Kutokumaliza MSc au PhD huko SUA na vyuo vingine vingi vya mchepuo wa sayansi kunasababishwa na sababu nyingi na sio kuangusha lawama zote kwa masupervisors.
Kwanza inawezekana mwanafunzi ni mzembe, au sio mzembe ila ana mambo mengi, mara nyingi wanafunzi wa huku juu wanakuwa na majukumu mengi maana ni watu wazima kwa hiyo unakuta hawatengi muda wa kutulia kufanya tafiti na kuandika tafiti nzuri. Hii inapelekea wanafunzi wengi kutengeneza data zinawapa wakati mgumu kuzianalyze na kuandika majibu vizuri. Kupitia huko husababishia hata supervisor nae kupata tabu sana kusoma na kuelewa kazi ya mwanafunzi, unakuta supervisor anachukua muda mrefu sana kuinyoosha kazi ya mwanafunzi kazi ambayo kiukweli alitakiwa kuifanya mwenyewe akiwa ametulia. Pia wanafunzi wajue kusoma kazi ya mtu inategemea pia na hamasa yaani namaanisha uandikaji wa mwanafunzi, ni kama vile unavyosoma hadithi kama mwandikaji anamtiririko vizuri,msomaji unapata hamasa zaidi.
Pia kuna tatizo la walimu ambalo wengi mmegusia, hakika ni kweli kuna aina ya walimu hawatumii muda wao kumsaidia mwanafunzi kuanzia mwanzo wa kufanya tafiti na hii inapelekea kugundua mwanafunzi amefanya tafiti wakati muda umeshapita na inakuwa ngumu kurekebisha. Pia hata akipelekewa kazi asome basi itamchukua muda mrefu kuisoma kwa sababu ya kuwa na mambo mengi nje ya tafiti, walimu siku hizi wamekuwa busy kufanya kazi za part time vyuo vingine, unakuta mwalimu anafundisha zaidi ya vyuo 5.
Mbali na sababu ya wanafunzi na walimu wao, sababu nyingine ni aina ya tafiti yenyewe, kiukweli kuna tafiti zinahitaji muda mrefu na zinachamoto nyingi ambazo mtafiti anakutana nazo, mfano kwa wale wa kilimo unakuta magonjwa unaharibu na kuchelewesha umalizaji na upataji wa majibu katika muda muafaka
Sababu nyingine ni upatianaji wa vifaa ambavyo wanafunzi wanahitaji kwenye tafiti, vingi na vya kuagiza nje ya nchi. Wakati mwingine mwanafunzi hawezi kuendelea na tafiti akingojea kifaaa au chemical kwa zaaidi ya mienzi sita.
Kwa Sababu hizo ni ngumu kwa wanafunzi kumaliza kwa muda wa miaka miwili, na hii sio SUA bali ni vyuo vingi vya sayansi, Tanzania na Afrika kiujumla