NetMaster
JF-Expert Member
- Sep 12, 2022
- 1,454
- 4,925
Kwa kuanza niseme tu kwamba kama vilevi hivyo havikuathiri kimaendeleo basi we endelea tu kuselebuka, Wapo watu kama kina snoop dog wanavuta bangi kwa muda mrefu na maisha yao wala hayana shida zaidi ya kutoboa zaidi.
Maada hii ni kwa wale ambao wanataka kubadili maisha yao na kuona wazi kwamba vilevi hivi vinawawekea vikwazo katika maendeleo yao kiuchumi, kijamii, kiafya, kisaikolojia, n.k. wanatamani kuacha lakini uraibu umewakamata sana.
Hali ya kwanza unapojaribu kuacha vilevi hivi ni kwamba unaacha lakini huna kingine cha kufanya na unaendelea kushinda na marafiki wale wale wa viti virefu, kublaze bangi viwanjani, n.k., kiufupi unakuwa hujabadilika ila ni kwamba umeacha kutumia kilevi, Matokeo yake hapa ni kwamba utaboreka sana, marafiki zako na mazingira yale yale yatakuzonga na mwisho wa siku utarudi tu kuanza upya ulevi wako tena kwa speed ya 4g yenye ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Wengi wakijaribu kuacha huwa wanapita njia hii.
Hali ya pili unapojaribu kuacha vilevi hivi ni kwamba inabidi utafute mbadala wa kitu cha kufidia mda wa ulevi, kuadili circle ya marafiki, mazingira na hali uliyokuwa nayo unapotumia kilevi. Hapa unaweza kujiwekea malengo mapya kama kupiga mazoezi, kujifunza vitu vipya, kuweka malengo mapya, kufungua biashara za ziada za kwenda kushindia ukitoka kazini, kujiunga na vikundi vipya kama vya wasoma vitabu, kwaya, kucheza draft, n.k. kwa kampani mpya. inabidi uanze kujichukulia majukumu mapya yeye tijamaishani mwako, hali hii inakusaidia kubadili mazingira, marafiki na kujua kwa kuipatia furaha mpya katika maisha yako mapya,
Kupitia mbinu ya pili baada ya muda utajikuta umeanza kupata mabadiliko positive makubwa sana, hautakuwa tena mtumwa wa kujihisi mpweke usipokuwa na marafiki walevi, hautakuwa mtumwa wa kuipata furaha yako kwenye vilevi pekee, vilevi hivi unaweza kujikuta unaviacha kabisa moja kwa moja ama kupunguza matumizi yake katika viwango ambavyo hukuwahi kuja kudhani utaweza na hatimae kuacha kabisa,
Maada hii ni kwa wale ambao wanataka kubadili maisha yao na kuona wazi kwamba vilevi hivi vinawawekea vikwazo katika maendeleo yao kiuchumi, kijamii, kiafya, kisaikolojia, n.k. wanatamani kuacha lakini uraibu umewakamata sana.
Hali ya kwanza unapojaribu kuacha vilevi hivi ni kwamba unaacha lakini huna kingine cha kufanya na unaendelea kushinda na marafiki wale wale wa viti virefu, kublaze bangi viwanjani, n.k., kiufupi unakuwa hujabadilika ila ni kwamba umeacha kutumia kilevi, Matokeo yake hapa ni kwamba utaboreka sana, marafiki zako na mazingira yale yale yatakuzonga na mwisho wa siku utarudi tu kuanza upya ulevi wako tena kwa speed ya 4g yenye ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Wengi wakijaribu kuacha huwa wanapita njia hii.
Hali ya pili unapojaribu kuacha vilevi hivi ni kwamba inabidi utafute mbadala wa kitu cha kufidia mda wa ulevi, kuadili circle ya marafiki, mazingira na hali uliyokuwa nayo unapotumia kilevi. Hapa unaweza kujiwekea malengo mapya kama kupiga mazoezi, kujifunza vitu vipya, kuweka malengo mapya, kufungua biashara za ziada za kwenda kushindia ukitoka kazini, kujiunga na vikundi vipya kama vya wasoma vitabu, kwaya, kucheza draft, n.k. kwa kampani mpya. inabidi uanze kujichukulia majukumu mapya yeye tijamaishani mwako, hali hii inakusaidia kubadili mazingira, marafiki na kujua kwa kuipatia furaha mpya katika maisha yako mapya,
Kupitia mbinu ya pili baada ya muda utajikuta umeanza kupata mabadiliko positive makubwa sana, hautakuwa tena mtumwa wa kujihisi mpweke usipokuwa na marafiki walevi, hautakuwa mtumwa wa kuipata furaha yako kwenye vilevi pekee, vilevi hivi unaweza kujikuta unaviacha kabisa moja kwa moja ama kupunguza matumizi yake katika viwango ambavyo hukuwahi kuja kudhani utaweza na hatimae kuacha kabisa,