Elections 2010 TBC 1 na mbinu ya kuchakachua hoja za Slaa (PhD)

TBC wote wakiongozwa na Tido na Joe kihampa ni vibaraka ******* wa mafisadi wa ccm na wameahidiwa
makubwa mara baada ya uchaguzi,pumbavu zao na hawanifanyi lolote lile!
 
Jana nimeshuhudia utumbo mwingine uliooza katika mfululizo wa utumbo wanao mwaga na kwa wa Tanzania,

Ndugu wanaJamvi, mie navyoelewa ni kuwa Journalist ni sawa na Mwalimu, more precisely ni MWALIMU kwani anaelimisha jamii kwa yale ayasemayo. Sasa nilipigwa butwaa zaidi pale nilipoona kipofu mmoja (maana wote pale TBC1 ni vipofu) akimfanyia interview fisadi fulani alovimba tumbo, eti ni mtaalamu wa kimataifa in CEMENT PRODUCTION INDUSTRY,,sure kila jambo lina maana.

Kwa juu juu ungeweza kusema kuwa alimaanisha yale aloyasema,kumbe contrary to that,alimaanisha tumbo lake lita-shrink kwa kukosa ile super prifit.Ili nieleweke zaidi,Mfano ni huu,wale mafisadi wa migodi ya dhahabu,ukiwauliza hata leo ambapo they make unconsiderable mega super profit over our resources,watakuambia kuwa hawapati faida kwa kisingizio cha RUNING EXPENSES..But uhalisia ni kuwa wanapata faida kubwa mno.

Yule jamaa jana,alikuwa anasema kuwa 5,000Tsh hailipi kwani hata gharama ya usafiri ipo juu,Kwa kukurupuka ni kweli haiwezekani,lakini anachosema Mh. Rais mtarajiwa ni kuwa tuangalie kuondoa au kupunguza kodi na gharama nyingine ktk uzalishaji,ikiwezekana serikali kuchangia (KAMA NIPO SAWA) ilimradi tuu kuna The real commitiment kuondoa suit za majani na kuwezesha makazi bora.

Anyway,yote hayo ni kujaribu kuona mantiki ya uwezekano wa makazi bora kwa Watanzania.

Pili,JE HAO TBC1 NI JUKUMU LAO KUANGALIA UWEZEKANO WA UTEKELEZAJI WA MANIFESTO YA CHADEMA TUU? JE ZILE AHADI ZA CCM ZINAZO WEZA KUHITA TRILION ZAID YA 50 kutekelezeka wanazihoji?

INGEFAA WAAITE PLANNERS AND ECONOMISTS ILI KUJALIBU KUONA UHALISIA WA MAMBO HAYO KWANI WAO KAMA WAO WANACHOFANYA NI UFISADI WA KUPOTOSHA UKWELI.
 
ALIYEKUWA mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Twiga Cement, Leon Hooper amedai kuwa bei ya mfuko wa saruji haiwezi kushuka na kuwa Sh5,000. Hooper, ambaye amekuwa kwenye biashara ya saruji kwa zaidi ya miaka 25 maeneo mbalimbali duniani, ameeleza kuwa anakubaliana na wazo kuwa sementi ishuke bei hapa nchini, lakini akasema ahadi hizo hazitakiwi kuwa za haraka na ambazo hazina mchanganuo akisema kuwa zinaweza kuuchanganya umma kuhusu bei halisi ya bidhaa hiyo. Hooper ameeleza kupanda kwa gharama za uzalishaji na usafirishaji ambazo ni kati ya dola 50 hadi 80 za Kimarekani kwa tani moja ikitegemea na sehemu ambayo simenti hiyo inapelekwa, zinafanya suala hilo kuwa gumu.

"Nimesikia kuwa kuna vyama vinatoa ahadi kuwa vitashusha bei na kuwa 5,000 katika maeneo kama Mara, Songea na Mwanza, kitu ambacho hakiwezekani kutokana na utaalam wangu," alieleza Hooper. Katika mikutano yake mbalimbali, mgombea urais wa Chadema Dk Willibrod Slaa amekuwa akiwaambioa wananchi kuwa serikali yake itahakikisha bei ya saruji itashuka hadi kufikia Sh5,000 kwa mfuko na pia kushusha bei ya vifaa vingine vya ujenzi ili wananchi waishi kwenye nyumba bora badala ya zile za nyasi na udongo.

