Terminal ya SGR kuwa katikati ya jiji

Mkuu vipi kuhusu intercity buses zinaanziaga wapi?
City centre. Kwa watu wenye akili public transport inaanzia in the heart of the city. Private cars ndio wanatumia mbinu tofauti kuziondoa katikati ya jiji.
 
Kutokana na uzoefu wangu binafsi, naona wako sahihi kuweka station ya SGR kule City Center, wako sahihi kabisa kuhusu hilo. Isipokuwa tatizo lipo kwenye Designing ya mtandao wa reli yenyewe. Reli kwa Treni za namna hiyo nimeona aidha ziwe za juu, Yaani katika maeneo ya mijini kulikojengeka sana treni inapita kwenye madaraja ya juu (overhead bridges) na hata stations zake zinakuwa huko huko juu kwenye majumba ya ghorofa au treni hizo zinapita chini ya Ardhi kwenye handaki (underground railroad) na stations zake pia zinakuwa huko huko chini ya Ardhi kwenye mahabdaki. Majengo ya stations yanakuwa na lift za Watu kushuka au kupanda. Walichokosea SGR hii ya kwetu ni Designing ya Ujenzi wa Reli yenyewe, kwa sehemu kubwa Sana reli ya SGR imepita kwenye usawa wa Ardhi (on the Land surface), kitu ambacho Siyo sahihi hususani kwenye maeneo ya mijini Kama Dsm kwaw sababu inaingiliana na shughuli zingine za binadamu.

Mathalani, ktk Jiji la Dsm Ile reli ilipaswa kuwa juu ya madaraja kuanzia kule Station bandarini na ingeenda kushuka na kuwa katikà usawa wa Ardhi (on surface railroad) kuanzia katikà eneo la Kisarawe na kuendelea kuelekea Morogoro.
Design ya reli ya SGR iliyopo hivi sasa ni ya hatari Sana kiusalama hususani kuanzia eneo la jirani na Airport, kiusalama ile reli haikupaswa kabisa kupita kwenye usawa wa Ardhi kwenye maeneo hayo ya airport. In case of any emergency that may occur in the airport premises, people from the Airport (JKNIA) have a very limited chance to escape the dangers or to be rescued due to the railroad barrier that located in the side of Vingunguti suburbs after crossing Nyerere Road.
 
Bora Dar inapita juu ya nguzo... Ok la walichokifanya Morogoro Iko siku wataibomoabhiuo relibili waombee Kura.

Wameziba mitaa kwa tuta kuubwa.. madhara yake.. kwanza wameziba njia za Maji, hata yale mafuriko kwa kiasi kikubwa yamechangiwa na tuta la reli ya mwendo kasi baada ya kuziba njia nyingi za asili za Maji na kuyalazimisha yapite katika sehemu chache walizoziacha kufuatana na mkondo mkuu wa Maji.. pili wamewatia wananchi umasikini na kuwaongezea gharama zisizo za lazima..

Kwa sasa frame nyingi hazitumiki kwakua hazipangishiki na chache watu wamezigeuza vyumba na mabanda ya kufugia kuku.

Mitaa imekosa wapangaji na waliokuwepo wengi wamehama kwakukwepa gharama za mzunguko kutokana na tuta hilo.

Hizo nguzo ilitakiwa na huku ziwekwe ili chini watu waendelee na mishe zao kama kawaida.

Natabiri kuna mwaka itatoka reli itabomolewab ili waweke nguzo.. tusubiri ahadi zao tuu

Mtaa wa karibu na Youth mission umetengwa utadhani sio sehemu ya makazi na kuna kituo cha Afya lakini barabara zina zaidi ya miaka mitano hazijawahi guswa na TARURA. so madaraja yana zaidi ya miaka hayatengenezwi na kuufanya mtaa kukosa wapita njia... zaidi ya wakazi tuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…