Elisha Kigahe
Member
- Aug 16, 2022
- 5
- 4
Hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kukosa ajira. Makala hii, itaangazia changamoto zinazo wakabili vijana katika sekta ya ajira binafsi.
Kutokana na wingi wa vijana wanaohitimu vyuo vya kati na vyuo vikuu, suala la ajira limekuwa tatizo sugu hapa Tanzania.
Mifumo yetu ya elimu inawaandaa vijana kuajirika katika sekta za umma na sekta binafsi. Hivyo, kutokana na uwingi wa wahitimu wa vyuo, mahitaji ya soko yamezidiwa na Kasi ya wahitimu. Hii imepelekea suala la ajira rasmi kukumbwa na bumbuwazi.
Siku za hivi karibuni kumekuwa na msukumo mkubwa wa viongozi na wanazuoni mbalimbali wa kutaka vijana wajikite katika kujiajiri au ajira binafsi.
Ukweli ni kwamba ajira binafsi zinakumbwa na changamoto nyingi. Mazingira yake Bado hayaruhusu urahisi wa kufanikisha adhima hiyo.
Makala hii inaangazia baadhi ya changamoto ambazo serikali na wadau wengine wanapaswa kuzitazama kabla ya kushikia mabango suala la kujiajiri kwa vijana.
CHANGAMOTO ZA AJIRA BINAFSI KWA VIJANA.
1. MFUMO WA ELIMU
Hapa tunaangalia madhaifu yaliyopo katika mfumo wetu wa elimu. Mfumo wa elimu yetu ni ule ambao umerithishwa kutoka kwa wakoloni. Ikumbukwe kuwa lengo kuu la elimu ya mkoloni ilikuwa kuwaandaa watu watakao tumika kwenye makampuni yao. Wakoloni walitoa elimu kwa baadhi yao ili waweze kuajiriwa Kama vibaraka wao. Mfano makalani wa mashamba ya chai enzi za mkoloni. Kwa mfumo huu ni ngumu kumuandaa kijana kujiajiri.
Kuna udhaifu mwingi katika mfumo wetu wa elimu, kiasi kwamba inakosa tija kwa vijana wetu.
MADHAIFU YA MFUMO WA ELIMU YETU
A. Kijana anatumia muda mrefu sana kutimiza malengo yake ya kielimu. Inamchukua muda wa zaidi ya 16 kutafuta elimu. Hii inawafanya vijana kukosa muda wa kujitanua kulingana na mahitaji ya kimazingira. Muda wote huu anakuwa ametingwa na masomo sambamba na mitihani.
B. Elimu yetu ina mawanda mapana ya taarifa ambazo mwanafunzi anatakiwa kuyabeba. Hii inapelekea vijana kukosa umahili wa eneo moja. Kwa mujibu wa wanafalsafa mbalimbali, ni ngumu Sana kuwa mahili kwenye kitu zaidi ya kimoja. Mfano, kijana wa kidato Cha nne anabeba masomo zaidi ya 9 ambayo yamejiegemeza katika sanaa, sayansi na biashara. Hii inamnyima mwanafunzi uwezo wa kuwa mahiri.
C. Elimu yetu ni dhahania kuliko vitendo. Taarifa nyingi zinazobebwa katika masomo yetu ni dhana za kuvikilika. Hivyo, inakuwa ngumu kwa kijana kutumia elimu yake kujiajiri kulingana na mazingira yetu.
D. Elimu yetu haiendani na uhalisia wa mazingira yetu na wakati wetu. Kuna baadhi ya mafunzo hayaendani kabisa na mazingira yetu ya Sasa. Hii inafanga vijana kushindwa kutumia elimu Yao katika kupambana na maisha.
Kwa ujumla, mfumo wa elimu yetu haimuwezeshi kijana kujiajiri. Tunahitaji maboresho makubwa katika mitaala ya elimu ili kukidhi haja ya mazingira ya Sasa.
Maboresho tunayoweza kufanya kwenye mfumo wetu wa elimu ni pamoja na muda wa kuanza na kumaliza shule upunguzwe, mawanda ya masomo yapunguzwe. Mwanafunzi aanza kuchagua taasusi au mkondo kuanzia shule ya msingi Hadi elimu ya juu. Hii itasaidia kuongeza tija katika sekta ya ajira binafsi.
2. KUKOSEKANA KWA MTAJI
Sababu nyingine inayoongeza ugumu kwa vijana wengi kujiajiri ni kukosekana kwa mitaji.
Ili uweze kuanzisha au kuendesha biashara yeyote unahitaji mtaji. Vijana wengi wanatokea katika familia duni kiuchumi. Hivyo wanashindwa kupata msaada kutoka wa wajumbe wa familia zao.
