Wadau wa soka na watz wenzangu nina mtizamo, nianze na swali kwanza. Ni wachezaji wangapi wa kitanzania wanacheza vilabu vya Uganda, Rwanda, Burundi na Kenya? na ni wachezaji wangapi toka hizo nchi majirani zetu wanacheza hapa kwetu? jibu ni moja, wanakuja kuliko sie tunavyokwenda. Ni nini sasa kinasababisha?
1.Hatuna wachezaji wengi wenye viwango vya kuwashawishi wenzetu. Na ndo maana utaona wanaturuka sie na badala yake wanaamua kwenda nchi zenye wachezaji wenye uwezo na vipaji kuliko wale walionao wao mf.Zimbabwe,Zambia,Sudani,Ethiopia n.k 2.Wachezaji wetu si washindani wa mafanikio. Wenzetu ni watu wa kutafuta mafanikio na kujituma sana, wakati wenzao wanacheza kazi kazi sisi wa kwetu wanacheza like for funny,show game bila kujali matokeo. Sasa hata tukisema tuzuie mapro, kimsingi haitawasaidia watu wa hivi badala yake itawaumiza Yanga ambao katika mashindano yao wanakutana na timu zinazoundwa na mapro wa maana kutoka nchi kibao.Tuelewe sahivi mpira ni kazi na ajira, kuwabeba wachezaji wa ndani wasiojitambua, wasiojituma, wasiojua maana ya timing ni kuviumiza vilabu vinavyoshiriki mashindano, hivi vilabu vinataka matokeo, vinataka mafanikio na ili wayapate haya ni lazima watafute watu wenye kuelewa nini maana ya kazi. Brazil hawazuii wachezaji kwenda kwao ila kwasababu wabrazili wanaeleweka kwa soka lao ndo maana utakuta kila club Ulaya kote kuna wabrazili lukuki,na nyinyi tengenezeni utaratibu wa kuwa na wachezaji wanouzika na kuitwa nje kulikoni mnaandaa mazingira ya kuzuia mapro eti ndo njia ya kukuza soka letu. Mkiwekeza kwenye academs ni dhairi mtapata wachezaji wanaofaa soko la ndani na muda si mrefu majirani zetu watakuja kununua vifaa kutoka Tz.