Tatizo na Nyumba Ndogo...


Kwanza hongera kwa kuwa post ya 400 and with this I rest my case kwa heshima ya Babu.
 
Nilikua sijagundua raha ya hii topic ni kusoma michango sio kuchangia....lol
 
Reactions: Mbu
Mbu naona hatimaye somo limeelewea...ama ndo ulikuwa unajifanya huelewi....hahaha MJ1 mjanja mjanja huyu kasema Bigirita!
 

MJ1,

Naomba niseme hili ingawa nilishajua tumemaliza hiki kibarua..

Hakuna love kwenye cheating & nyumba ndogo...Kuna usanii na kuchezeana kwa aina nyingi nyingi!!

Sijawahi kusikia mtu ambaye amependa (real love) nje halafu akabaki na ndoa.....

Nasubiri kusahihishwa kama nimezeeka vibaya

kwa maisha ya siku hizi ambapo kila mtu anatafuta opportunities popote zinakopatikana (shule, short-term kazi, etc) kila siku tutakuwa barabarani.............. leo baba anamfwata mama china, kesho mama anamfwata baba Sweden........ kaazi kweli

Huu mjadala umekuvua gamba kabisa..Kama kuna mtu hakuwa kumfahamu FP, basi aanzie kwenye post yako ya kwanza kwenye hii thread!!

Nimekukubali kwa nondo zako...Ubarikiwe sana!!

Mapenzi yanasumbua wengi sana humu.

Kwani wewe una immunity ya kudumu kwenye haya mambo??
 
Reactions: Mbu
Eh Babu DC, unawezanifafanulia kwa nini unampa RR mandatory ya kuifunga hii thread?? ameifungua yeye? je mimi kama mimi nimeridhika? mbona hunitendei haki Babu DC??

Nisamehe mdogo wangu,

Hii michango inazingua na bila kuwa mwangalifu, mtu unaweza kujikuta unaogelea tu bila kujielewa..

Lilikuwa ombi tu kwa super mod wetu...Ila naona hii thread ndo bado inaanza!!

Bado unahitaji maelezo ili utofautishe nyumba ndogo na huduma ya chap chap??

Babu DC!!
 
ukiweza kufanya hivyo

nitaomba uandike pepa
maana utastahili dk ya uvumbuzi

hakuna kitu utamfanyia mwanamme
afikirie kutulia tu
they are explorers

labda sijaeleweka, inawezekana. Kutulia au kutotulia ni swala la mtu kuamua ila mimi sitojenga mazingira ya yeye kutotulia. Wapo wanaume watulivu ila wanawake wanawatibua hadi wanaanza kufikiria vismall houses.
 
Yaalaiti,napenda pasi kifaniii(nyumba ndogo). Tafauuti,sikutilii moyonii,sikuwachi leo na kesho peponii,aaaa,a a a aa aaaa!
 
Tangawizi,

Ndo maana immediately unahitaji kuwa na nyumba ndogo maana kubwa imekuwa 'kubwa' kweli inakushinda kumanage... usivae kiatu kinakubana muda wote hadi miguu itoke malenge lenge...tafutapo na makubaz ya saizi yako....

dah.....kweli ushauri!!
 
Kua uyaone mtoto wa kike...ingelikuwa kama mambo mengine yana breki kama za gari, ungezikamata kabla mambo hayajaharibika. Ila hata ndege wajanja wananasa na tundu bovu, lol!

nikue mara ngapi?
 

Hehe he he umeamua kunisema hadharani he msome AshaDii hapo chini kwenye red huo ndo msimamo wangu....Mwajuma



Umenisoma Mwajuma???:A S-coffee:

dah! Dena naona na wewe umeamua kunibatiza hilo jina. Nilipoona tu post ya ID nikajua lazma msimamo wako ni huo kabla hata hujasema.
 

dah! Hivi kweli wanawake wote humu ndani mnaamini kwamba hakuna mwanaume anayeweza ishi bila nyumba ndogo?
Na wanaume wote humu ina maana mna nyumba ndogo.
 
dah! Hivi kweli wanawake wote humu ndani mnaamini kwamba hakuna mwanaume anayeweza ishi bila nyumba ndogo?
Na wanaume wote humu ina maana mna nyumba ndogo.


Hapana Hus,

Ila nadhani wengi wanakubali (hata kama hawaamini na hawataki kabisa) kwamba wanaume wengi wanatoka nje ya ndoa (kwa mtindo wa chap chap au nyumba ndogo)....hapa natumia definition ya Big!!

Na siyo wanaume wote wana nyumba ndogo (mie naweza kukuapia hata kwa mtutu wa bunduki kwamba sina na kuna wenzangu kibao) na pia wapo baadhi ambao hawajawahi kukamatwa kwenye mtego wa shetani (wapo au tupo)!!!!

Hata hivyo, wakati wanawake wengi wanapambana kuwazuia waume zao wasicheat au kuwa na nyumba ndogo (which is beyond cheating), wanaume wengi wanapambana kumshinda shetani wasikamatwe na mtego wa kuingia kwenye mambo ya small house au kupata huduma ya chap chap!!

Babu DC!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…