Elitwege
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 5,294
- 10,970
Baada ya kuwazidi nguvu na kanisa lake kufurika watu, wahubiri wenzake wa Nigeria walimchukia TB Joshua bila sababu ya msingi.
Licha ya kutompenda lakini alizidi kuwa moto wa kuotea mbali duniani kote, kama ilivyokuwa kwa Magufuli hapa Tanzania baada ya wanafiki Chadema kujitokeza kutompenda hata kama wanapita kwenye flyover na ndege alizonunua yeye.
Pia soma > Temitope Balogun Joshua, (TB Joshua) afariki Dunia
-----
Imeelezwa kuwa TB Joshua aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 57 alikuwa miongoni mwa wahubiri wakubwa nchini Nigeria ambaye hakukubaliwa na wenzake licha ya kuwa na wafuasi wengi barani Afrika.
Alitengwa na Chama cha Wakristo wa Nigeria (CAN) na Wapentekoste wa Nigeria (PFN) huku sababu mbalimbali zikitajwa licha ya kuwa hakuwa tofauti na wahubiri wengine waliokuwa wakihubiri katika televisheni na kuwateka raia wa Nigeria tangu mwanzoni mwa miaka ya 90.
“Joshua ambaye alikuwa kiongozi wa kanisa la Synagogue Church Of All Nations (SCOAN) hakuwa mmoja wao. Alikuwa mkali. Hakuogopa lolote. Njia zake hazikuwa za kawaida," amesema Abimbola Adelakun, profesa msaidizi katika idara ya mafunzo katika Chuo Kikuu chaTexas.
Joshua alianza mahubiri kwenye televisheni miaka ya 90 na wafuasi wake walimuona kama mtu wa kuaminiwa na mnyenyekevu na ujumbe wake ulienea duniani kote.
"Hawaamini kwamba unaweza kujisimamia mwenyewe bila kuwa na mtu wa kumtegemea," amesema Gbenga Osinaike, mchapishaji wa taasisi kuu ya uchapishaji wa vitabu ya Kanisa la Kipentekoste nchini Nigeria.
TB Joshua aliyezaliwa Juni 12, 1963 anatajwa kama mhubiri ambaye hakutumia nguvu katika shughuli zake za kiroho lakini maombi yake yalionekana kuwa na nguvu.
"Watu walikuwa na fikra akilini ya jinsi ambavyo Mungu angefanya kazi na walipoona kitu tofauti kutoka kwake wakaamini zilikuwa ni nguvu hizo.”
“Walitumia 'muujiza' sawa wa leso, waliuza mafuta sawa ya 'upako' na maji matakatifu ambayo waliamini kuwa yaliponya magonjwa yote na picha zao zilichorwa kwenye fulana na vijikaratasi vilivyotumiwa na wafuasi wao. Lakini kwa sababu hakuwa katika kundi au katika tafsiri yao ya vile wanavyomuona Mungu, alitengwa na kusemwa vibaya ," amesema Osinaike.
Amesema TB Joshua alishutumiwa na wachungaji wenzake kwa kubuni miujiza bandia, na kudai kuwa mchungaji huyo aliwajibu kuwa miujiza hiyo ilikuwa ya kweli akisisitiza kuwa alichokuwa akifanya TB Joshua pia kilikuwa kinafanywa na wachungaji wengine ambao hawakupingwa na watu waliowaamini.
Mwaka 2004, mamlaka ya usimamizi wa matangazo nchini Nigeria ilipiga marufuku vituo vya televisheni kupeperusha matangazo ya miujiza ya wachungaji moja kwa moja kwenye televisheni.
Iliaminiwa kuwa Joshua ndiye anayelengwa, kwamba wachungaji hasimu walikula njama ili Serikali iweke marufuku hiyo kwa sababu alikuwa ametawala vyombo vya habari.
"Huenda alikuwa ndiye mchungaji wa kwanza kutumia matangazo kupitia intaneti kunadi mahubiri yake kwa watazamaji kimataifa ," amesema Adelakun.
Amesema kuwa tofauti na wachungaji wengine, TB Joshua
hakuanzisha matawi ya kanisa lake katika kila kona ya mtaa na mara nyingi familia yake haikuhusishwa na kazi yake, mke wake alionekana mara chache karibu naye na hakuna mtoto wake hata mmoja aliyefahamika kuongoza kanisa lake.
Kwa sasa kanisa lake limefungwa huku wanajeshi wakiimarisha ulinzi kutokana na mamia ya waumini kujaa wakilia na kuomboleza.
"Ilikuwa ni kazi na maisha ya mtu mmoja, ingawa alikuwa na mitume wake. Ni vigumu kuona kanisa likiendelea bila yeye," amesema Osinaike.