Dk Slaa alisema bei hizo zinawezekana kushuka kwa kuwa serikali yake itaondoa kodi zote za bidhaa hizo. Hadi sasa bei ya simenti ni kati ya Sh1,2500 hadi Sh1,300 jijini Dar es salaam wakati mikoani bei inafikia hadi Sh1,700 kwa mfuko. Lakini simenti inayotoka nchi kama Pakistan ambayo iko maelfu ya kilomita kutoka Tanzania, inauzwa kwa bei hiyo ya Sh1,250 sawa na simenti inayozalishwa nchini. Mmoja wa wauzaji hao ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa bei ya jumla ya saruji ya hapa nchini kwa Twiga ni Sh 11,900 na ya Pakistani ni Sh 11,800 lakini ikiingia mtaani huuzwa kwa bei moja ya Sh 12,500. Rais wa Chama cha Wafanyabiashara wa Viwanda, Biashara na Kilimo(TCCIA), Mhandisi Aloyce Mwamanga alisema upangaji wa bei za vitu huendana na gharama za uzalishaji wa bidhaa hiyo.

Akizungumza na Mwananchi juzi, Mwamanga alisema kuwa lengo la mfanyabiashara na mzalishaji yeyote ni kupata faida hivyo ni vigumu kuuza bidhaa kwa bei ya hasara iliyo chini ya mstari wa uzalishaji. "Unataka niuze viazi kwa Sh200 wakati gharama za uzalishaji ni Sh300?, Hilo haliwezekani.

Unajua 'price'(bei) ya 'commodity' (bidhaa), lazima iendane na gharama ya uzalishaji," alisema. Alifafanua kuwa: Lazima uweke gharama zako za uzalishaji, baada ya kuweka gharama hizo za uzalishaji, ndipo utaje bei itakayokupa faida ili kesho uzalishe tena. "Mimi sijiingizi katika siasa, lakini, kama utauza saruji kwa Sh5,000 na gharama za uzalishaji zipo chini ya hapo, Ok," alisema Mwamanga.

Suala la saruji kuwa bei juu nchini lilizengumziwa mwaka jana na katibu mkuu wa Umoja wa Wazalishaji wa Saruji Afrika Mashariki (EACPA), Harpreet Duggal aliyeeleza kuwa kodi zinazotozwa na serikali kwa makampuni ya sementi Afrika Mashariki ziliwekwa ili kulinda viwanda vya bidhaa hiyo dhidi ya ile ya nje ambayo huzalishwa kwa gharama za chinikutokana na makampuni kupewa ruzuku na serikali zao. Akizungumza na gazeti la The East African ambalo ni gazeti dada la Mwananchi, Duggal alisema Tanzania imeathirika kwa kiasi kikubwa na saruji kutoka Pakistan ambayo imetawala soko kwa asilimia 15.

"EACPA inafikiria sana maendeleo haya na tuna wasiwasi kuhusu maendeleo ya viwanda vya saruji Afrika Mashariki kama jumuiya haitachukua hatua zinazofaa," alisema. Mtendaji mkuu wa Baraza la Biashara la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Charles Mbogori alisema akiwa Arusha kuwa kuingia kwa wingi kwa saruji ya bei rahisi kutoka nchi zinazozalisha kwa gharama ndogo, kutaleta matokeo mabaya kwa viwanda vya ndani baada ya muda.

Mbogori alisema kuwa viwanda vya ndani vinakabiliwa na gharama kubwa za uzalishaji zinazotokana na gharama kubwa za umeme, wafanyakazi na mtandao mbovu wa usambazaji haswa usafirishaji wa reli Alisema kuwa miundombinu mibovu na umbali kati ya viwanda vya saruji na wateja pia ni chanzo cha gharama kubwa za uzalishaji. "Serikali za EAC zinatakiwa kuangalia njia nyingine ya kupata umeme wa bei rahisi ili kufanya biashara ya saruji kuwa ya ushindani," alisema.

