Tatizo na Nyumba Ndogo...

ukiona hivyo ujue nyumba ndogo ya mumeo inajua kula na kipofu....
Inajua mipaka yake ni ipi....
 
Asipokwambia you live in the ILLUSION of happiness. Bora akwambie ili uweze kuchukua necessary measures to live in REAL happiness again.
 
Yaani kweli hamshtushwi wala kuogopa waume zenu wakiwa na nyumba ndogo?

Hamuogopi magonjwa ya zinaa? Hamuogopi ukimwi nyie?

Mna uhakika gani huko kwa nyumba ndogo kama hao waume zenu wanangonoka kwa kutumia kinga? Siku wakiwaletea magonjwa bado mtakuwa na hiyo 'attitude' ya kutojali?

Mwanamke ambaye hajali kama mumewe ana nyumba ndogo au la basi naye hajijali. Kama unajijali basi lazima utakwazika na huyo mumeo kuwa na kimada au vimada pembeni.

Na kwa vile hao wa pembeni ni vimada basi na wao mara nyingi hawajifungi kwa waume zenu tu. Wanakuwa na sexual partners wengine zaidi ya hao waume zenu.

Na chances are ukimpa mumeo 'non-verbal' rukhsa ya kuwa na vimada (on condition kwamba ili mradi hao vimada hawakusumbui kwa kukutumia sms za kejeli na mambo mengine kama hayo) basi upo wakati atachovya bila kinga.

Sasa akitaka kulalana na wewe mke wake halali utamlazimisha atumie kinga au utamwambia ni juu yake kama anataka kutumia au kutotumia?

Mimi siwaelewi kabisa nyie wanawake mnaosema eti hamna tatizo na nyumba ndogo za hao waume zenu! Au na nyinyi mna nyumba ndogo zenu?
 
Asipokwambia you live in the ILLUSION of happiness. Bora akwambie ili uweze kuchukua necessary measures to live in REAL happiness again.
unafikiri unaweza kuwa happy ukijua kuwa mumeo ana nyumba ndogo? mbaya zaidi mwenyewe akikiri kuwa anayo? labda akuambie akiwa ameshaachana nayo
 
unafikiri unaweza kuwa happy ukijua kuwa mumeo ana nyumba ndogo? mbaya zaidi mwenyewe akikiri kuwa anayo? labda akuambie akiwa ameshaachana nayo

So you would rather bury your head in the sand and live a lie?
 
Yaani kweli hamshtushwi wala kuogopa waume zenu wakiwa na nyumba ndogo?

Hamuogopi magonjwa ya zinaa? Hamuogopi ukimwi nyie?
siyo kama hatushtushwi wao kuwa na nyumba ndogo, hapa maana yake ni kwamba hatuwawazii waume kuwa wana nyumba ndogo pindi mambo yanapokuwa magumu nyumbani. hapa kuna mambo 2 tofauti
1. unajua kuwa ana nyumba ndogo lakini hujali..... siyo tunalozingumzia hapa
2. hujui kama ana nyumba ndogo ila unamuhisi tu sababu mapenzi kwako yamepungua au kuna maugomvi ya mara kwa mara................. hili ndo tunalolizungumzia
 
unafikiri unaweza kuwa happy ukijua kuwa mumeo ana nyumba ndogo? mbaya zaidi mwenyewe akikiri kuwa anayo? labda akuambie akiwa ameshaachana nayo
Utakua very unhappy at first, but after analysing the situation and the possible ways out utachukua hatua na utakua really happy, based on reality. Ukikataa kujua ukweli you are perpetuating the lie, you are guilty pia kwa sababu unaruhusu situation kuendelea.
Ukisha jua unachukua hatua. Kila mwanamke ana namna yake ya kuchukulia haya mambo, wengine wanasema wanapanga DOs and DON'Ts za kuwaongoza katika hiyo triangle, wengine pia wanasema wanaachana na huyo mume and move forward. in both cases, the lies stop, and life goes on.
 


