Wakuu wana JF,
Nasikitika kuwataarifu kuwa TBL wamepandisha bei ya bia kwenye maeneo yetu kabla hata ya siku iliyopangwa kwa madai kuwa serikali imepandisha kodi.
Hivi sasa bei ya kreti ya bia inauzwa 32000/= badala ya 28500/= ya zamani.Jana kwenye depot zao hawakuuza bia kisa serikali imepandisha kodi.Hivi sasa chupa moja inauzwa 2200/= badala ya 1800/=.
Kwa nini sasa wanapandisha bei kabla ya muda wake?
Kwa wanywa pombe mnapaswa kugoma kunywa.
Nimeayajua haya baada ya kutumwa kwenda kununua pombe za harusi ya ndugu yangu.
Maoni yenu.