TCRA yafuta akaunti yake ndani ya X/Twitter. Je, ni maandalizi ya kuifungia mtandao huo wa kijamii?

TCRA yafuta akaunti yake ndani ya X/Twitter. Je, ni maandalizi ya kuifungia mtandao huo wa kijamii?

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2017
Posts
458
Reaction score
1,280
Japo hatua hiyo inaweza kuwa imetokana na sababu nyingine, ukweli kwamba imetokea katika kipindi hiki cha vuguvugu kubwa kuishinikiza serikali iifungie X/Twitter unweza kuyumkinisha kuwa hizi ni dalili za awali za mtandao huo wa kijamii kufungiwa.

Hata hivyo, wakati viongozi mbalimbali wakuu wa kitaifa -Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Spika, kuwataja wachache kati ya wengi -sio tu bado wapo katika mtandao huo wa kijamii bali pia wanaendelea kuutumia, ni uthibitisho kuwa X/Twitter bado ina umuhimu mkubwa kwa Watanzania mbalimbali.

Kichekesho ni kwamba hata “askari wa maadili” walio mstari wa mbele kutaka X/Twitter ifingiwe, wanaendelea kuutumia mtandao huo wa kijamii kufikisha vilio vyao kwa serikali.

Umoja wa Vijana umekuwa mstari wa mbele kuitaka serikali iufungie mtandao huo wa kijamii ikiutuhumu kwamba maudhui yake ni ya ngoni na ushoga na ni kinyume na maadili ya Kitanzania.
 
Cha kuchekesha tu ni kuwa hata hiyo account yenyewe waliyoifuta haikua na lolote la maana na hata ukipitia retweets,likes , comments kwenye post zao unaona ni account iliyokuwa very weak sana.

Mtandao wa X sio Tanzania ni dunia nzima ambao umebaki na nguvu kubwa hasa kwenye "free speech" ni mtandao ambao umewalinda wengi dhidi ya serikali ovu zilipokuwa zikitaka kuwafuatilia ndio maana hata Mlawa hakuwa na account active mtandao mwingine tofauti na kule enzi za giza.

Kwangu huo ndio mtandao pekee uliobaki ambao sauti za umma zinasikilizwa hata ukiwa dunia ya tatu huko.
 
Kwani kazi ya vpn ni ipi!? Hakuna kitakachobadilika, Mbona Club House wameifungia muda sana ila kila siku watu tunajaa kule!
 
Kwa hiyo dawa ni kuifungia mitandao, au watawala waoga na wasio jiamini ndiyo wanatakiwa kujitathmini!!
 
Kufungia X ni sawa na kumfungia ndani binti yako aliyepevuka.
 
Back
Top Bottom