Tazama wizi huu kwa wananchi vijijini kutoka kampuni za simu

Tazama wizi huu kwa wananchi vijijini kutoka kampuni za simu

Bozi

Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
92
Reaction score
144
Makampuni ya simu huwa na kawaida ya kukodi ardhi kujenga minara kutokana na survey zao. Upangaji huu ungekuwa fursa nzuri kuongeza kipato kwa baadhi ya wazee maskini ambao ardhi yao imeonekana inafaa kuweka mnara wa simu. Mara anatokea mtu ooh natafuta eneo hili niweke mashine, hivyo niuzie eneo hili. bila kujua kitu gani nkiko nyuma wazee hawa huuza kipande cha ardhi kwa wajanjanja hawa. wiki mbili tatu unaona mnara huo unajengwa. wazee hawa maskini wamedanganywa.

Hawa watu ambao hununua ardhi muda mfupi kabla ya mnara kujengwa hupewa taarifa hizi na nani?

Je, inawezekana ni makampuni yenyewe huwa yanapanga hii hujuma

Jamani huu si wizi ambao unapaswa kupingwa.

Mfano mzuri ni mnara uliojengwa Mwandama, Kata ya Sapiwi Bariadi. huyo mzee anamaisha magumu mno, nilipomuuliza alimuuzia nani, hata hajui anasema walikuja kutoka mjini wakanunua , wiki moja baadae mnara ukaanza kujengwa.

KWA MTAZAMO WANGU HUU NI WIZI WA KUPINGWA KKWA NGUVU ZOTE.
 
Mkuu hapo kuna kosa gani?,mtu mtafutaji lazima achangamkie fursa.Mzee aliuza kwa ridhaa yake kwa hela aliyohijaji akapewa,sasa eneo hilo siyo lake na uzalishaji unao endelea yeye anauangalia tu.Hata unapoenda kununua shamba/kiwanja baada ya muda unajenga ghorofa,sasa kwasababu mtu aliyekuuzia bado anaishi kwenye nyumba za nyasi anashuhudia tu.Hakuna kosa hapo.
 
hpoa tatizo shule usiilaum kampun ya sim mlaumu dalali hyu ndye aliyrfanya wizi
 
Hapo hamna wizi wowote si amemuzia kwa hiari yake bila kulazimishwa na mtu yeyote na akiwa na akili timamu sasa hapo atakua amevunja sheria gani mpaka umwite mwizi
 
Back
Top Bottom