TCRA yasomesha watatu kwa Sh 2.2 bilioni

Jamani acheni kulalamika,kozi za mambo ya mawasiliano ni aghali sana
hahahaha si utoe mchnganua basi!
Au ukisoma Mawasilianao una kodishiwa chuo kizima?
 
Hivi upungufu wa madawati nchi nzima gharama yake sh. ngapi?
Mtoto anakaa chini wengine wanasomeshwa ka 2.2 bilioni? manina walai!

Umegusa ndipo mkuu,maana hapa tunajadili watu 3 kupewa elimu tena ya muda mfupi kwa vijisent bil.2++ wakati akina kayumba hawana madawati,walimu,vitabu na kaka zao vyuoni wanakosa mikopo!aaargh!!
 
Umegusa ndipo mkuu,maana hapa tunajadili watu 3 kupewa elimu tena ya muda mfupi kwa vijisent bil.2++ wakati akina kayumba hawana madawati,walimu,vitabu na kaka zao vyuoni wanakosa mikopo!aaargh!!
Kuna vitu vinatia hasira nchi hii we acha tu
 
Kwenye RED:
Kama tunakubaliana na majibu hayo watanzania nis shuruti pia tukubaliane na ndugu zetu wa MOI Muhimbili waliopasua kichwa badala ya goti.
Wao pia ni binadamu. Hawana viungo vya ziada kuwazidi wahasibu wa TCRA
Why double standards!
 
Jamani acheni kulalamika,kozi za mambo ya mawasiliano ni aghali sana

Nafikiri tukiweka akili vizuri utagundua kuwa hiki kitu hakiwezekani na si cha kweli. Hakuna CEO atakayesaini kitu hiki hata kama haoni.
 
Ardgggg ndio maana huku huwa napita tuu maana mambo mengine yanakatisha tamaa
Wanafunzi wanakosa mikopo ya milioni moja tuu wakasome pale UDSM ila kuna watu wanajilipia 2billion kujisomea nje
na bado mtu anasema sio ubadhirifu ni makosa ya kibinadam
aaarrgggg
 
Leo nimetokwa machozi. Nchi haina uongozi haina wenyewe. Nimesoka uk wa kwanza wa mwananchi kuwa tcra imetumia 2.2 bilioni kusomesha wafanyakazi watatu kwa mwaka mmoja. Nimepiga mahesabu hela hii ingesomesha watoto wa tanzania 300 vyuo vikuu hadi wamalize. Vijana wetu wanaambiwa hakuna hela ila kumbe wakubwa wanalipana mabilioni.

Wale washabiki wa ccm kina malaria sugu shangilieni tena. Mnashangilia wenzenu wanaokula, walioamua kuiangamiza nchi. Shame to ccm, shame to jk
 
Loh!! Hallelujah!!

Kuna watu kumbe wanaishi kama malaika hapa duniani.
 
Tungoje na mengine mengi tutayajua.. Hii inauma maana hata mahakamani hawataenda
 
Acha bana Mibange!!
Hiyo ni balaa, acha niitafute habari yenyewe manake inatia hasira!! 2Billion??!!:hatari:
 
bilioni 2.2 kusomesha watu wa2! u can't e serious man! walipelekwa kusoma kwenye kituo cha angani 'space station' nini?
 
Yawezekana ni kweli kuwa hizo gharama ni halisi kama kozi hiyo walioenda ni very expensive - yaani kama ili-involve practical sessions za kuangalia mawasiliano yalivyo ukiwa mwezini, kwenye space station au ukiwa out of the Earth's atmosphere!!! Hivyo mmoja alienda kwenye space station, mwingine mwezini na mwingine kuwepo hapa duniani!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mkiambiwa nchi hii ni tajiri mnabisha -- tena mmoja kati ya wale wanafunzi namjua ndiyo karudi nchini hivi karibuni. Hapo ndipo nakumbuka ule waraka wa LEMA kabla ya kuingia lupango.

Nchi itajengwa na wenye moyo wachache tu tuliobaki.
 
labda hawakuelewana ...nafikiri walimaanisha ni gharama walizonunulia chuo
 
wizi wa aina hii ndio unaliaangamiza taifa hili matokeo yake ni uingereza kuiambia serikali ikubali ushoga wapewe misaada akati mabilioni ya fedha yanaporwa na waizi wachache tu, infact huko TCRA hata wafanya kazi wanalipwa kwa dola, kati ya fedha billion 45 walizo kusanya TCRA matumizi yalikua billion 30 alafu watu wanatetea ccm na dola yake ya majambazi ni aibu kwa tz.
 
Jamani 2billions watu3 asa mbona hamukutupa mchanganuo wa hayo matumizi.
Wajameni mi nahisi hii country sasa...inaliwa na watu3..
 
Siku imeshaharibika ngoja niondoke hapa
 
ni wanafunzi wangapi vyuoni wangepata mikopo kwa hizo pesa walizotumia kuwasomeshea hao jamaa watatu?
 
Nilipata kumfahamu DG wa TCRA, Prof John Nkoma alipokuwa Botswana, ni miongoni mwa Watanzania makini waliopata kutokea, siamini kama angeweza kuwasomea wafanyakazi watatu kwa Billion 2.2, something is wrong somewhere...
 

Du!! Kama walikuwa wanasoma digrii ambao itasaidia Tanzania kuondokana kabisa na tatizo la umeme hapo sawa. Lakini vinginevyo huo in ukichaa mkubwa sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…