Tatizo la Moyo kujaa maji

Tatizo la Moyo kujaa maji

chwechinyong

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2011
Posts
223
Reaction score
105
Habari wataalamu wote humu ndani.

Mke wangu anasumbuliwa sana na tatizo tajwa hapo juu. Moyo wake umejaa maji ambayo kwa mara ya kwanza yalitolewa kwa mpira na yalikuwa mengi sana ila baada ya wiki yakaonekana kurudi ingawa si katika hali ile ya mwanzo, mara hii yakiwa ni kiasi kidogo ila si kile ambacho kinatakiwa kuwepo (kwa mujibu wa madaktari). Ameshazunguka sana na tatizo hili na mbaya zaidi madaktari hawajui chanzo cha hayo maji kujaa. Ameshatumia dawa aina mbalimbali za kukausha maji moyoni, pia za TB (walihisi huenda ikawa TB inamsumbua) yapata miaka mitatu sasa ila bado maji yanaonekana kuwepo ingawa wataalamu wanasema yanapungua kwa kiasi kidogo mnoo. Hali hii humsababishia sana maumivu mke wangu upande wake wa moyo. Tumeshaenda Regency and Muhimbili katika hangaika yetu.

Je, kuna yeyote ambae kwa namna moja au nyengine ameshawahi kukutana na mgonjwa wa namna hii na tiba yake ipoje?
Je, kuna yeyote anaefahamu hospitali yoyote (ukiachwa tajwa hapo juu) walioweza kushughulika na kuliponya taizo kama hili?

Msaada wenu ni muhimu sana kwetu.

Ahsanteni
 
Habari wataalamu wote humu ndani.

Mke wangu anasumbuliwa sana na tatizo tajwa hapo juu. Moyo wake umejaa maji ambayo kwa mara ya kwanza yalitolewa kwa mpira na yalikuwa mengi sana ila baada ya wiki yakaonekana kurudi ingawa si katika hali ile ya mwanzo, mara hii yakiwa ni kiasi kidogo ila si kile ambacho kinatakiwa kuwepo (kwa mujibu wa madaktari). Ameshazunguka sana na tatizo hili na mbaya zaidi madaktari hawajui chanzo cha hayo maji kujaa. Ameshatumia dawa aina mbalimbali za kukausha maji moyoni, pia za TB (walihisi huenda ikawa TB inamsumbua) yapata miaka mitatu sasa ila bado maji yanaonekana kuwepo ingawa wataalamu wanasema yanapungua kwa kiasi kidogo mnoo. Hali hii humsababishia sana maumivu mke wangu upande wake wa moyo. Tumeshaenda Regency and Muhimbili katika hangaika yetu.

Je, kuna yeyote ambae kwa namna moja au nyengine ameshawahi kukutana na mgonjwa wa namna hii na tiba yake ipoje?
Je, kuna yeyote anaefahamu hospitali yoyote (ukiachwa tajwa hapo juu) walioweza kushughulika na kuliponya taizo kama hili?

Msaada wenu ni muhimu sana kwetu.

Ahsanteni
+255713 928 117
 
+255713 928 117
Nipe maelezo kidogo mkuu..naona umeniachia namba tu..najua natakiwa kupiga ila ungeweka nyama kidogo. Je, wewe ni daktari? au unajua sehemu ambayo tunaweza pata tiba ya hilo tatizo? au ni mtaalamu wa tiba asilia?..Please maelezo kidogo. Thanks
 
Back
Top Bottom