Termination on medical grounds

Claranito

Member
Joined
May 26, 2014
Posts
28
Reaction score
3
Habari za kazi!

Kuna mfanyakazi alipata ajali lakini nje ya ofisi. Alikuwa position ya mlinzi, sasa alipewa likizo ya kuumwa ya siku 126 kama sheria ya ajira inavyosema. Siku zimekwisha lakini Inavyoonekana bado hayuko katika hali nzuri kwani mkono uliwekewa chuma na hivyo itakuwa vigumu kwake kufanya kazi hasa katika nafasi hiyo ya mlinzi.

Nauliza ni procedure gani zinapwa kufuatwa kama unataka kumuachisha kazi kwa sababu za kuumwa? Asanteni na nitafurahi kwa ushauri.
 
Kama alishapewa sick leave kulingana na takwa la sheria ya kazi na mahusiano kazini, 2004/6.

Kinachofuata ni taratibu za fair termination.

So atalipwa stahili zake zote.

Sheria haimfungi mwajiri ampe kazi tofauti kwani na yeye yupo after profit maximization.
 
Asante sana. Malipo anayotakiwa kulipwa ni kama yapi? maana mkataba wake ni mwaka mmoja mmoja, huu ni mwaka wa pili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…