Saruji ni moja ya bidhaa ambazo ni nyeti hivyo katika suala la kodi imewekewa asilimia 55 mwaka 2005 ambayo ilikuwa kupunguza kiwango cha asilimia 5 kwa mwaka na kuifanya ifikie asilimia 35 kwa mwaka 2009. Hata hivyo, Juni 2008 unyeti katika sekta ya saruji liliondolewa na uingizaji wa bidhaa hiyo kutoka nje ulipunguzwa kutoka asilimia 40 hadi asilimia 25.

"Kitu hiki kilifanywa bila mawasiliano na wadau katika biashara ya saruji," alisema Mbogori.


CHANZO>>


MY TAKE:

CCM 😛uke:
 
mzungu gani huyo na anautaalam gani wanaotuambia hapa!!!
huyu mzungu ni kwamba kapandikizwa n MAFISADI ili aje aupotoshe umma...hatudanganyiki...na tarehe 31/10/2010 ndio mwisho wa hawa wazungu uchwara wanaokuja TZ kujipatia mali bila kuwaonea huruma waTZ.

 

Mie naomba nipingane ya mtaalamu huyu kwani serikali ikitaka inaweza kushusha bei ya cement kufika hata Tshs 4,000. Tuchukulie mfano aliyosema kuwa gharama za uzalishaji zinafikia dola 50 to dola 80 to me this is complete nonsense argument kwakuwa cost of production inaweza kupanda kutokana na gharama za nje na gharama za ndani. Gharama za nje kama vile vipuri vya kununua na kuagiza vinaweza kuwa vimepanda bei hilo linaweza kupelekea gharama za uagiza kupanda kiasi hicho. Serikali inaweza kupunguza gharama hizi kwa kutoa misamaha ya kodi katika uagizaji wa vipuri hivyo ili kushusha gharama za uzalishaji wa saruji nchi (Kama alivyosema Dr Slaa) ikisha gharama hizo za vipuri zikafidiwa na saruji zinazokuja kutoka nje (Pakistani na kwengineko) ili kuvisaidia viwanda vyetu viuze saruji zaidi na vilevile kuprotect ajira za vijana wetu nchini.

Vilevile njia nyengine ya kuweza kushusha hiyo bei ya saruji ni kutoa ruzuku kwa viwanda vyetu nchini ili viweze kuuza saruji kwa bei nafuu. Hili litasaidia Tanga Cement, Twiga Cement na wengineo kuuza saruji kwa bei ndogo kuweza kufikia malengo tuliojiwekea. Serikali kama inaweza kutoa ruzuku za pesa kama pipi katika kilimo bila ya kuwa strategy ya jinsi gani hizo pesa zinaweza kuwafikia walengwa wanashindwa vp kushindwa kuwapa haya makampuni ruzuku ili kushusha bei za vifaa vya ujenzi ili kila mtanzania akawa na pakuishi?

Binafsi I totaly disagree with this non sense argument!!!
 

...TBC imejaa wapumbbavu toka mkurugenzi wao hadi news presenters wote ni bootleaker wa majizi ya nchi hii!
mambo madogo km hayo wala hayahitaji elimu kubwa kupambanua, inajulikana kuwa Slaa anapoongelea bei ya saruji kushuka anaainisha mambo kadhaa pale, KODI,GHARAMA ZA UMEME,USAFIRISHAJI nk yote haya yakihuishwa kwa lengo la kumsaidia mwananchi amudu kununua saruji, bei ya sh. 5,000 kwa mfuko inawezekana, wala hakuna sababu ya kwenda muhoji huyo mzungu sijui walimtoa wapi! halafu kwa nini wao wanakuwa km wanajibu mambo yasiyowahusu? mbona ahadi anazotoa kikwete hatuoni kuuliza kwa hao wanaowatafita kama zinawezekana?