Licha ya jitihada za serikali kujaribu kutatua tatizo hili kwa kutenga 10% ya mapato yote ya halmashauri kwa mwaka, Bado uhitaji ni mkubwa kuliko kilichopo. Bado serikali haiwezi kuwafikia vijana wote wenye nia ya kujiajiri.
Zipo baadhi ya taasisi za fedha zinazotoa fedha ambazo zinaweza kutumika Kama mtaji. Masharti yake yamekuwa magumu kufikiwa na vijana wengi. Mfano, wanahitaji uje na dhamana ya mali isiyo hamishika Kama nyumba. Inakuwa ngumu kwa vijana wengi kukidhi kigezo hiki.
Pamoja na jitihada mbalimbali zinazofanywa na wadau mbalimbali Bado suala la mtaji limekuwa changamoto kubwa.
3. KUKOSEKANA KWA UBUNIFU MIONGONI MWA VIJANA
Vijana wengi wanashindwa kubuni au kuibua biashara mpya zitakazo tatua matatizo katika jamii. Hii inawafanya wafanye biashara kwa historia za watu wengine.
Wanapenda kuiga biashara za watu kwa kusikia faida zake. Hii inapelekea kushindwa kumudu changamoto za biashara hiyo.
4. UTITILI WA KODI NA TOZO
Kumekuwa na Kodi, ushuru na tozo nyingi ambazo zinapunguza tija katika biashara za vijana. Ni wajibu wa Kila Mtanzania kulipa Kodi kwa maendeleo ya taifa letu. Lakini, zikizidi inapelekea kuanguka kwa biashara nyingi. Mfano, unasafilisha mazao ya misitu unatakiwa kulipa (kibali cha ofisi ya misitu, ushuru wa halmashauri, ushuru wa usafilishaji, Kodi ya serikali 5%) Hii inapelekea biashara nyingi kushindwa kujiendesha.
5. UVIVU NA TABIA YA KUTOPENDA KAZI
Baadhi ya vijana ni wavivu, hawapendi kufanya Kazi. Wanakesha kwenye mitandao ya kijamii. Vijana wengi hawajitambui
HITIMISHO
Kwa kuhitimisha, sekta ya ajira binafsi ndio sehemu pekee ambayo itakwamua taifa kutoka katika janga la vijana wengi kukosa ajira.
Inapaswa kutengenezewa mazingira wezeshi Kama vile mitaji ya Hali na mali, mikopo rahisi, elimu ya biashara, sera zinazotabilika na kadharika.
Asante kwa muda wako ulioutoa kwaajili ya kuisoma makala hii.
IMEANDALIWA NA:
ELISHA KIGAHE
0757366084
Kutokana na wingi wa vijana wanaohitimu vyuo vya kati na vyuo vikuu, suala la ajira limekuwa tatizo sugu hapa Tanzania.
Mifumo yetu ya elimu inawaandaa vijana kuajirika katika sekta za umma na sekta binafsi. Hivyo, kutokana na uwingi wa wahitimu wa vyuo, mahitaji ya soko yamezidiwa na Kasi ya wahitimu. Hii imepelekea suala la ajira rasmi kukumbwa na bumbuwazi.
Siku za hivi karibuni kumekuwa na msukumo mkubwa wa viongozi na wanazuoni mbalimbali wa kutaka vijana wajikite katika kujiajiri au ajira binafsi.
Ukweli ni kwamba ajira binafsi zinakumbwa na changamoto nyingi. Mazingira yake Bado hayaruhusu urahisi wa kufanikisha adhima hiyo.
Makala hii inaangazia baadhi ya changamoto ambazo serikali na wadau wengine wanapaswa kuzitazama kabla ya kushikia mabango suala la kujiajiri kwa vijana.
CHANGAMOTO ZA AJIRA BINAFSI KWA VIJANA.
1. MFUMO WA ELIMU
Hapa tunaangalia madhaifu yaliyopo katika mfumo wetu wa elimu. Mfumo wa elimu yetu ni ule ambao umerithishwa kutoka kwa wakoloni. Ikumbukwe kuwa lengo kuu la elimu ya mkoloni ilikuwa kuwaandaa watu watakao tumika kwenye makampuni yao. Wakoloni walitoa elimu kwa baadhi yao ili waweze kuajiriwa Kama vibaraka wao. Mfano makalani wa mashamba ya chai enzi za mkoloni. Kwa mfumo huu ni ngumu kumuandaa kijana kujiajiri.
Kuna udhaifu mwingi katika mfumo wetu wa elimu, kiasi kwamba inakosa tija kwa vijana wetu.
MADHAIFU YA MFUMO WA ELIMU YETU
A. Kijana anatumia muda mrefu sana kutimiza malengo yake ya kielimu. Inamchukua muda wa zaidi ya 16 kutafuta elimu. Hii inawafanya vijana kukosa muda wa kujitanua kulingana na mahitaji ya kimazingira. Muda wote huu anakuwa ametingwa na masomo sambamba na mitihani.
