TBC radio matangazo ya kombe la dunia mnatangaza moja kwa moja kutoka Qatar au mnatangaza kutokea Dar kwa hisani ya runinga?

masare

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2010
Posts
1,791
Reaction score
1,830
Maswali ya kujiuliza
-Mtangazaji yuleyule mmoja siku zote ila wachambuzi tofauti ...Je hao wachambuzi nao wamesafiri hadi Qatar?

-Mechi zinachezwa kwenye viwanja na miji tofauti tofauti....inawezekanaje mtangazaji huyohuyo kutangaza mechi zote kwa siku

-Wachambuzi kuchambua matukio kama penati n.k. kwa kutumia "replay" za TV


Siamini kabisa kama kweli matangazo ya radio TBC yanaruka mojakwamoja kutoka Qatar kama TBC Radio wanavyotaka kutuaminisha.

Nawasilisha
 
Mmepewa hisani ya kuona WC, tulieni muangalie..
Matangazo Live yako Dstv, unaweza yatizama.
 
Mmepewa hisani ya kuona WC, tulieni muangalie..
Matangazo Live yako Dstv, unaweza yatizama.
Nazungumzia Radio (TBC Taifa na TBC Fm) sio Televisheni.....elewa topic
 
unapenda vya bure eeh, lipia dstv bwashee
Sisi tunapenda vya bure ngoja tuendelee kuburudika na wakati mwingine kuumia....
Ila aliyesema vya bure ni ghali hakukosea. Mfano kuna mechi ambazo unapenda zisikupite, halafu ndio hawazionyeshi. Wakati mwingine chaneli yao inapata kifafa.... inaweza kupoteza network kwa dakika kadhaa.........
 

Kama jana usiku[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Tbc
 
Kama jana usiku[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Tbc
usiku wapi Qatar au Tanzania mbagala??? unachekesha ujueee, au unafikiri kila mtuu yupo mbagala???
 
usiku wapi Qatar au Tanzania mbagala??? unachekesha ujueee, au unafikiri kila mtuu yupo mbagala???

Usiku kwa Tanzania,ila pia Qatar ni usiku mana majira yanafana.Una lolote la nyongeza?
 
Wawe Qatar au Bamaga muhimu tunawaona Senegal wanavyonyanyua kwapa mwaka huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…