUTAMKA "R" NA "L"
Hili tatizo la shida ya kushindwa kutofautisha kati ya "R" na "L" ni tatizo jipya.

Nyakati zetu tunasoma shule ya msingi katika miaka ya 1950 tatizo hili halikuwapo

Walimu walikuwa makini kuanzia miaka ya awali katika kunyoosha matamshi ya wanafunzi yawe ya Kiswahili au Kiingereza.

Nashangaa leo kuwasikia watu waliofika hadi chuo kikuu hawajui tofauti ya "R" na "L".

Najiuliza inawezekanaje?
Hawa wamesomeshwa na walimu gani?

Najiuliza kuwa hata huko vyuoni walikuwa wakitamka, "Plesident," badala ya "President?"

Nilipokuwa sekondari niliingia katika mchuano wa English Elocution shule za Dar-es-Salaam.

Shule yetu St. Joseph's Convent miaka yote tukishinda nafasi ya kwanza na sababu ni kuwa shule yetu ilikuwa English Medium toka enzi na enzi.

Kiingereza kilikuwa ndiyo Kiswahili chetu.

Imefika siku ya mchuano kuchagua watakaokwenda kuwakilisha shule yetu.

Kwangu haikuwa shida wala tabu kuhifadhi ukurasa mzima wa William Shakespeare.

Mwalimu wangu wa Kiingereza Mrs. Grant kasimama mbele yangu kunisikiliza.

Darasa zima liko kimya.

Nimechagua hotuba ya Dr. Martin Luther King "I Have a Dream."

Nashuka bila tabu bila kujikwaa popote.

Hifdhi nilijifunza chuoni yaani madrasa na walimu wangu wa kwanza nawakumbuka Mwalimu Badi na Mwalimu Mussa walionihifadhisha majina ya Mtume kwenda nyuma.

Yote yalikuwa yamenasa.
Nilikuwa hata darasa la kwanza sijaanza.

Hiki kilikuwa Kiarabu na ilinisaidia sana baadae katika matamshi yangu katika lugha ya Kiingereza.

Ndiyo maana niliingia kwenye mchuano bila shida wala hofu.

Sikupita mpambano huu.
Nini sababu ya kushindwa kwangu?

Mrs. Grant mwalimu wetu wa Kiingereza hakunipasisha kwa kuwa mshindani mwenzangu alikuwa na "accent" nzuri akikizungumza Kiingereza kama Mwingereza mwenyewe.

Mrs. Grant alikuwa Mwingereza.

Haikuwa tatizo la "Glound" badala ya "Ground" lililonifanye nishindwe.

Ndiyo leo nashangaa kumsikia mtangazaji wa Radio na TV akitamka, "Blitish Bloadcasting Coplation."

Maini yananikatika nikisikia matamshi hayo.
Tunatokaje katika shida na dhiki hii?
Pole.
NECTA wanapotutangazia ufaulu wa mitihani mbalmbali, tusiwe tunafurahia. Muda mwingine ni ufaulu wa kisiasa, kwa wanafunzi waliosoma mitaala ya kimagumashi. Elimu imechakachuliwa. Ni wanafunzi hao ndio wanafika chuo kikuu.
 
Mzee nashukuru umeleta hii mada jukwaani.Shida kubwa ni elimu inayotolewa hivi sasa ukifatilia wanao shindwa tofauti ya R na L ni hili kundi la vijana wa miaka 30's na 20's.Nadhani kuna shida sana huko mashuleni kwa sababu hai ingii akilini msomi mzima kusema "plesident" badala ya president.
Na bashungwa, jee ana miaka 30 na yeye pia !!?
 
Kweli matumizi ya "R" na "L" ni tatizo katika matumizi ya lugha ya kiswahili Tanzania. Sijui nini kifanyike?
 
Na bashungwa, jee ana miaka 30 na yeye pia !!?
Huyo nadhani ni kutokana n kabila lake lakini ukitazama kwa muktadha wa tatizo kiujumla chanzo ni mashuleni,sasa hivi imekuwa kama ndio sahihi leo nimepita mahali nikaona tangazo tunauza kahawa,kashata na kalanga
 
Back
Top Bottom