B. Elimu yetu ina mawanda mapana ya taarifa ambazo mwanafunzi anatakiwa kuyabeba. Hii inapelekea vijana kukosa umahili wa eneo moja. Kwa mujibu wa wanafalsafa mbalimbali, ni ngumu Sana kuwa mahili kwenye kitu zaidi ya kimoja. Mfano, kijana wa kidato Cha nne anabeba masomo zaidi ya 9 ambayo yamejiegemeza katika sanaa, sayansi na biashara. Hii inamnyima mwanafunzi uwezo wa kuwa mahiri.
C. Elimu yetu ni dhahania kuliko vitendo. Taarifa nyingi zinazobebwa katika masomo yetu ni dhana za kuvikilika. Hivyo, inakuwa ngumu kwa kijana kutumia elimu yake kujiajiri kulingana na mazingira yetu.
D. Elimu yetu haiendani na uhalisia wa mazingira yetu na wakati wetu. Kuna baadhi ya mafunzo hayaendani kabisa na mazingira yetu ya Sasa. Hii inafanga vijana kushindwa kutumia elimu Yao katika kupambana na maisha.
Kwa ujumla, mfumo wa elimu yetu haimuwezeshi kijana kujiajiri. Tunahitaji maboresho makubwa katika mitaala ya elimu ili kukidhi haja ya mazingira ya Sasa.
Maboresho tunayoweza kufanya kwenye mfumo wetu wa elimu ni pamoja na muda wa kuanza na kumaliza shule upunguzwe, mawanda ya masomo yapunguzwe. Mwanafunzi aanza kuchagua taasusi au mkondo kuanzia shule ya msingi Hadi elimu ya juu. Hii itasaidia kuongeza tija katika sekta ya ajira binafsi.
2. KUKOSEKANA KWA MTAJI
Sababu nyingine inayoongeza ugumu kwa vijana wengi kujiajiri ni kukosekana kwa mitaji.
Ili uweze kuanzisha au kuendesha biashara yeyote unahitaji mtaji. Vijana wengi wanatokea katika familia duni kiuchumi. Hivyo wanashindwa kupata msaada kutoka wa wajumbe wa familia zao.
Licha ya jitihada za serikali kujaribu kutatua tatizo hili kwa kutenga 10% ya mapato yote ya halmashauri kwa mwaka, Bado uhitaji ni mkubwa kuliko kilichopo. Bado serikali haiwezi kuwafikia vijana wote wenye nia ya kujiajiri.
Zipo baadhi ya taasisi za fedha zinazotoa fedha ambazo zinaweza kutumika Kama mtaji. Masharti yake yamekuwa magumu kufikiwa na vijana wengi. Mfano, wanahitaji uje na dhamana ya mali isiyo hamishika Kama nyumba. Inakuwa ngumu kwa vijana wengi kukidhi kigezo hiki.
Pamoja na jitihada mbalimbali zinazofanywa na wadau mbalimbali Bado suala la mtaji limekuwa changamoto kubwa.
3. KUKOSEKANA KWA UBUNIFU MIONGONI MWA VIJANA
Vijana wengi wanashindwa kubuni au kuibua biashara mpya zitakazo tatua matatizo katika jamii. Hii inawafanya wafanye biashara kwa historia za watu wengine.
Wanapenda kuiga biashara za watu kwa kusikia faida zake. Hii inapelekea kushindwa kumudu changamoto za biashara hiyo.
4. UTITILI WA KODI NA TOZO
Kumekuwa na Kodi, ushuru na tozo nyingi ambazo zinapunguza tija katika biashara za vijana. Ni wajibu wa Kila Mtanzania kulipa Kodi kwa maendeleo ya taifa letu. Lakini, zikizidi inapelekea kuanguka kwa biashara nyingi. Mfano, unasafilisha mazao ya misitu unatakiwa kulipa (kibali cha ofisi ya misitu, ushuru wa halmashauri, ushuru wa usafilishaji, Kodi ya serikali 5%) Hii inapelekea biashara nyingi kushindwa kujiendesha.
5. UVIVU NA TABIA YA KUTOPENDA KAZI
Baadhi ya vijana ni wavivu, hawapendi kufanya Kazi. Wanakesha kwenye mitandao ya kijamii. Vijana wengi hawajitambui
HITIMISHO
Kwa kuhitimisha, sekta ya ajira binafsi ndio sehemu pekee ambayo itakwamua taifa kutoka katika janga la vijana wengi kukosa ajira.
Inapaswa kutengenezewa mazingira wezeshi Kama vile mitaji ya Hali na mali, mikopo rahisi, elimu ya biashara, sera zinazotabilika na kadharika.
Asante kwa muda wako ulioutoa kwaajili ya kuisoma makala hii.
IMEANDALIWA NA:
ELISHA KIGAHE
0757366084
Upvote
7