Mwanzisha mada kasema hapati "shida wala kushtushwa na suala zima la nyumba ndogo"

Maybe she needs to qualify her statement.
 
So you would rather bury your head in the sand and live a lie?
la maana ni kwamba nisijue. sijasema kwamba nikijua nitakaa kimya na kumwacha aendelee na anayoyafanya. na kama sijui, sitachimbachimba kutafuta ninachodhani kuwa ni ukweli
 
ukishaachana na huyo mume unafanyaje? unaachana na mpango mzima unaohusu wanaume au unakuwa na mwanaume mwingine? naye ukimgundua?......................
Huwezi kuwa guilty kuruhusu hali kuendelea kama huna wazo kuwa kuna lolote linaendelea, nimesema mwanzo kuwa, kama nitajua kwa uhakika kabisa kuwa kuna linaloendelea nitachukua hatua, lakini kama sijui then siwezi kupekuwa kutafuta kujua kitu ambacho huwenda hakipo
 
Mwanzisha mada kasema hapati "shida wala kushtushwa na suala zima la nyumba ndogo"

Maybe she needs to qualify her statement.
mimi nilichomuelewa (na pamoja na kusoma post zake nyingine) ni kwamba, siyo kama hatishiki hata akijua kuwa mumewe ana nyumba ndogo anaacha tu aendelee, that means, hajali kabisa, anajua ataenda then atarudi, bali akiona mumewe kabadilika hawezi kuwaza kwamba kilichomfanya abadilike ni nyumba ndogo, labda kuna sababu nyingine.
labda kama mimi sijamwelewa vizuri
 
la maana ni kwamba nisijue.

Kwa nini la maana iwe ni kutokujua? Na kwa nini kujua kusiwe kwa maana?

sijasema kwamba nikijua nitakaa kimya na kumwacha aendelee na anayoyafanya. na kama sijui, sitachimbachimba kutafuta ninachodhani kuwa ni ukweli

Na ukishajua utafanya nini?
 
ukiona hivyo?
Jua mmeo mmeo na nyumba ndogo wote ni vilaza.

Yaani kupata tu ule uthubutu wa kutuma meseji ni tatizo, achia mbali alichoandika.

rafiki, na zipo nyumba ndogo ambazo zinakutumia sms kukuambia mimi ndo nyumba ndogo ya mumeo
 
Kwa nini la maana iwe ni kutokujua? Na kwa nini kujua kusiwe kwa maana?



Na ukishajua utafanya nini?
Mpaka nijue ndo nitajua cha kufanya.......... kwa sasa sitaki kabisa kuwaza nikijua nitafanya nini na wakati hicho kitu cha kujua labda hakipo
 
ukiona hivyo?
Jua mmeo mmeo na nyumba ndogo wote ni vilaza.

Yaani kupata tu ule uthubutu wa kutuma meseji ni tatizo, achia mbali alichoandika.
ni kweli, lakini kuna vilaza wengi sana, maana nimesikia hizi kesi nyingi sana. cha kushangaza huyo mdada sijui anapata namba ya mkeo wapi na saa ngapi
 
Kwa nini la maana iwe ni kutokujua? Na kwa nini kujua kusiwe kwa maana?

Na ukishajua utafanya nini?

Mpaka nijue ndo nitajua cha kufanya.......... kwa sasa sitaki kabisa kuwaza nikijua nitafanya nini na wakati hicho kitu cha kujua labda hakipo

Niliuliza maswali matatu. Umejibu moja tu, la mwisho. Vipi hayo mengine mawili.
 

Duuuu,

RR, sikujua kwamba huwafahamu wanaume kiasi hicho????

Babu DC!!
 
sijui umewahi kusoma a thread humu nilianzisha kuhusu nyumba ndogo?
ina mafunzo yote ya kuzuia hiyo...
Rafiki, nitumie link tafadhali...
hii on-off sometimes tunakosa mengi............ hii haijawahi kunikuta lakini, ila nimesikia kesi za hivyo nyingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…