Chanzo: Mwananchi
Licha ya kutompenda lakini alizidi kuwa moto wa kuotea mbali duniani kote, kama ilivyokuwa kwa Magufuli hapa Tanzania baada ya wanafiki Chadema kujitokeza kutompenda hata kama wanapita kwenye flyover na ndege alizonunua yeye.
Pia soma > Temitope Balogun Joshua, (TB Joshua) afariki Dunia
-----
Imeelezwa kuwa TB Joshua aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 57 alikuwa miongoni mwa wahubiri wakubwa nchini Nigeria ambaye hakukubaliwa na wenzake licha ya kuwa na wafuasi wengi barani Afrika.
Alitengwa na Chama cha Wakristo wa Nigeria (CAN) na Wapentekoste wa Nigeria (PFN) huku sababu mbalimbali zikitajwa licha ya kuwa hakuwa tofauti na wahubiri wengine waliokuwa wakihubiri katika televisheni na kuwateka raia wa Nigeria tangu mwanzoni mwa miaka ya 90.
“Joshua ambaye alikuwa kiongozi wa kanisa la Synagogue Church Of All Nations (SCOAN) hakuwa mmoja wao. Alikuwa mkali. Hakuogopa lolote. Njia zake hazikuwa za kawaida," amesema Abimbola Adelakun, profesa msaidizi katika idara ya mafunzo katika Chuo Kikuu chaTexas.
Joshua alianza mahubiri kwenye televisheni miaka ya 90 na wafuasi wake walimuona kama mtu wa kuaminiwa na mnyenyekevu na ujumbe wake ulienea duniani kote.
"Hawaamini kwamba unaweza kujisimamia mwenyewe bila kuwa na mtu wa kumtegemea," amesema Gbenga Osinaike, mchapishaji wa taasisi kuu ya uchapishaji wa vitabu ya Kanisa la Kipentekoste nchini Nigeria.
TB Joshua aliyezaliwa Juni 12, 1963 anatajwa kama mhubiri ambaye hakutumia nguvu katika shughuli zake za kiroho lakini maombi yake yalionekana kuwa na nguvu.
"Watu walikuwa na fikra akilini ya jinsi ambavyo Mungu angefanya kazi na walipoona kitu tofauti kutoka kwake wakaamini zilikuwa ni nguvu hizo.”
“Walitumia 'muujiza' sawa wa leso, waliuza mafuta sawa ya 'upako' na maji matakatifu ambayo waliamini kuwa yaliponya magonjwa yote na picha zao zilichorwa kwenye fulana na vijikaratasi vilivyotumiwa na wafuasi wao. Lakini kwa sababu hakuwa katika kundi au katika tafsiri yao ya vile wanavyomuona Mungu, alitengwa na kusemwa vibaya ," amesema Osinaike.
Amesema TB Joshua alishutumiwa na wachungaji wenzake kwa kubuni miujiza bandia, na kudai kuwa mchungaji huyo aliwajibu kuwa miujiza hiyo ilikuwa ya kweli akisisitiza kuwa alichokuwa akifanya TB Joshua pia kilikuwa kinafanywa na wachungaji wengine ambao hawakupingwa na watu waliowaamini.
Mwaka 2004, mamlaka ya usimamizi wa matangazo nchini Nigeria ilipiga marufuku vituo vya televisheni kupeperusha matangazo ya miujiza ya wachungaji moja kwa moja kwenye televisheni.
Iliaminiwa kuwa Joshua ndiye anayelengwa, kwamba wachungaji hasimu walikula njama ili Serikali iweke marufuku hiyo kwa sababu alikuwa ametawala vyombo vya habari.
"Huenda alikuwa ndiye mchungaji wa kwanza kutumia matangazo kupitia intaneti kunadi mahubiri yake kwa watazamaji kimataifa ," amesema Adelakun.
Amesema kuwa tofauti na wachungaji wengine, TB Joshua
hakuanzisha matawi ya kanisa lake katika kila kona ya mtaa na mara nyingi familia yake haikuhusishwa na kazi yake, mke wake alionekana mara chache karibu naye na hakuna mtoto wake hata mmoja aliyefahamika kuongoza kanisa lake.
Kwa sasa kanisa lake limefungwa huku wanajeshi wakiimarisha ulinzi kutokana na mamia ya waumini kujaa wakilia na kuomboleza.
"Ilikuwa ni kazi na maisha ya mtu mmoja, ingawa alikuwa na mitume wake. Ni vigumu kuona kanisa likiendelea bila yeye," amesema Osinaike.
Chanzo: Mwananchi