Tatizo la macho kuwasha; msaada

Fideliiiz

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2016
Posts
632
Reaction score
407
Doctor nawashwa sana na macho naomba msaada wako.
 
Yana muda gani? Rangi ikoje ni mekundu? Ni moja au yote mawili? Unawashwa na mahala pengine au macho tu? Yanatoa machozi? Hebu ongeza nyama kweny ugonjwa wako tukusaidie.
 
ni macho tu yanawasha sana hasa usiku
 
Yana muda gani? Rangi ikoje ni mekundu? Ni moja au yote mawili? Unawashwa na mahala pengine au macho tu? Yanatoa machozi? Hebu ongeza nyama kweny ugonjwa wako tukusaidie.

Mkuu samahani, na mimi nina tatizo la macho kuwasha.
Ni muda mrefu nimekua nikiwashwa, macho ni mekundu na huwasha sana sana wakati wa usiku. Yanatoa machozi pia yanaambatana na mafua.
 
Mkuu samahani, na mimi nina tatizo la macho kuwasha.
Ni muda mrefu nimekua nikiwashwa, macho ni mekundu na huwasha sana sana wakati wa usiku. Yanatoa machozi pia yanaambatana na mafua.
Je umewahi tumia dawa gani ya macho tangu yaanze kuwasha?
 
Yana muda gani? Rangi ikoje ni mekundu? Ni moja au yote mawili? Unawashwa na mahala pengine au macho tu? Yanatoa machozi? Hebu ongeza nyama kweny ugonjwa wako tukusaidie.
Mkuu msaada pia na mimi..
Nitangulize pia samahani kwa kuvamia uzi wa watu..

Macho yananitesa sana yanawasha sana na ni tangu nizaliwe mpaka dakika hii.. nimezunguka hosptal kibao nikaambiwa ni allergy nikifika 18 yrs yataisha.. nikafikisha na kupitiliza baado naambiwa ni allergy. Nimebadilisha sabuni,chakula,manukato ila still yananiwasha sana mpaka yanakua mekundu sana..
Nimetumia dawa kibao tu za macho ila bado matokeo bila bila..
Sasa hivi natumia CHLORAMPHENICOL.. pale napozidiwa ndo hiyo kidoogooo inapunguza hyo adha ya kuwasha..
MSAADA tutani..
 
Wakubwa naomba mnisaidie" macho yangu sasa yana siku tatu yakiwa yanawasha, lakini yanaanza kuwasha kuanzia mishale ya jioni"
hivi tatizo linawezakuwa nini? maana najikuna saana ndani ya macho mpaka yanavimba.
 
Ni allergy,una zoezi la kuanza kufanya uchunguzi wa nini hasa ni kisababishi mf.body spray, mafuta ya kujipaka ,wanja kwa kina mama n.k.
Namna nyingine ni kuosha macho kwa maji ya baridi pindi unapokumbana na tatizo hilo.
Upande wa dawa tumia dawa ambazo kitaalamu wanaziita "mast cell stablizers" kama vile "sodium cromoglycate 2% eye drop".
Kwa Chloramphenico unayotumia sijui ni vidonge au ni ya matone ya kudondoshea machoni? Haina msaada sana kwa tatizo lako ,tumia dawa zinazosaidia shida ya mzio "allergy".
 
Nonsense unaambiwa taangu akiwa Mdogo wazazi wametafuta dawa wamekosa yeye pia Aliambiwa akifika miaka 18 atapona Sasa ana miaka iliyopitiliza

Je katika Mda wote huo hajagundua Kinachomdhuru? Na Alishabadilisha Mafuta na Manukato Na vyakula pia
 
Nonsense unaambiwa taangu akiwa Mdogo wazazi wametafuta dawa wamekosa yeye pia Aliambiwa akifika miaka 18 atapona Sasa ana miaka iliyopitiliza

Je katika Mda wote huo hajagundua Kinachomdhuru? Na Alishabadilisha Mafuta na Manukato Na vyakula pia
kaka haya ndo umeona unitapikie! asante,mshauri we sasa,au wakati akiwa mdogo body sprays hazikuwepo,au visababishi vingine? kama aliambiwa na wengine mlango wa wengine kumshauri unakuwa umefungwa?.Acha utoto,if you know things just go straight to what you you know sio kutukana watu, kama una elimu ya "immunology" nafikiri ungeenda deep wala sio mashudu unayoyatoa.
 
Nonsense unaambiwa taangu akiwa Mdogo wazazi wametafuta dawa wamekosa yeye pia Aliambiwa akifika miaka 18 atapona Sasa ana miaka iliyopitiliza

Je katika Mda wote huo hajagundua Kinachomdhuru? Na Alishabadilisha Mafuta na Manukato Na vyakula pia
ushauri wako niupi weye usiye nonsense.?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…