Ningekuwa na uwezo, ningeagiza SITAKI KODI YANGU NINAYOTOA ITUMIKE KULIPA WATU WAPUMBAVVU KAMA HAWA WA TBC!!
 
POOR LEADERSHIP AND CORRUPT GOVERNMENT usitegemee wangelikuja na jibu tofauti na hilo. Waliwekeza sana kwenye umasikini na ujinga wakidhani watanzania wataendelea kuwa mbumbu na kusema ndiyo kwa kila kinachosemwa lakini sasa hali imegeuka.Mtanzania wa leo hata kama bado umasikini unatuandamaa lakini upeo wa kutambua jema na baya, uongo na ukweli tumejikwamua kwa hilo na hii itawasumbua sana mafisadi hata kama mkitutawala, hatatutawala kama mlivyozoea.


Cement inawezekana kushuka mpaka 5,000 kama ambavyo ameishasema DR Slaa na hili liko wazi. Kwa mara ya mwisho nilitembelea Wazo Hill 2000, mali ghafi zote zinapatikana humu ndani, gharama za uzalishaji ukizingatia Wazo Hill tayari wameunganishwa na Songas hivyo upande wa umeme tayari gharama si kubwa kiasi hicho, kuhusu usafirishaji huwezi ukasema production cost is less than than transportation cost within the country otherwise tusingelikuwa tunaimport kitu kutoka nje. Tumeua reli ya kati ili tupandishe gharama za usafirishaji wa bidhaa kwenda bara? Alafu tunasema bei hawezi kushuka. Acheni uzushi CCM hata kama mkipinga ukweli uko hapo hapo, watanzania tumefunguka macho!
 

Lack of visionary leaders, lack of accountability and corruption is the key to Tanzania problems.
 


Cheki shati alilolivaa kama si kada wa CCM ni nani? Hawezi kuisaliti CCM, hawa ndio wacheza dili zote zilizotufikisha hapa, lakini mwisho unakuja.
Aje na data za upatikanaji wa mali ghafi, uzalishaji na usambazaji wa saruji na kodi anayolipa (VAT) pamaja na idadi ya watu aliowaajiri kutoka nje na CV zao huone kama hajajipa jibu la Dr. Slaa.
 
Yaani sie wadanganyika ndio maana Wakenya na Waafrika wa nchi zingine wanatudharau sana TBC1 wametuweka mzungu koko atudanganye hapo kwenye bold mbona hata pale Wazo cement tunanunua TZS 12,000 -13,000 kwa mfuko jamani fungukeni macho
 
Yaani sie wadanganyika ndio maana Wakenya na Waafrika wa nchi zingine wanatudharau sana TBC1 wametuweka mzungu koko atudanganye hapo kwenye bold mbona hata pale Wazo cement tunanunua TZS 12,000 -13,000 kwa mfuko jamani fungukeni macho

Ndio maana Dr Slaa alisema if you think Education is expensive you could try ignorance ndio matokeo ndio hayo Mfunyukuzi
 
mbona misamaha ya mabilioni ya kodi yaliwezekana?
mbona uuzaji wa mbolea kwa sh. 25,000 badala ya 50,000 iliwezekana?
mbona EPA ilwezekana kujazwa mabilioni ya fedha na zikatumika kuliwa na wachache?

Mimi naamini hata ikisemekana 1,000 inawezekana.....!
 
Ukiacha usafirishaji ambao anaouona ni ishu ,je bei ni shilingi ngap? Bei ya sasa ni sh. 13,500 less usafiri wa sh 8,000 less Vat 18% = 2, 430/=
Balance Tsh 3,070.

Ukiondoa usafiri na VAT tayari Cement itakuwa sh 3, 070/= ikiwa na faida kiwandani na kwa mmuuzaji. Kwa hiyo Mzungu amechemka.
Slaa amesema ataondoa kodi . Wasafirishaji wa cement watapewa special rates na kufutiwa kodi .
 
Tanzania bila ccm na kikwete inwezekana........tuliisha amua kutowapa kura ccm na kikwete na mafisadi wake anaowalinda kila siku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…