sembo
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 4,350
- 3,451
'Tawi la Yanga lazidi kupukutika'.. ndivyo waweza kusema juu ya Singida United ambao ni 'tawi' la Yanga. Hii inakuja baada ya beki wao kisiki, Mganda Shafiq Batambuze kusaini rasmi mkataba wa kuitumikia Gor Mahia hapo jana.
Zoezi hili limekuja baada ya beki huyo kugoma kurejea nchini tangu msimu wa TPL wa 2018/19 ulipoanza kwa kile kinachodaiwa kuwa ni suala la kutolipwa mshahara na kumaliziwa fedha za usajili.
Majanga mengine yanayowakumba Singida United ni;
1. Makocha wake wasaidizi Athuman Mfaume na Jumanne Chale waliachia ngazi kwa sababu ya kutokulipwa mishahara ya miaka kadhaa.
2. Golikipa wao tegemeo, Manyika Peter naye kajiengua katika timu kwa kutolipwa stahiki zake.
Habari bila picha hainogi.. Wale 'matomaso' wenzangu mzigo huo hapo.
Zoezi hili limekuja baada ya beki huyo kugoma kurejea nchini tangu msimu wa TPL wa 2018/19 ulipoanza kwa kile kinachodaiwa kuwa ni suala la kutolipwa mshahara na kumaliziwa fedha za usajili.
Majanga mengine yanayowakumba Singida United ni;
1. Makocha wake wasaidizi Athuman Mfaume na Jumanne Chale waliachia ngazi kwa sababu ya kutokulipwa mishahara ya miaka kadhaa.
2. Golikipa wao tegemeo, Manyika Peter naye kajiengua katika timu kwa kutolipwa stahiki zake.
Habari bila picha hainogi.. Wale 'matomaso' wenzangu mzigo huo hapo.