Tetesi:ATCL kurudishiwa AOC TAR 24....

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
57,951
Reaction score
32,619
Habari zilizotufikia zinasema kampuni ya ndege ya atcl inawea kurudishiwa kuanza kurusha ndege zake tar 24...chanzo chetu kutoka TCAA kinasema
katika makabrasha yanaletwa kuna baadhi imeamuliwa wayachukue kama yalivyo na baadhi zisaihihishwe amabzo mpaka tar 21watakuwa wameshamaliza na hivyo kutoa nafasi kurudishiwa kabla ya tar 25...
kila la kheri ila mawazo yetu yabaki kama yalivyo wahusika wote waliohusika washugulikiwe vilivyo.....
 

Matatizo yalipofikia, ni sawa na TANESCO ilivyo. Mwaka huu nimesikia TANESCO wamelipana BONUS, ili hali waliunganisha wateja 50,000 tu kwa mwaka, tena ni record ya mwaka huu, miaka ya nyuma ni 20,000 kwa mwaka. Watanzania wako 46ml, kati ya hao 10% ndiyo wanaishi kwenye nyumba zenye umeme wa GRID! Idrissa na wenzake wanawezaje kugawana BONUS ili hali nchi iko gizani? Walitakiwa ile BONUS watoe kwa wateja kama offer kwa free connection kwa mwaka mmoja nchi nzima. Naamini the following year wanaweza wakashangaa kwa mapato yatakavyokuwa!

Lakini Tanesco wakibanwa wanasema deni ni la Serikali na si lao, wenyewe wanaumia kwa makosa ya Serikali! Hii ni akili kweli? KIla kitu wakishauriwa wanadai ati deni tatizo! Mimi nadhani, wangeweza kuunganisha umeme kwa wadau wote wakiwemo jamaa wa Madini, TANESCO inaweza kuwa richest company in East Africa.

Hela wanayolipana BONUS inaweza kuwa kianzio kizuri. Plus mobilisation ya tarrifs collection.

Mwanzoni niliposikia Idrissa anakwenda TANESCO nikajua sasa mambo yamekuwa mambo. Kumbe hata hivyo nilishindwa kujua kuwa na yeye alikalia account ya EPA akiwa BOT, timing tu ya mlipuko ndiyo imem-save, kama Tibaigana alivyokoswakoswa kimiujiza na sakata la Kombe!

Mungu Ibariki sana nchi yetu
 
Kama TCAA itafuata sheria ya kuregulate airlines properly , hii kampuni ya Ndege ATCL haiwezi kurudishiwa cheti cha kurusha ndege zake mpaka hapo itakapoonyesha kuwa ina mtaji wa kutosha wa kuwahudumia wateja wake kikamilifu na kufuatana na taratibu za ndege za biashara za kimataifa!! Je serikali iko tayari kurecapitalize kampuni yetu ya ATCL?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…