TCRA yasomesha watatu kwa Sh 2.2 bilioni

Yetu macho na masikio, ngojea tuone hawa watu watachuliwa hatua gani????
 

Hizi self enrichment project zinazoendelea sasa zitaiangamiza nchi kama hatutachukua hatua. Hicho ni chombo cha serikali. Kilichotakiwa kufanyika ni kuusimamisha uongozi with immediate effect na kufanya uchunguzi wa rushwa haraka.

Haya mazingaombwe sijui yatakwisha lini jamani??? Hii ni tamaa, uroho au ndiyo time ya Chukua Chako Mapema (CCM) kabla ya 2015??
 

Inawezekana walibadilishiwa ubongo wakawekewa wa kizungu ili wafikiri kama wazungu LOL
 
Hili gap la wenye nacho na wasionacho linatia kinyaa hapa nchini. Elimu ambayo ndio ingewakomboa waTZ na kuinua nchi ndo kwanza 'inafitiniwa' bila aibu na mijitu iliyosomeshwa bure. waTZ tuamke kwa kuikana CCM kwanza mengine yafuatie hapo.
 
manina zao.........na huyo anayejiita mdhibiti n amkaguzi wa hesabu za serikali naomba arekebishe title yake kuwa mkaguzi wa hesabu za serikali maana udhibiti haupo hapa!
 
Haya mambo hayataisha mpaka hapo tutakapoacha kuabudu accademic qualifications na kuangalia zaidi TRACK RECORD OF PERFORMANCE! performers wengi wamezama huko chini ya mfumo; walanguzi wa vyeti ndo wanapanda vyeo. Ukiwa well connected unaambiwa tafuta cheti fulani basi! Nobody cares wewe umeshafanya nini huko nyuma.
 
kwa kweli inauma sanaa! kuona watanzania wengi wanateseka maskini ,huku watu wachache wenye tamaa wananeemeka kihivyo!
 

Hawa si watakuwa walikaguliwa vitabu vyao na Auditor General kabla ya kamati kupitia. Inamaana Auditor aliona mambo safi tu. Ushenzi mtupu.

Kuna taasisi ngapi zenye matatizo kama haya.
 
Kwa kweli lile shirika ndio maana limeshindwa kuboresha huduma zake kwanza kupunguza tariffs za kwenye simu huwa gaharama ni kubwa mno Tanzania na ndio hata Dstv huwa tunalipa viwango kubwa sana Tanzania ikilinganishwa na nchi akama Angola wa Premium ya USD 78 kwa Tanzania wao ni dola 40 na hii inatokana kodi kubwa inayopelekwa TCRA yaaani Prof Nkoma is a failure kwani fees anazokusanya kwenye mashirika ya communication ni mwiba kwa mashirika ambao yapo kwenye sekta ya mawasiliano. Sasa basi ni pesa wanachukua mashirika ya cm na kuishia matumbo mwa TCRA ushauri ni bora nkoma na wezi wenziwe wang'atu tu tumechoka kuonewa.
 
Mpaka kufika 2015 patakuwa hapatoshi Bongo
 
huyu jaji alokua anasoma hyo taarifa ni KILAZA

Tena kilaza hasa! Nikifikiria ni watanzania wangapi wamehukumiwa kwa mkono wake ikiwapo kunyongwa hadi kufa sina hamu. This situation shows the type of people we are having in the public sector.

Nilivyokuwa nasoma gazeti sikuamini kwamba majibu yalikuwa yanatolewa na Mh. Jaji kwa Kamati husika kutetea wizi na ufisadi ulikubuhu. Nilitegemea chombo ambacho Mwenyekiti wa Bodi ni mtu wa aina ya Jaji na Mkurugenzi Mkuu ni Profesa tena anayeheshimika kimataifa, basi chombo hicho kingekuwa na uadilifu uliotukuka kama si kupindukia lakini wapi!

Nikikumbuka ile hukumu maarufu ya "mgombea binafsi" iliyotolewa na jopo la majaji saba wa Mahakama ya Rufaa, nikikumbuka vituko mbalimbali vifanywavyo Bungeni dhidi ya maslahi ya wananchi na taifa, nikikumbuka ufisadi na ubabaishaji uliojaa serikalini na mambo mengine chungu nzima; nafikia conclusion kwamba nchi yetu inaangamia kama siyo kusambaratika kabisa.
 

..there you r! tena kuanzia at family levels, watz hawana disciline kabisa!!! on anything!
 
Nilipata kumfahamu DG wa TCRA, Prof John Nkoma alipokuwa Botswana, ni miongoni mwa Watanzania makini waliopata kutokea, siamini kama angeweza kuwasomea wafanyakazi watatu kwa Billion 2.2, something is wrong somewhere...

Mkuu, hii imetokea kwa sababu ya mfumo wetu wa kiutawala ulishakufa. There is absolutely zero good governance and personal responsibility. Hakuna atakayejiudhuru kutokana na hili. Kila mmoja katika nafasi yake kuanzia kwa Bodi ya Wakurugenzi, DG, menejimenti utamsikia akijitetea na kujilinda kwa kutoa visingizio lukuki. Subiri hivi visingizio utaniambia kuanzia leo hii utaona Press release kwenye TV, magazeti kesho.

Bila, kupata Sata wa Kitanzania au China style tutaendelea kupata habari za uozo kila siku bila ya watu kuwajibika au kupelekwa Segerea. Ni hatua mbaya sana tuliyofikia kwa nchi ambayo ilikuwa kioo cha haki na uwajibikaji.
 
hizi kamati za bunge zikishabaini kuna ubadhirifu au upotevu wa pesa za umma then what next? Am tired of this trend of business as usual.

hayo ndiyo madili yao......nasikia wanakasirika kama wanakagua hesabu halafu hawapati kosa.......wananuna kama trafiki barabarani wakikukuta bila kosa la triangle na fire extinguisher kwenye gari.
 
nimejaribu ku google gharama ya kusoma chuo babu kubwa kama mit usa naona tuition fee kwa mwaka ni kama dola 40000 sawa na tsh million 70 na kitu hivi, hiki chuo cha bilion 2.2 kwa wanafunzi 3 ni kipi isije ikawa ni mambo ya pangu pakavu?????
 
Duuh! Hao jamaa itakuwa walikuwa wanasomea kushikiria mkonga wa mawasiliano ndani ya bahari. Ili usije kutawanya mawasiliano halafu samaki wakaanza kutumia internet bila kulipia.
Hii mbona kali! Wanasomea nini hicho cha ajabu???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…