Save NUNDU
New Member
- May 2, 2024
- 3
- 0
Tatizo la Traffic Police barabarani: wananchi tunacheleweshwa sana kwenye shughuli zetu tukiwa kwenye daladala kwa daladala hiyo moja kusimamishwa mara kadhaa na Traffic kwa trip hiyo hiyo moja. Kwanini zisitumike mbinu mbadala?
Viongozi wetu wanasafiri nchi za nje sana na wanaona nchi za wenzetu mfano Marekani huwezi kumuona Traffic Police barabarani, mimi niliishi Marekani na siku moja nilikuwa haraka nimechelewa kwenye appointment, nikiwa nimesimama kwenye traffic lights zikiwa nyekundu, niliangalia kushoto/kulia hakuna gari wala Police nikapita kwenye taa nyekundu!
Wiki mbili kabla, nilipokea barua kwenye mailbox ya nyumbani, kufungua ile barua nilikutana na picha ya gari langu likipita kwenye taa nyekundu tarehe ile ile niliopita pale na faini ya dola sabini imeandikwa humo na maelekezo ya kuilipa. Hizo ni mbinu za Serikali kufanya kwa kupunguza mapolisi barabarani.
Viongozi wetu wanasafiri nchi za nje sana na wanaona nchi za wenzetu mfano Marekani huwezi kumuona Traffic Police barabarani, mimi niliishi Marekani na siku moja nilikuwa haraka nimechelewa kwenye appointment, nikiwa nimesimama kwenye traffic lights zikiwa nyekundu, niliangalia kushoto/kulia hakuna gari wala Police nikapita kwenye taa nyekundu!
Wiki mbili kabla, nilipokea barua kwenye mailbox ya nyumbani, kufungua ile barua nilikutana na picha ya gari langu likipita kwenye taa nyekundu tarehe ile ile niliopita pale na faini ya dola sabini imeandikwa humo na maelekezo ya kuilipa. Hizo ni mbinu za Serikali kufanya kwa kupunguza mapolisi barabarani.
Upvote
0