Telegraph From Iddi Amin Dada kwa Nyerere Kisa cha Vita ya Kagera?

duh hata mie hii niliisikia tena nliion video yake AMIN akijisifu kwa kuituma kwa NYERERE ... ila ilikua miaka ya nyuma sana kabla ya vita...nafikiri miaka mitano hivi before the war
 
ndio maana mwalimu akaamua kumwita idi amini 'DADA' sababu ya mambo yake ya ki dada dada
 
Yatufaa sote tujadili zaidi vichwani mwetu kuliko kurukia hitimisho ambalo ni upuuzi. Je, kuna ushahidi gani kwamba maneno hayo ya Iddi Amin ndiyo yalikuwa chanzo cha vita? Tusipoangalia, tutakuwa tunadai kwamba jua linachomoza asubuhi kwa amri ya jogoo. Chuki yako kwa JKN angalao iongozwe na ubunifu wa hoja zaidi.
 
Hapana, Mwalimu hakuwa na visasi namna hiyo, na wala hilo la Telegram lisingekuwa jambo kubwa sana kwa Mwalimu. Kumbuka kuwa aliwahi kumsamehe Gaddaffi ambaye alilite jeshi lake kutupiga, lakini bado mwalimu alimsamehe na kumsaidia kupeleka mkutano wa OAU huko Libya. Vile vile Mwalimu aliwasamehe akina Lifa Chipaka, Titi Mohammed na wengineo waliokuwa wamekutwa na hatia ya kutaka kumwua yeye binasfi. Kuna taarifa kuwa hata Zakaria Hanspope aliachiwa siyo kwa hurumua ya Mwinyi aliyekuwa madarakani wakati huo bali ilikuwa ni kutokana na huruma ya Mwalimu mwenyewe. Nyerere huyo huyo aliwahi kumkaribisha Amini Mwanza bila kukaribishwa, lakini mwalimu akamvumilia. Mwalimu angekuwa jeuri na mwenye visasi basi angeamuru ndege ya Amini itunguliwe ikiwa angani kwa sababu kuwa ilikuwa ni ndege ya kijeshi iliyokuwa imeingina katika anga la Tanzania bila kibali.

Idi Amini mwenyewe ndiye aliyenunua kipigi hicho kwa bei nafuu sana kwa kuvuka mipaka ya aina yote dhidi ya Tanzania: (a) kwa kuishambulia Tanzania mara kwa mara kwa mabomu na ndege za kivita, na (b) kuhamishia sehemu ya jeshi lake nchini kwetu na kuweka bendera yake katika eneo la Tanzania.
 
well said mkuu,mwalimu hakuwa mtu wa visasi na wala hakuwa kiongozi mzandiki na mbinafsi,nakumbuka alipoiteka ndege ya kivita ya libya uwanja wa ndege wa mwanza,akawakamata makomandoo wale waliotumwa na ghadafi,baada ya vita kuisha ,akamrudishia ghadafi makomandoo wake na ujumbe kuwa''nilidhani utaleta wanajeshi vitani,kwa nini unaniletea watoto wa shule''??chukua watu wako,ila ndege hakurudisha
 
Mwl alitufundisha uvumilivu na inapobidi kujilinda hata kama ni maskini , heko Watanzania wa kipindi kile kwa uzalendo.
 
Kumbe vilikuwa vita vya kibinafsi! vikituacha wengine kulipia hadi leo hii,achilia mbali waliomwaga damu zao, walioachwa wajane, watoto walioingizwa katika uyatima...

Hivi ulitegemea Nyerere kama amiri jeshi mkuu afanyeje pale ambapo mshenzi kama Idd Amini alipovuka mpaka, kuua raia wetu na kutangaza ardhi yetu kuwa yake??
Watu walikufa Kagera, mali ziliharibiwa, wanawake walibakwa, watoto wasio na hatia waliuawa kinyama na majeshi ya amini. Ultegemea nani awaokoe wahaya kama si majesh yao chini ya amri ya amirijeshi wao? Halafu bila aibu unasema ni vita binafsi??? Shame!
 
Nasikia na udini ulichoa sana vita ile hivi kweli?
 
Nasikia na udini ulichoa sana vita ile hivi kweli?[/QU ....... Mzee wako ndio alikuwa wa kwnza kuleta mambo ya udini ndio maana hata karne hii wewe unatuletea udini coz umelithishwa na baba ako
 
AMINI Alimchukia NYERERE kwasababu alimpa hifadhi ya kisiasa obote na mwl alikuwa kwanza kumlaani iddi amin alipompindua obote
 

Habari hii inawajia Kutoka Radio Tanzania Dar es salaaam, Msomaji wenu ni David Wakati.
 


sijapata ona mtu akimdharau/kejeli mwalimu na bado akashinda nasema sijaona: This guy must be saint!
 
Kweli huyu jamaa alitudharau sana lakini nilichompendea ni hiki hapa!



Na hii hapa!


Kumbe watu walikuwa wanampenda kisi hiki hadi kumbeba? Ndallo hata wewe unaweza kufanya hivi? Unyama ni unyama tu regardless unafanyika kwa nani
 
Last edited by a moderator:

Vitendo gani tulikuwa tunamchokoza Id Amin?
 
"ukubwa jaa" mkuu,ukiwa kiongozi unatakiwa utumie busara hata watu wakikutukana.
Imagine wewe ni mkuu wa nchi. Mkuu wa nchi nyingine anakutukana kiasi hicho na ukanyamaza eti ni vita binafsi...kwangu haiingii akilini. Nitampiga na wananchi wangu watanisupport kuondoa dharau kwa kiongozi mkuu wa nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…