Ten Hag kazini kwake kuna kazi

Ten Hag kazini kwake kuna kazi

Fakyuol

Senior Member
Joined
Nov 26, 2023
Posts
148
Reaction score
325
Klabu ya Manchester United inafikiria kumpa kazi katika nafasi ya kocha mkuu, mkufunzi wa timu ya taifa ya Uingereza Gareth Southgates.

Mmiliki mwenza wa klabu hio bwana Jim Ratcliffe, anaamini kocha huyo ndie mbadala sahihi wa mwalimu wa sasa bwana Erik Ten Hag itakapo fika mwishoni mwa msimu huu. Kupitia vyanzo mbalimbali ambavyo vipo karibu na Jim Ratcliffe, vinadai kwamba mmiliki mwenza huyo ni muumini mkubwa wa mwalimu huyo raia wa Uingereza.

Mkataba wa Gareth Southgates na shirikisho la soka la Uingereza utafikia tamati mwezi December mwaka huu. Lakini licha ya juhudi mbalimbali za shirikisho hilo kumtaka asaini kandarasi mpya, mwalimu huyo ameonekana kusuasua kuongeza mkataba mpya, huku akidai atarudi kwenye meza ya mazungumzo pale tu michuano ya Euro 2024 itakapo tamatika.

#Unaambiwa
 
sizani kama SouthGate anatosha Old trafford zaidi zaidi atajaza wangiireza wezake kwenye timu
 
Klabu ya Manchester United inafikiria kumpa kazi katika nafasi ya kocha mkuu, mkufunzi wa timu ya taifa ya Uingereza Gareth Southgates.

Mmiliki mwenza wa klabu hio bwana Jim Ratcliffe, anaamini kocha huyo ndie mbadala sahihi wa mwalimu wa sasa bwana Erik Ten Hag itakapo fika mwishoni mwa msimu huu. Kupitia vyanzo mbalimbali ambavyo vipo karibu na Jim Ratcliffe, vinadai kwamba mmiliki mwenza huyo ni muumini mkubwa wa mwalimu huyo raia wa Uingereza.

Mkataba wa Gareth Southgates na shirikisho la soka la Uingereza utafikia tamati mwezi December mwaka huu. Lakini licha ya juhudi mbalimbali za shirikisho hilo kumtaka asaini kandarasi mpya, mwalimu huyo ameonekana kusuasua kuongeza mkataba mpya, huku akidai atarudi kwenye meza ya mazungumzo pale tu michuano ya Euro 2024 itakapo tamatika.

#Unaambiwa
Unauza bunduki na kununua panga.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom